PAYE
JF-Expert Member
- Jun 19, 2025
- 354
- 395
Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuwa endapo atapata ridhaa ya wananchi, serikali yake itaendelea kutoa ruzuku ya mbolea kwa wakulima ili kuendeleza sekta ya kilimo nchini.
Dkt. Samia ametoa ahadi hiyo leo Septemba 25, 2025 wakati akinadi sera zake kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Mchinga, mkoani Lindi, ambapo amesisitiza kuwa lengo ni kuhakikisha wakulima wa zao la korosho wanapata mbolea na pembejeo kwa ajili ya kuongeza uzalishaji.
Aidha, amesema serikali yake itaendelea kutafuta masoko ya korosho ili kuongeza tija kwa wakulima.
Dkt. Samia ametoa ahadi hiyo leo Septemba 25, 2025 wakati akinadi sera zake kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Mchinga, mkoani Lindi, ambapo amesisitiza kuwa lengo ni kuhakikisha wakulima wa zao la korosho wanapata mbolea na pembejeo kwa ajili ya kuongeza uzalishaji.
Aidha, amesema serikali yake itaendelea kutafuta masoko ya korosho ili kuongeza tija kwa wakulima.