Sasa nimejua: CHADEMA ndilo Tumaini la Kweli

Sasa nimejua: CHADEMA ndilo Tumaini la Kweli

MPANDA Jr

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2011
Posts
1,295
Reaction score
159
WaTz wenzangu, nimetafakari na kupata majibu haya:

1. Tumekuwa wepesi sana kukihukumu chama cha CHADEMA kwa maelekezo ya CCM, tena kwa mambo ya kutunga tu!

2. Tumekuwa wepesi sana kuvunjwa moyo juu ya safari yetu ya mabadiliko inayoongozwa na CHADEMA kwa kutishiwa na CCM, ambao ndio sababu ya matatizo mengi yasiyotatulika ktk nch yetu

3. Tumekuwa wepesi kulishwa maneno ya uongo na CCM dhidi ya CHADEMA halafu cha ajabu kuna baadhi yetu wanayasadiki na kuyashikia BANGO.

Ni vema tukajua kwamba, katka vita hii ndani ya taifa letu dhidi ya UFISADI, RUSHWA (Kikwete amekiri kwamba CCM imejaa rushwa), DHULUMA, UBABE, UPORAJI WA RASILIMALI, UJANGILI nk. maadui zetu hawawezi kukaa kimya! Ni lazma nao watatafuta mbinu za kutushambulia. Lakin TOFAUTI YETU ni kwamba wao (CCM) wanatumia mbinu za uongo, sisi (CHADEMA) tunasema kweli Daima.

Pia tujue hata katika kazi ya MUNGU wasaliti hawakosekani. Sisi ni nani tusisalitiwe? Kama YESU KRISTO alisalitiwa na Mwanakamati wake (YUDA) sembuse CHADEMA?

TUTASHINDA
 
Kwa hiyo maneno ya Lema katumwa na CCM aje ayaseme kwenye mitandao?
 
Nimesikitishwa sana na CHADEMA kukaa kimya bila kuchukua hatua yoyote kuhusu kauli za Sophia Simba,alizotoa akiwa huko nyanda za juu kusini - Mbeya, kukashifu chadema, Naomba nifahamu iwapo kuna hatua yoyote ilichukuliwa kwa kauli hizo "zilizo kituhumu chama kwa harakati zake , pamoja na kashfa za moja kwa moja kwenda na Mh. - Simon Mbilinyi"
 
Nimesikitishwa sana na CHADEMA kukaa kimya bila kuchukua hatua yoyote kuhusu kauli za Sophia Simba,alizotoa akiwa huko nyanda za juu kusini - Mbeya, kukashifu chadema, kama kuna hatua yoyote ilichukuliwa kwa kauli hizo "zilitumu chama na mbuge - Simon Mbilinyi" naomba nifahamishwe

Mbunge wa Mbeya anaitwa "Joseph Mbilinyi" sio "Simon...". Lakin kuhusu maneno ya Sophia, ni kwamba Chama kilijibu tuhuma lakin tayari wananchi walishawapuuza hao maccm. Hawawezi kutuamulia jinsi ya kuendesha Chama chetu.
 
Kuna maneno hua nikiyasikia nafarijika sana.

well said kamanda.
kama yesu ambaye hakuwahi ku
tenda dhambi ailsalitiwa kwa vipande thelathini tu vya fedha tena na mtu aliyeshinda naye masaa yote wakifarijiana na kushauriana vipi Cdm ambayo viongozi wake huingizwa kwenye mitego ya mamilioni ya pesa...

ATAKAYEVUMILIA MPAKA MWISHO NDIYE ATAKAYEOKOKA!
 
Asante kwa marekebisho ya jina la Mhe.... kuwa ni Joseph badala ya Simon,

ila kama Hoja za Sophia Simba zilijibiwa basi haikuwa kwa wino mnene sana, mie napata shinda kumuweka sawa Bibi yangu (M-UWT)ambaye bado anaamini kuwa alichokisema mwenyekiti wao kuhusu CHADEMA ni sahihi
Mbunge wa Mbeya anaitwa "Joseph Mbilinyi" sio "Simon...". Lakin kuhusu maneno ya Sophia, ni kwamba Chama kilijibu tuhuma lakin tayari wananchi walishawapuuza hao maccm. Hawawezi kutuamulia jinsi ya kuendesha Chama chetu.
 
viongozi wa juu Wa Chadema inabidi watolee ufafanuzi mzuri juu ya tuhuma mbalimbali sio kusema kuna wasaliti alaf hawatajwi sasa hapa tofauti ya CCM na Cdm iko wapi kama wote wako theoritically tena kwa hapa ni bora hata na CCM maana nzuri ni hii kama kweli CDM ni mbadala wa ccm alaf hakuna mfumo thabiti wa kuleta iman kwa watu na kuwa na uwazi ktk kazi zake hapa utabaki na Bendi isiyo kuwa na wachezaji maana wachezaji wamechoka hawaoni improvement ndani ya Bendi yao Viongozi wenye asili ya kaskazin ndani ya CHADEMA ifike mheshimu mawazo ya wenzanu maana wote mmekuwa wasemaji na kila mtu anasema anavyojisikia bila hofu wala woga Tafakari chukuwa hatua ni WAKATI MGUMU SANA KWA SASA NDANI YA CDM ongeeni na watz watambue malengo ya chama sio shutuma hizi tulishachoka daily ndani ya ccm tena nyie mnafanya yale yale,,,,well done Slaa,zitto,marando,and others God may bless them
 
