PostGE2025 Samia: Nimeliponya Taifa kwa kuanzisha Wizara ya Vijana na kuwaachia huru watuhumiwa wa kesi ya Uhaini

PostGE2025 Samia: Nimeliponya Taifa kwa kuanzisha Wizara ya Vijana na kuwaachia huru watuhumiwa wa kesi ya Uhaini

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
844
Reaction score
1,608
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, amesema ili kuliponya Taifa amechukua hatua kadhaa ikiwemo kuanzisha Wizara ya Vijana iliyopo chini ya Ofisi ya Rais, kuwaachia huru watuhumiwa wa kesi ya Uhaini na kuanzisha Tume Huru ya Uchunguzi wa vurugu za Oktoba 29.

Samia ameyasema hayo katika hafla ya kufungua Mwaka na mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania, leo Januari 15, 2026 Ikulu Chamwino, jijini Dodoma.


 
Hongereni vijana maana mmepata wizara yenu na taifa limepona.

Sasa hakuna shida ya maji, pesa kibao tu mifukoni, ajira kama zote, kazi ya bodaboda imefika mwisho, maisha mepesi, uchumi umekua mara moja, utekaji kwisha, uchaguzi huru ndo mmepata, walioko gerezani wametolewa, na waliopoteza ndugu zao wamepata miili. Hongereni sana vijana wa TZ.

Taifa limepona kweli kweli. Kwa wazee na watoto poleni sana!!!!
 
Hongereni vijana maana mmepata wizara yenu na taifa limepona. Sasa hakuna shida ya maji, pesa kibao tu mifukoni, ajira kama zote, kazi ya bodaboda imefika mwisho, maisha mepesi, uchumi umekua mara moja, utekaji kwisha, uchaguzi huru ndo mmepata, walioko gerezani wametolewa, na waliopoteza ndugu zao wamepata miili.

Hivi kutengeneza wizara ya vijana imewasaidia nini vijana? Hiyo wizara ya vijana imerudisha miili ya vijana aliowafukia msitu wa kondo?

Mwenye uhakika wa kunufaika na kuanzishwa kwa hiyo wizara ni huyo nduguye aliyempa uwaziri., kuna mwingine yeyote amenufaika kwa lolote mpaka sasa?
 
Back
Top Bottom