Sasa ni wazi kwamba CCM ni Dhaifu

Mindi

JF-Expert Member
Apr 5, 2008
3,523
4,991
Inaonekana mastratejisti wa CCM hawajaelewa uzito wa Waraka wa Makatibu wakuu wastaafu wa CCM, wazee Kinana na Makamba. Ukiusoma huo waraka katika hali ya kawaida tu, utaona kwamba waliouandika ni watu wenye weledi na wametafakari sana na kuchagua maneno na sentensi za kutumia. kuna strateji nyingi sana zinazofikirisha. nitataja baadhi tu. kwamba waraka umeelekezwa kwa baraza la ushauri pia ni strateji. Kwamba barua imewekwa wazi hadharani, nayo ni strateji.

Kilichotarajiwa ni kwamba wahusika ndani ya CCM nao wangetafakari sana. moja ya hatua za haraka ingekuwa ni kuwapongeza hao walioandika waraka, kwamba wametumia haki yao ndani ya chama, na kwamba chama cha CCM kama Baba wa Demokrasia, kitafanyia kazi malalamiko yao kwa mujibu wa taratibu za chama. umuhimu wa kauli ya namna hii ni kuliondoa SAKATA hili kwenye uwanja wa nje na kulileta ndani ya chama. Hii ingesaidia kukipa chama nafasi ya kurekebisha makosa yaliyofanywa kwa kuwaruhusu akina Musiba wakitumbukize chama kwenye UVUNDO.

Kinyume chake, tumeshuhudia ubabaishaji na ukosefu wa weledi na umakini, wa kiwango cha juu kuwahi kuonekana. Katika mwendelezo wa utendaji wa KIBASHITE, zimeonekana clip zikiwa na udukuzi wa mawasiliano kati ya akina Nape, Kinana, Mzee Makamba, Ngeleja, Membe, nk. Nadhani lengo hapa ni KUWAZODOA na KUWAANIKA akina Kinana na Makamba na hivyo kutia mchanga kwenye waraka wao. Hili ni kosa kubwa sana kistrateji.

Kwanza kuna matatizo mengi ya kisheria kwenye udukuzi huo, ambao unaleta complications nyingi sana. Pili inathibitisha kwamba kweli CCM inatumia MBWA KOKO kufanya kazi zake, na kuwahalalisha hao MBWA KOKO wote kwamba wanatumwa. hata kauli ya Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ali, inaonekana kuthibitisha kwamba chama kinatumia magenge machafu. Hatujaona akina Musiba wakikemewa, lakini kwa kuwakemea walalamikaji, inathibitisha madai ya Waraka kwamba hawa akina Musiba wanalindwa na hawawezi kuguswa na mtu yeyote au taasisi yoyote ya hapa nchini. Pia Bashiru anaonekana kutumia maneno ya kwenye hizo clip kutoa matamko na makemeo yake. kwa hiyo hizo clip ni kama zimetolewa IN ADVANCE ili kusafisha njia.

Tatu, hizo Clip zinatoa ujumbe mwingi sana tofauti na malengo ya waliozirusha. Kama kweli watendaji wakuu wastaafu wa CCM wanaweza kudukuliwa, ni fedheha kubwa kwa CCM. CCM ina sifa ya kulinda wastaafu wake. Leo kulikoni? na mbaya zaidi, kwa kusikika hadharani wakiongea hayo wanayoongea, ni ishara kwamba CCM ipo kwenye hali mbaya sana. EEeee, unawezaje sasa ukainuka na kudai kwamba CCM ni imara, kama watangulizi wako na wasaidizi wao, tena wanaokuzidi kwa ukongwe na weledi katika kukitumikia chama, wamefikia hatua ya kukata tamaa kiasi hicho, na kutaharuki kiasi hicho? Yaani CCM inaruhusu watu wa ngazi za juu hivyo kusikika hadharani wakitoa ya moyoni? huo ni upungufu mkubwa sana hata kijasusi. Kwa kweli kitendo cha kutoa clip hizi kumewathibitisha hao watendaji wakuu na kuimarisha madai yao, na kwa upande mwingine, kimefichua uchafu wa ndani kabisa wa CCM kwa namna ambayo haijawahi kutokea.

