PreGE2025 Selasini: Kuzuia uchaguzi usifanyike ni 'ndoto za mchana'

PreGE2025 Selasini: Kuzuia uchaguzi usifanyike ni 'ndoto za mchana'

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Chama cha NCCR Mageuzi kimeeleza kuwa hakitasusia uchaguzi Mkuu wa baadae mwaka huu, wakieleza wazi pia mpango wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kutaka kuzuia uchaguzi ni suala ambalo haliwezekani.

Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa, Joseph Selasini amekiri kusema kuwa kuzuia uchaguzi ni ndoto za mchana zisizoweza kutimia, akisema Chadema pia imeshindwa kuwa na mkakati wa wazi katika kueleza ni namna gani watazuia uchaguzi, akisisitiza umuhimu wa kujiepusha na baadhi ya maneno nyakati hizi za maandalizi ya uchaguzi kwani zitakiweka Chama na Wanasiasa wao kwenye nafasi mbaya mbele ya vyombo vya dola.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Alipoulizwa na Mwandishi wa Jambo TV kuhusu matumizi ya nguvu ya Umma kwenye kuuzuia uchaguzi,Selasini ameeleza kuwa hakuna chama chenye uhakika wa matumizi ya nguvu ya umma, akikumbusha namna ambavyo kumetokea mfululizo wa maandamano kufeli yaliyokuwa yakiitishwa na vyama vya upinzani nchini.

Source: Jambo TV
 
Siasa bwana. Hii NCCR hii,, Tumewahi sukuma gari/shangingi ya Mrema ikiwa silencer kwa umbali kama Km 10 hivi.. tukiwa vijana enzi hizo. Watu kibao mzee 😁

Kweli Mrema alijua kucheza na akili zetu. Nikisikiaga neno NCCR-Mageuzi waga nakumbuka mbali na kufikiria mengi sana.😁 gone are the days
 
Siasa bwana. Hii NCCR hii,, Tumewahi sukuma gari/shangingi ya Mrema ikiwa silencer kwa umbali kama Km 50 hivi.. tukiwa vijana enzi hizo. Watu kibao mzee 😁

Kweli Mrema alijua kucheza na akili zetu. Nikisikiaga neno NCCR-Mageuzi waga nakumbuka mbali na kufikiria mengi sana.😁 gone are the days
Mzee KM 50?
 
Huyo Mzee ni tapeli fulani. Linataka hela ya CCM.
 
..Na vyama vya upinzani kushinda uchaguzi, bila Reforms, kwa Sheria na Tume iliyoko sasa hivi, ni ndoto za mchana.
 
Selasini ni aina ya wanasiasa njaa wasakatonge katika Taifa hili Wanasiasa wa aina hii tuwaepuke ka UKOMA.
 
Back
Top Bottom