Kwahiyo mwigamba,lema,shonza,mtela,bavicha mpanda,mbeya nk wote hawa walitumwa na ccm kuleta mvutano ndani ya chadema,
kunawatu sijui nani anawaza kwa niaba yao.
 
viongozi wa juu Wa Chadema inabidi watolee ufafanuzi mzuri juu ya tuhuma mbalimbali sio kusema kuna wasaliti alaf hawatajwi sasa hapa tofauti ya CCM na Cdm iko wapi kama wote wako theoritically tena kwa hapa ni bora hata na CCM maana nzuri ni hii kama kweli CDM ni mbadala wa ccm alaf hakuna mfumo thabiti wa kuleta iman kwa watu na kuwa na uwazi ktk kazi zake hapa utabaki na Bendi isiyo kuwa na wachezaji maana wachezaji wamechoka hawaoni improvement ndani ya Bendi yao Viongozi wenye asili ya kaskazin ndani ya CHADEMA ifike mheshimu mawazo ya wenzanu maana wote mmekuwa wasemaji na kila mtu anasema anavyojisikia bila hofu wala woga Tafakari chukuwa hatua ni WAKATI MGUMU SANA KWA SASA NDANI YA CDM ongeeni na watz watambue malengo ya chama sio shutuma hizi tulishachoka daily ndani ya ccm tena nyie mnafanya yale yale,,,,well done Slaa,zitto,marando,and others God may bless them
Yawezekana viongozi kutoka kaskazini ndiyo wanaakili na maono ya mbali wengine hawana akili na maono ya mbali.
 
Asante kwa marekebisho ya jina la Mhe.... kuwa ni Joseph badala ya Simon,

ila kama Hoja za Sophia Simba zilijibiwa basi haikuwa kwa wino mnene sana, mie napata shinda kumuweka sawa Bibi yangu (M-UWT)ambaye bado anaamini kuwa alichokisema mwenyekiti wao kuhusu CHADEMA ni sahihi
Kwanza kuwa na adabu kwa bibi yako unataka kumweka sawa bibi yako kweli utamaduni wetu umekwisha kama vijana wa bavicha mmefika mahala hapo basi tena.

Pili mambo aliyosema sofia simba ni ya kweli kila mtu anajua kuwa hayo yaliyosemwa chadema ndiyo zao.
 
mkuu ukiwa unasafiri baharini kuna mambo mengi utakutana nayo na inabidi uyakabili. Kwa mfano baharini kuna papa nyanguni na kubwa kuliko yote ni dhoruba kali za mara kwa mara. Kwa sisi watumiaji wa bahari yote hayo yanakufanya uhimalishe chombo chako unachotumia na si kuacha kazi ya uvuvi. CDM karabatini chama chenu na kama kuna mbao mbovu ziondoeni.
Mungu awbariki sana na aibariki TZ.
 
Yawezekana viongozi kutoka kaskazini ndiyo wanaakili na maono ya mbali wengine hawana akili na maono ya mbali.

Unajiskijia raha sana kuzungumzia ukabila???? Acha hizo.. Sisi wote ni kitu kimoja ndiyo sababu wote tunatoka kwa mwanamke na mwisho wa siku tunarudi mavumbini... Hebu zungumzia tofauti ya waliokuwa nacho na wasiokua nacho ndani ya CCM.... Au wote mnkwanja sawa????
 
Kasome thread ya Lema ndo uje uendelee kutoa allegation zako

Unaongea too general. Hakuna cha ajabu alichosema Lema zaidi ya ukweli mchungu. Lema hajatumia ID feki, nzuri zaidi amesimama upande wa chama... Mimi nimeeleza namna nyie MACCM mnavyotaka kutake advantage kupandikiza uzush na uongo. Stay far
 
Unaongea too general. Hakuna cha ajabu alichosema Lema zaidi ya ukweli mchungu. Lema hajatumia ID feki, nzuri zaidi amesimama upande wa chama... Mimi nimeeleza namna nyie MACCM mnavyotaka kutake advantage kupandikiza uzush na uongo. Stay far

ubabe, unafiki, uzushi na uzandiki wa nyinyiem uko ukingoni. nguvu inayotumika kukiangamiza CHADEMA ingetumika kututatulia matatizo na kero zetu, hakika TZ tungekuwa tumeendelea sana. CCM imepoteza mwelekeo. wajadili hoja ya Lema: POSHO WANAZOPATA ZICHAGIZE KUPIGANIA MASLAHI YA WATUMISHI WENGINE NCHINI.
 
Back
Top Bottom