njiwaji
JF-Expert Member
- Jul 15, 2015
- 289
- 209
Sayari 4 ziko katika mstari angani na Mwezi unazikaribia kati ya 14 hadi 23 Agosti 2018
Zuhura (Venus), Mshtarii (Jupiter), Zohali (Saturn) na Mirihi (Mars) zinaonekana angani zikiwa katika mstari mnyoofu kutoka magharibi kwenda mashariki na Mwezi unazikaribia kati ya tarehe 14 hadi 23 Agosti, 2018.
Muda wa kuziona sayari zote hizi ni kuanzia saa moja. Zuhura itatua magharibi na kupotea baada ya saa tatu.
Sayari huonekana kama nyota angani kwa hiyo namna ya kutofauitsha ni kwa mn'gao wake. Sayari ya Zuhura (Venus) inawaka kabisa kwa unjano upande wa magharibi wakati Mirihi (Mars) inamulika kwa rangi nyekundu upande wa mashariki.
Mshtarii (Jupiter) inan'gaa sana utosini.
Mn'gao wa Zohali (Saturn) ni mkali lakini ni sawa na nyota zingine. Kwa hiyo namna ya kutofautisha ni kwamba mwanga wa sayari zote haumeremeti kama nyota za kawaida.
Kwa hiyo uangalie nyota kwa makini na kama haimeremeti basi ni sayari.
Zuhura (Venus), Mshtarii (Jupiter), Zohali (Saturn) na Mirihi (Mars) zinaonekana angani zikiwa katika mstari mnyoofu kutoka magharibi kwenda mashariki na Mwezi unazikaribia kati ya tarehe 14 hadi 23 Agosti, 2018.
Muda wa kuziona sayari zote hizi ni kuanzia saa moja. Zuhura itatua magharibi na kupotea baada ya saa tatu.
Sayari huonekana kama nyota angani kwa hiyo namna ya kutofauitsha ni kwa mn'gao wake. Sayari ya Zuhura (Venus) inawaka kabisa kwa unjano upande wa magharibi wakati Mirihi (Mars) inamulika kwa rangi nyekundu upande wa mashariki.
Mshtarii (Jupiter) inan'gaa sana utosini.
Mn'gao wa Zohali (Saturn) ni mkali lakini ni sawa na nyota zingine. Kwa hiyo namna ya kutofautisha ni kwamba mwanga wa sayari zote haumeremeti kama nyota za kawaida.
Kwa hiyo uangalie nyota kwa makini na kama haimeremeti basi ni sayari.