Samatta, tafadhali wekeza kwe shule ya soka (academy)

EZZ CHEZZ

JF-Expert Member
Apr 10, 2011
1,230
1,352
Samatta angalia usije kuwa kama Emmanuel Eboue na wengine kama yeye.

Tumeona kilichompata aliyekuwa mchezaji mahili wa washika bunduki wa London mchezaji Emmanuel Eboue. Mafanikio aliyoyapata yalimtia upofu akaishia kuwanufaisha wazungu (kwa kuwatumikia uwanjani na kisha jasho lake lote kumzawadia Delila wa kizungu aliyemgeuza mgodi wa mafanikio).

Kwa kuchupa mpaka kwenye kitovu cha mafanikio ya soka ulimwenguni (EPL) na kupata mkataba (mnono?) wa miaka mi4 na nusu ni dhahili kuwa kijana katusua.

Nakuomba sana #Samagoal usianze kuishi maisha kama vile hauna deni huku Tz. Yaani kesho keshokutwa tuanze kusikia eti umenunua jumba la vyumba vi3 kwa £mil 2, 3 au 4 ! Ilhali unaweza ishi maisha ya kawaida tu huko na kisha mipesa kama hiyo ukaja kuwekeza huku Tz (kwa kujenga shule ya soka kwa mfano).

Maeneo ya uwekezaji yako mengi sana yanaeleweka na faida zake zinaeleweka (kwako na kwa taifa lako).

Wajibu wa kuanzisha academy umejipa wewe mwenyewe kwa mafanikio uliyoyapata. Sasa fanya utengeneze njia ili wadogo zako uliowaacha huku watinge pande hizo za ulimwengu wa kwanza wa soka mapema (umri wa akina Kelvin John).

Faida za kuanzisha soccer/sports academy kwako;

Kwanza itazidi kukujengea heshima mbele ya Taifa lako. Pia ni uwekezaji mzuri sana kiuchumi kwani ukifanyika vizuri mazao kama ya akina Kelvin John yatakiingizia kituo chako pesa nyingi na manufaa mengine ya kiuchumi. Vile vile itakufanya unufaike na "social capital/network" ambayo ni dhahili kuwa umeijenga huko ughaibuni.

Faida kwa Taifa na jamii;

Kwanza ni ajira hususan kwa watumishi na wengine wote watakaohusishwa na mnyororo huo. Kubwa zaidi ni kuwajengea uwezo wa kitaaluma (ya soka) watoto au vijana wetu. Yaani utakuwa umetupatia jiko la kuwapika akina Kelvin John.

Mbali na hayo utaifungua zaidi hii sekta ya michezo na kuwavutia wawekezaji wengine (wa ndani na nje) kwenye eneo hilo la kiuwekezaji.

Nawasilisha maada wadau. Hebu tuipe nyama zaidi mpaka imfikie mhusika.

Anayeweza kumtag mhusika (au management yake!?) popote pale alipo afanye hima amtonye.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pesa za mwingine unampangia matumizi yako au idea zako azifanyie kazi kisa tu anachakata mpira majuu kwa kigezo cha watu flan walio faidi pesa zao watakavyo na kuishi watakavyo wewe unaona walipotea
Ebu tafuta zako na wewe ndo ujipangie la kufanya kila mtu afe na usawa wake wabongo sisi ni wanafki sana yani mara hii mmeanza kumtolea macho mtu na mshahara wake kisa yupo EPL before amkuliona ilo acheni hadhithi za kikenge kabisa


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
ni ushauri mzuri anaweza kuanzisha akampa baba yake aisimamie hapa Tanzania hatuna academy ambayo inaendeshwa kisasa ikiwa na walimu/makocha sahihi na vitu vyote ambavyo academy inastahili kuwa nazo najua wengine wataitaja Azam lakini angalia makocha wanaofundisha academy za Azam kama ni wabobezi
 
Kuna Nchi labda akaanzishe hiyo Academy...

Huku watu wanaonzisha kila uzi wa kumpinga na kumsema kuwa ana bahatisha ndio aje aweke Academy?

Mnasahau mapema sana.

Huku ambako bodi ya League inasahau kupanga Ratiba.

Awasaidie tu vijana kama ilivyo kwa Kelvin kupata Michongo ya Mbele.Zaidi ya hapo ale tu pesa zake na Familia yake.

Asiitafute majanga.
 
ni ushauri mzuri anaweza kuanzisha akampa baba yake aisimamie hapa Tanzania hatuna academy ambayo inaendeshwa kisasa ikiwa na walimu/makocha sahihi na vitu vyote ambavyo academy inastahili kuwa nazo najua wengine wataitaja Azam lakini angalia makocha wanaofundisha academy za Azam kama ni wabobezi
Well said. Naona wengi wamejibu kwa mihemuko na negative mentalities. Tatizo la hizi ngozi zetu nyeusi ni kutotaka kusikia yale tusiyoyafikiria. Hapa tunajaribu kutanua fikra na kutoa ushauri na maoni.

Mfano mzuri ni Thiery Henry ambaye alianzisha shule yake ya soka pamoja na kwamba kwao Ufaransa kuna academies kibao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna anayempangia mzazi. Just ondoa negativity utaona kuwa huu ni ushauri au maoni na wala siyo malekezo. Tatizo mindset ikiwa ndani ya boksi ni kuona kila kitu kwa sura hasi.
Pesa za mwingine unampangia matumizi yako au idea zako azifanyie kazi kisa tu anachakata mpira majuu kwa kigezo cha watu flan walio faidi pesa zao watakavyo na kuishi watakavyo wewe unaona walipotea
Ebu tafuta zako na wewe ndo ujipangie la kufanya kila mtu afe na usawa wake wabongo sisi ni wanafki sana yani mara hii mmeanza kumtolea macho mtu na mshahara wake kisa yupo EPL before amkuliona ilo acheni hadhithi za kikenge kabisa


Sent from my iPhone using JamiiForums

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna Nchi labda akaanzishe hiyo Academy...

Huku watu wanaonzisha kila uzi wa kumpinga na kumsema kuwa ana bahatisha ndio aje aweke Academy?

Mnasahau mapema sana.

Huku ambako bodi ya League inasahau kupanga Ratiba.

Awasaidie tu vijana kama ilivyo kwa Kelvin kupata Michongo ya Mbele.Zaidi ya hapo ale tu pesa zake na Familia yake.

Asiitafute majanga.
Yeah, bado tuna safari ndefu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom