Sasa naamini Zitto aliwekewa mizengwe

Sasa naamini Zitto aliwekewa mizengwe

Kauli ya maelekezo kutoka ngazi ya juu ni ya kitoto sana kwani alidai kuwa eti kuna mtu alitoka nje akaongea na simu karibu saa nzima kisha akarudi na kutoa kauli kuwa ngazi za juu wanasema mchakato uenedelee.Huu ni utapeli wa kisiasa kwani yeye kama mtendaji mkuu wa serikali iweje atuambie kuwa kuna ngazi za juu tena kwa njia ya simu? Ivi inaingia akili kuwa PM hawezi kuongea na raisi wake mpaka mtu wa kati ndio ALETE taarifa tena ya mdomo kwa maswala muhimu yanayohusu hatima ya nchi. umakini wake unapatikana wapi ikiwa alishiriki kupitisha jambo asililiamini tena kwa maelezo ya mtu aliedai alipigiwa simu toka ngazi za juu? Kwanini leo? kama yeye ni mtu safi kwanini muda wote huu amekaa kimya mpaka alivokatwa jina na kuhamia ukawa ndio aanze kusema haya? kama asingekatwa inamaana angbaki kimya uku akijua kuwa alishiriki katika kuhujumu nchi? wapi uadilifu wake katika hili?
Mkuu hii tabia viongozi wengi wanayo na kama ni hivyo ni uzembe wa hali ya juu. Ninachofahamu ni kuwa Seriklai inafanya kazi kwa maadishi sio maelekezo ya mdomo, hata ukipewa maelekezo ya mdomo, unatakiwa uyaweke katika maandishi ili yaweze kutekelezeka na kuweka kumbukumbu. Kama alipokea tu kwa mdomo, basi ni kosa tena kubwa sana. Hata hvyo, kwa hadhi ya PM hawezi kuwa aliishia hapo, ni lazima baada ya hapo angempigia Rais au aende waongee kwa urefu kuhusu suala alilooona kuwa lilikuwa na utata. Ambacho mimi na wewe hatufahamu nikama alifanya yote hayo, na kama alifanya nini kilikuwa maelekezo ya Rais kwake, na ukumbuke kwa kuwa hawa watu ni marafiki na walishawahi sema kuwa hawakuktana njiani, huenda kuna maelekzo yalitolewa ambayo baadaye yalikuja kumgharimu mwingine kwa hiyo ndo maana ana hasira na kuamua kusema vile, aidha, anaweza kuwa ana mengine makubwa zaidi ambayo kwa hadhi yake asngeweza kuyasema katika hadhira ya aina ile ya siku alipokuwa anapokelewa CDM. Sasa ni wajubu wa upande wa "mamlaka ya juu" kukanusha kama kweli ni uwongo maana watu kwa sasa wanaamini vingine kuhusu Richmond na hii ndo agenda kubwa iliyotumika kumsafisha mtu.
 
Kwani aliyesema lowasa fisadi nani jibu unalo utaishia kapiga kelele mamvi haingii ikulu
 
9k=
 
Zitto asingekubali huu upumbavu.
 
Mkuu, ulimsikia Lowasa alichosema kuhusu tuhuma dhidi yake katika Richmond ? Hebu fikiria kama ungekuwa wewe ndo mwenye maamuzi, mtu akuhahakishie mbele ya hadhara kama ile kwamba kulikuwa na ,aelekezo kutoka Mamlaka za Juu kuhusu kutovunja mkataba wa Richmond ungeendelea kumtuhumu ?? Sasa hayo Mamlaka ya Juu yajitokeze na kukanusha kuwa hayakutoa malekezo kuhusu Richmond. Aidha, nathani kuna mambo mengi ambayo Lowasa aliwaeleza hawa UKAWA hadi wamkubalie kuingia kwao, vinginevyo, kwa jinsi walivyokuwa wanamsema vibaya wangemkaribisha kama kweli wana nia nzuri na maendeleo ya Upinzani nchini. Halfu post yako ya kwanza tu inaonyesha kuwa huenda umeingia kwa ID nyingine kwa makusudi maalum !!!!
Inakuwaje Waziri Mkuu mtu aliyechini yako anakuambia mamlaka ya juu imeamua na wewe kama kiongozi unakubali kirahisi bila ya kufanya cross check kwa hiyo mamlaka ya juu kabla ya kukubaliana na nae...?
 
Kwa yote yanayoendelea Sasa ndani ya CDM, kwa kula matapishi yao na kutuaminisha Lowassa Ni safi na anafaa kutuongoza, naanza kuamini ndugu Zitto aliwekewa mizengwe ndani ya CHADEMA ili atoke.
Kama aliwekewa zengwe basi subiri uone nyota yake iking'ara.
Ila kama alijiwekea zengwe mwenyewe nadhani majibu utayapata soon.
Mpaka sasa nimekusaidia kupokea buku 7 yako kihalali kwa kurespond uzi huu.
 
Wana Jamvi,

Katika harakati za siasa tumeona misemo mingi sana , nachelea kujua nini maana halisi ya neno siasa,
Siasa ni sanaa ya maneno ambayo msanii anaweza kuyatumia kubadili hulka ya mwanadamu kufuata mwongozo wake kwa wakati fulani, na mahesabu fulani.
Siasa ni njia ya kufanya maamuzi katika taifa, mji au hata dunia nzima (siasa ya kimatatifa).
Sehemu muhimu ya siasa ni majadiliano kati ya watu mbalimbali wenye nguvu au mamlaka.
Katika demokrasia kila mtu ana kiasi fulani cha nguvu, kwa hiyo siasa ya demokrasia ina maana ya watu wote kuchangia maamuzi

Maana, chama cha siasa ni mkusanyiko wa watu wenye itikadi, madhumuni, shabaha na malengo yenye kufanana. Ni chama kilichojiwekea kanuni za kufuatwa kwa viongozi na wanachama wake. Ni vigumu kukawa na chama cha siasa kitakachodumu muda mrefu kikiundwa na watu wenye itikadi tofauti na wasiokubaliana katika madhumuni na malengo ya msingi. Mbowe amefanya mahesabu yake ya kuchnga karata vizuri akachukua mtu muhimu katika kukamilisha malengo yake OCt 25


 
Inakuwaje Waziri Mkuu mtu aliyechini yako anakuambia mamlaka ya juu imeamua na wewe kama kiongozi unakubali kirahisi bila ya kufanya cross check kwa hiyo mamlaka ya juu kabla ya kukubaliana na nae...?
Atakuwa alifanya cross check ndo maana ana hasira, siku ile alipokuwa anapokelewa kwa hadhi yake asingeweza kusema yote hayo. If you are wise, you don't slap someone in his/her house.
 
Back
Top Bottom