SAME;Wananchi watengeneza barabara ya km 3

SAME;Wananchi watengeneza barabara ya km 3

JAMHURI

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2010
Posts
449
Reaction score
60
TUTATOKA TU - HEDARU SAME

Wiki hii ilikuwa ni kutengeneza barabara umbali wa km. 3 kwa kumwaga moram na kuisambaza katika kitongoji cha Mbuyuni B kijiji cha Hedaru kata ya Hedaru. Barabara hiyo ni ya mtaa inaelekea kijiji cha Makasa umbali wa Km. 30 kutoka Hedaru.
Wananchi wa kitongoji hicho walimuomba DC wa Same Mh. Rosemary Senyamule aridhie ombi lao la kuiita barabara hiyo kwa jina lake. DC awapongeza kwa kujitokeza wakiwa na vifaa vya kazi.
Katika mkutano wa hadhara, kero ya maji kwa mradi ujulikanao kama mradi wa Masasi yatawala mkutano; ikiongozwa na Mkt. Wa CCM kata.
DC atoa wiki moja kwa wataalamu kukamilisha kero zote ili mradi huo ukabidhiwe kwa kamati iliyoteuliwa.
Aagiza mgogoro wa wakulima na wafugaji ushughulikiwe ndani ya wiki moja.
DC aeleza mpango wa Wilaya wa kiwanda kila kata- kwa maana ya kiwanda kidogo. Atembelea kiwanda cha tangawizi kilicho mbioni kuanza.
Afurahishwa na watu kuitika mwito wa Mh. Rais juu ya serikali ya viwanda na kufanya kazi.

" Same is not same"
 

Attachments

  • IMG-20180915-WA0020.jpg
    IMG-20180915-WA0020.jpg
    85.7 KB · Views: 28
Hao wana kila sababu ya kuitwa Watanzania sio wale wapinga kila kitu
 
Eti kiwanda kila kata!!! Ha ha ha haaaaaaa.... nacheka kwa dharaaaaaau.... ha ha ha aaaa
 
Majembe mengi kuliko moram wanayoisambaza

Mwambieni DC tumeshtukia janja ya nyani kula hindi bichi.
 
Back
Top Bottom