MakinikiA
JF-Expert Member
- Jun 7, 2017
- 5,692
- 7,864
Tuelekee kule Hormuz
Iran imetangaza kuwa jeshi lake litashambulia majeshi ya Marekani endapo yatajaribu kuingia katika Mlango wa Hormuz, kufuatia tangazo la Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu operesheni ya kusaidia meli kupita katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi la Iran kupitia kituo cha utangazaji cha taifa IRIB, mkuu wa kamandi ya kijeshi amesema kuwa Iran itashambulia “kikosi chochote cha kijeshi cha kigeni” kitakachokaribia au kuingia katika mlango huo, hasa majeshi ya Marekani ambayo ameyaita ya “uchokozi”.
Meja Jenerali Ali Abdollahi amesema Iran imekuwa ikisisitiza mara kwa mara kuwa Mlango wa Hormuz uko chini ya udhibiti wa majeshi yake, na kwamba usafiri salama katika eneo hilo lazima uratibiwe na Tehran chini ya masharti yote.
Tishio hilo linakuja baada ya Marekani kutangaza operesheni iitwayo “Project Freedom”, ambayo itahusisha meli za kivita, ndege zaidi ya 100, mifumo ya droni pamoja na wanajeshi takriban 15,000 kusaidia kulinda usafirishaji katika eneo hilo nyeti la Bahari ya Ghuba.
Mvutano kati ya mataifa hayo mawili umeendelea kuongezeka, huku Mlango wa Hormuz ukiwa njia muhimu ya usafirishaji wa mafuta duniani, na hivyo kufanya hali hiyo kuwa na athari kubwa kimataifa endapo itazidi kushadidi.
Jinsi Iran Ilivyogeuza Mlango wa Hormuz kuwa silaha yenye nguvu zaidi duniani
Mlango Hormuz: Hatari ya mabomu ya baharini ni ipi na kwa nini kuyaondoa n