Scorpion anayetoboa watu Macho Buguruni, akamatwa

Scorpion anayetoboa watu Macho Buguruni, akamatwa

Kuhusiana na tukio la Hekaheka ya jana kuhusu Mwanaume mmoja mkazi wa Ubungo Makuburi Saidi almaarufu baba D kujeruhiwa vibaya na kutolewa macho na Mbabe mmoja wa Buguruni anayejiita Scorpion tena mbele za watu na hakuna hata mmoja aliyejitokeza kumsaidia kwa madai ya kamba huyo Scorpion anaogopeka na watu wote maeneo hayo ya buguruni.

Idara ya Hekaheka ikishirikiana na website yako pendwa geahhabibu.co.tz imefika eneo la Buguruni kwa mnyamani ambapo ndipo tukio hilo lilifanyika nakuweza kuongea na baadhi ya wananchi wa waeneo hilo kutaka kujua zaidi kuhusiana na huyo jamaa anayejiita scorpion imekuaje mpaka mtu anapigwa hadi kutolewa macho mbele yao bila wao kutetea chochote.

Wengi wao hawakuwa tayari kumuongelea kutokana na hofu waliokuwa nayo juu ya mtu huyo na hata hao waliokubali walijikuta wakielezea kwa kujificha bila kutaka kujulikana.

Wakazi hao wa Buguruni walidai kuwa jamaa ni mtaalamu wa mambo ya ngumi na huwa haogopi mtu yoyote hata mkienda wengi yeye ndio anafurahi.Vilevile walieleza kuwa hilo ni tukio lake la tatu la kumjeruhi mtu na kumtoa macho alishawahi kumvunja kiuno na mkono mwanamke mmoja.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Salum Hamdani amethibitisha kukamatwa kwa jamaa huyo ambapo anasema kwa sasa yupo ndani Magereza na kesi yake itasomwa tena tarehe 5 mwezi wa 10 2016.

Ni kweli hilo tukio limetokea na polisi tayari walishachukua hatua kwa maana ya huyo mtuhumiwa Scorpion jina lake halisi anaitwa Salum Mpepe alikamatwa siku ya tarehe 12 mwezi wa 9 akawa pale kituo cha polisi Buguruni wakati upelelezi ukiendelea tarehe 23 mwezi wa 9 alifikishwa mahakami na kusomewa jinai namba 276 unyanganyi kwa kutumia silaha, yupo magereza kesi yake itatajwa tena tarehe 5 mwezi wa 10 2016.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe.Paul Makonda zimemfika taarifa hizi ambapo yeye pamoja na Idara ya Hekaheka kupitia Leoetena ya Cloudsfm tutaungana kwa pamoja siku ya jumapili saa tisa jioni kwenda kuongea na wakazi wa Buguruni ili kuweka sawa mambo haya ya uhalifu yanayoendelea mtaani
Nice work sa huyo bwege serikali si Ingemnyoosha tu
 
Wanajamvi tuache sheria ichukue mkondo wake na kuhamasisha wananchi wakatoe ushahidi ili apatikane na hatia huyo asiye na tofauti na gaidi
 
Kuhusiana na tukio la Hekaheka ya jana kuhusu Mwanaume mmoja mkazi wa Ubungo Makuburi Saidi almaarufu baba D kujeruhiwa vibaya na kutolewa macho na Mbabe mmoja wa Buguruni anayejiita Scorpion tena mbele za watu na hakuna hata mmoja aliyejitokeza kumsaidia kwa madai ya kamba huyo Scorpion anaogopeka na watu wote maeneo hayo ya buguruni.

Idara ya Hekaheka ikishirikiana na website yako pendwa geahhabibu.co.tz imefika eneo la Buguruni kwa mnyamani ambapo ndipo tukio hilo lilifanyika nakuweza kuongea na baadhi ya wananchi wa waeneo hilo kutaka kujua zaidi kuhusiana na huyo jamaa anayejiita scorpion imekuaje mpaka mtu anapigwa hadi kutolewa macho mbele yao bila wao kutetea chochote.

Wengi wao hawakuwa tayari kumuongelea kutokana na hofu waliokuwa nayo juu ya mtu huyo na hata hao waliokubali walijikuta wakielezea kwa kujificha bila kutaka kujulikana.

