Chama cha Sauti ya Uma-SAU kimesema kimeshtushwa na uteuzi wa Mkiti wa NCCR James Mbatia kuwa mbunge,uteuzi uliofanywa na Mkiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete.
Mwenyekiti wa SAU Paul Kyara alisema hata mtoto mdogo atatambua kwamba Mbatia anakwenda kutetea CCM bungeni na kupambana na upinzani.
Kiongozi huyo wa SAU pia ameunga mkono kauli ya Mbunge wa Nyamagana Ezekiah Wenje aliyotoa kwamba Mbatia ni kibaraka wa CCM. Amesema ili kurejesha heshima yake ni bora Mbatia ajiuzulu uenyekiti wa NCCR ili apate muda mzuri wa kutetea hoja za serikali bungeni.
Source:Tanzania Daima Alhamisi.
Mwenyekiti wa SAU Paul Kyara alisema hata mtoto mdogo atatambua kwamba Mbatia anakwenda kutetea CCM bungeni na kupambana na upinzani.
Kiongozi huyo wa SAU pia ameunga mkono kauli ya Mbunge wa Nyamagana Ezekiah Wenje aliyotoa kwamba Mbatia ni kibaraka wa CCM. Amesema ili kurejesha heshima yake ni bora Mbatia ajiuzulu uenyekiti wa NCCR ili apate muda mzuri wa kutetea hoja za serikali bungeni.
Source:Tanzania Daima Alhamisi.