Lakini kuna kitu kibaya zaidi ya yote hayo kilichofichuliwa kwenye hizo clip, kiasi kwamba naanza kuhisi kwamba pengine aliyefanya hivyo ana akili zaidi kwa maana kwamba ana lengo la kumhujumu bosi wake kwa kumwanika hadharani!!! Kitu hicho ni kumhusisha Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, kwamba naye ameonesha kukerwa na hali ya mambo ilivyo. Sasa tunajua kwamba Rais Mkapa aliwahi kumkosoa Magufuli hadharani siku ambayo watendaji wakuu wastaafu waliiitwa ikulu na Rais Magufuli. Mkapa alisema kwamba hii ni Serikali ya CCM, na siyo ya fulani. sasa tunajua kwamba Mkapa ndiye BABA MLEZI wa Magufuli. kama naye ana kichefuchefu, basi hali ni mbaya sana

Hapa naona jambo moja tu linaloniingia akilini. Mastratejisti wa CCM wamewekwa pembeni na ni Magu Mwenyewe anayeshika usukani na kuelekeza nini kifanyike. hiyo ndiyo consistency ninayoiona katika madhila mbalimbali yanayoikuta nchi yetu hivi sasa. Najiuliza CCM inajua inakokwenda? lakini mbaya zaidi, Taifa la Tanzania linakwenda wapi?

Sasa tunashuhudia msururu wa wachumia tumbo lukuki wakimsifu Magufuli. lakini ukweli tumeujua. Ni wakati muafaka watanzania tuwe na msimamo kama CAG Prof. Assad. Tutetee maslahi ya Taifa letu, ambayo siyo maslahi ya Magufuli
 
Kabati linatakiwa kutunza vilivyomo ndani. kama vinagongana hovyo na kuvunjika, huo uimara wa kabati utatoka wapi na utakuwa na maana gani?

Tatizo la mpangilio wa vyombo ni tatizo la mpangaji sio kabati lenyewe
 
Tatizo la mpangilio wa vyombo ni tatizo la mpangaji sio kabati lenyewe
Hapo tupo pamoja kabisa. Kwa hiyo sasa ni uimara wa MPANGAJI wa vyombo kabatini ndio kitu muhimu. MPANGAJI wetu wa vyombo ni tatizo. Tufanyeje?
 
Nimependa ujengaji wako wa hoja. Nitatofautiana na wewe kweye hoja moja tu.

Naamini Magufuli pamoja na kuwa ndiye mwenye maono ya kiujumla kuhusu nini anataka kufanya, anaye 'mpanga mikakati' ingawa wote hatumjui ni nani na siyo hawa tunaowanyoosheaga vidole kila siku.
 
Inaonekana mastratejisti wa CCM hawajaelewa uzito wa Waraka wa Makatibu wakuu wastaafu wa CCM, wazee Kinana na Makamba. Ukiusoma huo waraka katika hali ya kawaida tu, utaona kwamba waliouandika ni watu wenye weledi na wametafakari sana na kuchagua maneno na sentensi za kutumia. kuna strateji nyingi sana zinazofikirisha. nitataja baadhi tu. kwamba waraka umeelekezwa kwa baraza la ushauri pia ni strateji. Kwamba barua imewekwa wazi hadharani, nayo ni strateji.

Kilichotarajiwa ni kwamba wahusika ndani ya CCM nao wangetafakari sana. moja ya hatua za haraka ingekuwa ni kuwapongeza hao walioandika waraka, kwamba wametumia haki yao ndani ya chama, na kwamba chama cha CCM kama Baba wa Demokrasia, kitafanyia kazi malalamiko yao kwa mujibu wa taratibu za chama. umuhimu wa kauli ya namna hii ni kuliondoa SAKATA hili kwenye uwanja wa nje na kulileta ndani ya chama. Hii ingesaidia kukipa chama nafasi ya kurekebisha makosa yaliyofanywa kwa kuwaruhusu akina Musiba wakitumbukize chama kwenye UVUNDO.

