raia_mwema
JF-Expert Member
- Oct 10, 2012
- 479
- 314
Binafsi nachukua nafasi hii kuipongeza serikali ya JMTZ kwa kuanzisha sekretarieti ya ajira ambayo kwa kiasi kikubwa imepunguza matatizo mengi yaliyokuwa yamegubika katika sekta ya ajira hapa nchini kwetu.
1.Napenda kushauri sekretarieti hiyo ijaribu kuangalia uwezekeno wa kujigawa kikanda na sahili zifanyike katika kanda kulingana na jografia ya nchi yetu ili kuwaepushia vijana gharama kubwa na safari ndefu za kwenda Dar es salam kufanya usahili.
2.Napenda uishauri pia tume hiyo kuwa kwa upande wa utumaji wa maombi ya ajira, pangetengenzwa mfumo wa kompyuta ili kuwawezesha waombaji kujisajili na kutuma maombi yao kupitia mtandao kwani kwa sasa wataalamu wa IT wapo wengi hivyo ni kitu kirahisi sana kuwa na mfumo wa aina hiyo. ikionekana kuwa wazo ilo linafaa hata mimi binafsi nipo tayari kujitolea kuandaa mfumo huu ambao utawasaidia waomboaji wengi
1.Napenda kushauri sekretarieti hiyo ijaribu kuangalia uwezekeno wa kujigawa kikanda na sahili zifanyike katika kanda kulingana na jografia ya nchi yetu ili kuwaepushia vijana gharama kubwa na safari ndefu za kwenda Dar es salam kufanya usahili.
2.Napenda uishauri pia tume hiyo kuwa kwa upande wa utumaji wa maombi ya ajira, pangetengenzwa mfumo wa kompyuta ili kuwawezesha waombaji kujisajili na kutuma maombi yao kupitia mtandao kwani kwa sasa wataalamu wa IT wapo wengi hivyo ni kitu kirahisi sana kuwa na mfumo wa aina hiyo. ikionekana kuwa wazo ilo linafaa hata mimi binafsi nipo tayari kujitolea kuandaa mfumo huu ambao utawasaidia waomboaji wengi