GE2025 Samia: Tuna akiba ya kutosha ya chakula

GE2025 Samia: Tuna akiba ya kutosha ya chakula

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

PAYE

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2025
Posts
354
Reaction score
395
Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi( CCM), Samia Suluhu Hassan amesema Serikali yake itaendelea kutoa ruzuku ya pembejeo na mbolea kwa wakulima kwa lengo la kuongeza uzajilishaji wa chakula.

Akizungumza na wananchi wa Arumeru mkoani Arusha, Oktoba Mosi 2025, Samia alisema sababu ya kuendelea kusimamia sera hiyo ni kutokana na matunda yaliyoonekana ya kuongezeka kwa akiba ya chakula.

"Tunaweka akiba, akiba yetu ya chakula sasa ni miezi minne, kama mvua zisiponyesha Mungu atuepushie hili mwaka mzima hatuwezi kufa njaa tuna chakula cha kutosha"

Samia ameongeza kuwa katika kuhakikisha sekta ya kilimo inazidi kustawi wataweka mkazo katika kilimo cha kutumia teknolojia kuanzia mashine za mashambani, uhifadhi wa vyakula na upimaji vyakula.

'Tunapokwenda kuuza hata malipo sasahivi hatumlipi mkulima mkononi ni teknolojia tunamtilia kwenye akaunti anapata ujumbe kwenye simu yake, hata unapokwenda kupima magunia yako uliyopeleka kama ya mahindi, pamba au chochote mashine ikishapima inakuambia uzito na pesa zako unapata ujumbe kwenye simu yako hapohapo kwahyo tunakwenda kukuza kilimo.

Aidha Samia amesema Serikali yake itakwenda kukuza vyama vya ushirika ambavyo kwasasa vimeanza kufanya kazi nzuri na sio tena chaka la wizi na upotevu wa fedha za wakulima.

"Tumeujenga ushirika kiasi ambacho sasa tunauamini, tumeweza kuwaachia ugawaji wa pembejeo kwa wakulima na wanafanya vizuri, ushirika sasa wao ndio wanawakilisha wakulima wakati wa minada na minada hiyo inafanyika wazi"
 
Back
Top Bottom