Kinyume chake, tumeshuhudia ubabaishaji na ukosefu wa weledi na umakini, wa kiwango cha juu kuwahi kuonekana. Katika mwendelezo wa utendaji wa KIBASHITE, zimeonekana clip zikiwa na udukuzi wa mawasiliano kati ya akina Nape, Kinana, Mzee Makamba, Ngeleja, Membe, nk. Nadhani lengo hapa ni KUWAZODOA na KUWAANIKA akina Kinana na Makamba na hivyo kutia mchanga kwenye waraka wao. Hili ni kosa kubwa sana kistrateji.

Kwanza kuna matatizo mengi ya kisheria kwenye udukuzi huo, ambao unaleta complications nyingi sana. Pili inathibitisha kwamba kweli CCM inatumia MBWA KOKO kufanya kazi zake, na kuwahalalisha hao MBWA KOKO wote kwamba wanatumwa. hata kauli ya Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ali, inaonekana kuthibitisha kwamba chama kinatumia magenge machafu. Hatujaona akina Musiba wakikemewa, lakini kwa kuwakemea walalamikaji, inathibitisha madai ya Waraka kwamba hawa akina Musiba wanalindwa na hawawezi kuguswa na mtu yeyote au taasisi yoyote ya hapa nchini. Pia Bashiru anaonekana kutumia maneno ya kwenye hizo clip kutoa matamko na makemeo yake. kwa hiyo hizo clip ni kama zimetolewa IN ADVANCE ili kusafisha njia.

Tatu, hizo Clip zinatoa ujumbe mwingi sana tofauti na malengo ya waliozirusha. Kama kweli watendaji wakuu wastaafu wa CCM wanaweza kudukuliwa, ni fedheha kubwa kwa CCM. CCM ina sifa ya kulinda wastaafu wake. Leo kulikoni? na mbaya zaidi, kwa kusikika hadharani wakiongea hayo wanayoongea, ni ishara kwamba CCM ipo kwenye hali mbaya sana. EEeee, unawezaje sasa ukainuka na kudai kwamba CCM ni imara, kama watangulizi wako na wasaidizi wao, tena wanaokuzidi kwa ukongwe na weledi katika kukitumikia chama, wamefikia hatua ya kukata tamaa kiasi hicho, na kutaharuki kiasi hicho? Yaani CCM inaruhusu watu wa ngazi za juu hivyo kusikika hadharani wakitoa ya moyoni? huo ni upungufu mkubwa sana hata kijasusi. Kwa kweli kitendo cha kutoa clip hizi kumewathibitisha hao watendaji wakuu na kuimarisha madai yao, na kwa upande mwingine, kimefichua uchafu wa ndani kabisa wa CCM kwa namna ambayo haijawahi kutokea.

Lakini kuna kitu kibaya zaidi ya yote hayo kilichofichuliwa kwenye hizo clip, kiasi kwamba naanza kuhisi kwamba pengine aliyefanya hivyo ana akili zaidi kwa maana kwamba ana lengo la kumhujumu bosi wake kwa kumwanika hadharani!!! Kitu hicho ni kumhusisha Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, kwamba naye ameonesha kukerwa na hali ya mambo ilivyo. Sasa tunajua kwamba Rais Mkapa aliwahi kumkosoa Magufuli hadharani siku ambayo watendaji wakuu wastaafu waliiitwa ikulu na Rais Magufuli. Mkapa alisema kwamba hii ni Serikali ya CCM, na siyo ya fulani. sasa tunajua kwamba Mkapa ndiye BABA MLEZI wa Magufuli. kama naye ana kichefuchefu, basi hali ni mbaya sana

Hapa naona jambo moja tu linaloniingia akilini. Mastratejisti wa CCM wamewekwa pembeni na ni Magu Mwenyewe anayeshika usukani na kuelekeza nini kifanyike. hiyo ndiyo consistency ninayoiona katika madhila mbalimbali yanayoikuta nchi yetu hivi sasa. Najiuliza CCM inajua inakokwenda? lakini mbaya zaidi, Taifa la Tanzania linakwenda wapi?