Wakazi hao wa Buguruni walidai kuwa jamaa ni mtaalamu wa mambo ya ngumi na huwa haogopi mtu yoyote hata mkienda wengi yeye ndio anafurahi.Vilevile walieleza kuwa hilo ni tukio lake la tatu la kumjeruhi mtu na kumtoa macho alishawahi kumvunja kiuno na mkono mwanamke mmoja.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Salum Hamdani amethibitisha kukamatwa kwa jamaa huyo ambapo anasema kwa sasa yupo ndani Magereza na kesi yake itasomwa tena tarehe 5 mwezi wa 10 2016.

Ni kweli hilo tukio limetokea na polisi tayari walishachukua hatua kwa maana ya huyo mtuhumiwa Scorpion jina lake halisi anaitwa Salum Mpepe alikamatwa siku ya tarehe 12 mwezi wa 9 akawa pale kituo cha polisi Buguruni wakati upelelezi ukiendelea tarehe 23 mwezi wa 9 alifikishwa mahakami na kusomewa jinai namba 276 unyanganyi kwa kutumia silaha, yupo magereza kesi yake itatajwa tena tarehe 5 mwezi wa 10 2016.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe.Paul Makonda zimemfika taarifa hizi ambapo yeye pamoja na Idara ya Hekaheka kupitia Leoetena ya Cloudsfm tutaungana kwa pamoja siku ya jumapili saa tisa jioni kwenda kuongea na wakazi wa Buguruni ili kuweka sawa mambo haya ya uhalifu yanayoendelea mtaani

Acheni kumuogopa na kumpamba huyu sijui SCORPION wenu huko Buguruni na kusema kuwa hakamatiki. Sidhani kama huyo SCORPION wenu anafikia ' UKATILI ' wa Mtu mmoja ' TISHIO ' na ' HATARI ' anaitwa MBUZI YAKE KAMBA aliyekuwa akitikisa Kawe nzima na vitongoji vyake na kuna wakati kwa Uwoga tu Watu walikuwa wakipishana nae barabarani wanamsalimu na kumwambia tafadhali MBUZI YAKE KAMBA leo nina Simu nzuri na HELA mfukoni chukua tu. Kwa wale waishio KAWE nadhani watakuwa wanaelewa ninachokisema kwani huyu Jamaa hata Police tu wa Kawe walikuwa wanamwogopa ila tunashukuru kwa ujio wa Kamanda mpya SIRO na Mkuu mpya wa Kituo cha Kawe kwa kushirikiana na Wananchi kadhaa waliojitoa mhanga walishirikiana hadi wakafanikiwa kumkamata huyo MBUZI YAKE KAMBA na sasa yupo SEGADANSI nadhani Ukonga au Keko.

Hakuna MAASI ambayo huyu Jamaa MBUZI YAKE KAMBA wa Kawe hajayafanya na nakumbuka hata siku ile alipokamatwa tu sehemu mbalimbali za Kawe Wakazi walikuwa wakifanya Sherehe na kuna hata baadhi ya Police walisikika wakisema kuwa sasa WATAPUMUA. Nimeshamfuatilia huyo SCORPION wenu ila kwa aliyokuwa anawafanyia wana Buguruni miaka hii ya karibuni mwenzake MBUZI YAKE KAMBA wa huku Kawe aliyafanya miaka kumi ( 10 ) iliyopita.

Huyo SCORPION wala hashindikani kukamatika au kuchukuliwa hatua ila inaonyesha dhahiri kuwa nyie Wakazi wa Buguruni hamna Ushirikiano halafu yawezekana pia kuna Mtu au Mamlaka fulani inamlinda kwa minajili kuwa labda wanakula nae pale anapofanikisha ' tukio ' fulani lenye ' mtonyo ' wa maana. Nijuavyo Buguruni ndiko kumejaa ' Masela ' wa maana sasa inakuwaje mnlishindwa au mnashindwa kumdhibiti huyo SCORPION wenu?
 
Utadhani yeye hajui kwamba naye atakufa siku moja tu
 
Kwahiyo jamaa kawa kipofu kabisa? kama ndivyo kwanini na huyu anayejifanya mbabe asimwagiwe tu tindikali usoni then wakamuacha ili aone mateso yake.
 
Kisheria when attacked or provoked hutakiwi kuretaliate iyo ni kazi ya vyombo vya dola. Nadhan ndio maana watu wabugurun walisita kumchukulia hatua.

Pia kisheria ni polisi pekee yake mwenye uniform ndie anahusika kumtia nguvun mtuhumiwa.
 
Vituko kweli wanaumeeee....... eee
Mapanga...
 
Yapaswa tuangazie sheria za kunyonga huu ni ujinga mashtaka ya nini mjinga kama huyo ni wa Kunyonga au kuuawa Kwa namna yoyote .
Inauma sana .
 
Back
Top Bottom