Sasa tunashuhudia msururu wa wachumia tumbo lukuki wakimsifu Magufuli. lakini ukweli tumeujua. Ni wakati muafaka watanzania tuwe na msimamo kama CAG Prof. Assad. Tutetee maslahi ya Taifa letu, ambayo siyo maslahi ya Magufuli
Sisi kazi yetu ni kuchochea ili moto uendelee kuwaka ili hiki kichaka kinachoitwa ccm kiteketee kiishe kwa manufaa ya mama Tanzania,ninaumia sana pale ninapoona Kuna mtanzania anajaribu kuondoa kuni jikoni
 
Kinachonekana sasa hivi ni uongozi wa juu wa ccm kukosa busara na hekima eti makatibu wakuu wastaafu Kinana na Nape ni wapumbavu ,INA maana chama nilikuwa kinaongozwa na wapumbavu vipi wenyeviti wao na wana chama wao sio wapumbavu kwa hiyo ni chama cha wapumbavu. kwahiyo Bashiru kapokea chama toka kwa mpumbafu ,chama cha kipumbavu ,aisee reasoning ya viongozi wa sasa wa ccm ni ya ajabu sana .
 
Nimependa ujengaji wako wa hoja. Nitatofautiana na wewe kweye hoja moja tu.

Naamini Magufuli pamoja na kuwa ndiye mwenye maono ya kiujumla kuhusu nini anataka kufanya, anaye 'mpanga mikakati' ingawa wote hatumjui ni nani na siyo hawa tunaowanyoosheaga vidole kila siku.
Nashawishika kukubaliana na wewe, shida ni kwamba kama yeye Magufuli anaye huyo mshauri, basi atakuwa keshawabadilisha mara nyingi, kwa jinsi walivyomwingiza mkenge. vinginevyo ana udhaifu mkubwa zaidi kuliko inavyoonekana, kwamba hatambui madhara ya ushauri huo anaopewa.
 
Sisi kazi yetu ni kuchochea ili moto uendelee kuwaka ili hiki kichaka kinachoitwa ccm kiteketee kiishe kwa manufaa ya mama Tanzania,ninaumia sana pale ninapoona Kuna mtanzania anajaribu kuondoa kuni jikoni
Wala usiwe na wasiwasi mkuu, hawa jamaa hawana uwezo wa kuchambua mambo na kuona mbali. tayari wanateketea. tunahitaji kuwatia moyo wale wenye viberiti ili nao wawashe huko waliko
 
Chama imara lazima kiwe na migogoro bado sijaona mgogoro kama ule wa Lowassa na CCM ikabaki imara
Ni kweli migogoro ni lazima iwepo. Lakini ili usonge mbele, lazima chama kiwe na uwezo wa kushughulikia hiyo migogoro. zamani CCM walikuwa na uwezo huo. naona unazidi kupungua siku hadi siku. Ni sawa na mgonjwa wa UKIMWI. CCM sasa hivi inashambuliwa na magonjwa nyemelezi. na pia magonjwa hutofautiana. unapokuwa na magonjwa sehemu nyeti kama Moyo na ubongo na mapafu na figo, kifo hakipo mbali...
 
Kinachonekana sasa hivi ni uongozi wa juu wa ccm kukosa busara na hekima eti makatibu wakuu wastaafu Kinana na Nape ni wapumbavu ,INA maana chama nilikuwa kinaongozwa na wapumbavu vipi wenyeviti wao na wana chama wao sio wapumbavu kwa hiyo ni chama cha wapumbavu. kwahiyo Bashiru kapokea chama toka kwa mpumbafu ,chama cha kipumbavu ,aisee reasoning ya viongozi wa sasa wa ccm ni ya ajabu sana .
Hizo ndio hoja ambazo walitakiwa kujiuliza kabla ya kuwananga hadharani hao great men wa CCM. Busara adimu kabisa huko CCM
 
Badala ya kuona udhaifu wa mifumo yetu kwamba dhahabu hiyo imekamatwa kenya, sisi tunasherehekea tena Ikulu! Makubwa. lakini tumeyazoea
Hawasemi aliyesafirisha hiyo dhahabu ni nami na kaito wapi, haya ni maigizo yale yale kama ya Polis wa Mwanza walio escort wizi wa dhahabu.
 
Back
Top Bottom