Mwanongwa
JF-Expert Member
- Feb 15, 2023
- 866
- 805
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Paramagamba Mwaluko Kabudi amelazimika kuingilia kati sakata la uchaguzi mkuu wa TFF baada ya Naibu Waziri wake Hamis Mwinjuma "MwanaFA" kushindwa kuyafanyia kazi mapendekezo ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT).
Taarifa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo zinasema kuwa, Naibu Waziri Hamis Mwinjuma ameshindwa kulitolea maelekezo suala la mchakato wa uchaguzi baada ya kupokea uchambuzi wa kitaalamu na mapendekezo ya BMT.
"Suala hilo lilipofika BMT wataalamu walifanya uchambuzi wa kitaalamu na kutoa mapendekezo kwa Naibu Waziri kwa ajili ya maelekezo."
"Mapendekezo ya BMT ni kuwa baadhi ya viongozi wa TFF, vyama vya mikoa, wilaya na vyama shiriki wamezidisha muda wa kukaa madarakani, hawastahili kuwepo muhula wa tatu kwa mujibu wa Sera ya Maendeleo ya Michezo ya Taifa, lakini Naibu Waziri alikosa maamuzi akaamua kufungia faili kabatini kusikilizia upepo"
"Jambo hilo ndio limemsukuma Waziri Kabudi kuingilia kati. Ameitisha faili na limefikishwa kwake wiki hii, ufumbuzi wa sakata la uchaguzi mkuu wa TFF huenda ukatoka kabla ya wiki ijayo kuisha.", chanzo kilidokeza.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) lilikuwa linapata kigugumizi kuchukua hatua dhidi ukiukwaji wa Sera ya Taifa ya Michezo kutokana ukinzani kutoka kwa Naibu Waziri, Hamis Mwinjuma "MwanaFA"
"Sera ya Michezo ya Taifa inamuondoa Karia kwenye mchakato. MwanaFA na Karia ni marafiki hivyo Naibu Waziri alishindwa kuchukua hatua stahili kwa kuhofia maamuzi yanayomuathiri swahiba wake"
Suala la mgongano wa Katiba ya TFF na Sera ya Maendeleo ya Michezo ya Taifa lilifikishwa BMT zaidi ya mwezi mmoja uliopita na baadhi ya wagombea urais wa TFF na wanasheria na kutokana na unyeti wake BMT walifanya uchambuzi wa kitaalamu na kulifikisha kwa Naibu Waziri, lakini ameshindwa kulitolea maelekezo kwa BMT ili wachukue hatua stahili.
"Mwanzoni kabisa suala hilo lilifika moja kwa moja kwa Waziri kwa kuwa barua ya mmoja wa wadau wa sheria ilielekezwa kwake. Waziri akaitisha kikao cha Msajili, Katibu Mkuu BMT na Naibu Waziri lakini MwanaFA hakuhudhuria, Waziri akaamua kuahirisha kikao.", alisema.
Taarifa kutoka ndani ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo zinaeleza kuwa BMT walishapeleka mapendelezo ya kumng'oa Karia kwenye mchakato wa uchaguzi lakini Naibu Waziri Mwinjuma 'alilifungia kabatini faili' ili lisisogee kokote.
"BMT walilileta hili suala mapema sana. Mapendekezo yao ilikuwa ni kusimamia Sera ya Michezo ya Taifa, jambo ambalo lilikuwa linamuathiri Rais wa TFF,l Karia. Kutokana na athari hizo kwa Karia, MwanaFA alikosa maamuzi akalifungia faili kabatini", chanzo kilisema.
"Unajua Karia na MwanaFA ni maswahiba na wote wanatokea Tanga. Na Karia kupitia influence yake katika mpira wa miguu, kuna namna anamsaidia kwa hali na mali MwanaFA kule jimboni Muheza", kilieleza chanzo.
Mnyetishaji wa habari hizi anaeleza kuwa imekuwa ni kawaida kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Palamagamba Mwaluko Kabudi kumuachia Naibu Waziri wake ashughulikie masuala ya sanaa na michezo lakini katika suala hili la Karia, Naibu Waziri anaathiriwa na maslahi binafsi.
"Kikawaida masuala ya Sanaa na Michezo yanashughulikiwa na Naibu Waziri moja kwa moja ndio maana sakata hilo lilikuwa mezani kwa MwanaFA lakini sasa Waziri kaona alishughulikie mwenyewe"
Taarifa zinaeleza kuwa Naibu Waziri anashindwa kusimamia sheria linapokuja suala ambalo ana maslahi nalo akitolea mfano pia sakata la mechi ya Simba na Yanga lililomalizika hivi karibuni.
"Angalia hata suala la dabi ya Simba na Yanga, Waziri Kabudi alikuwa very smart, alieleza masuala hayo hayawezi kushughulikiwa na serikali lakini Naibu Waziri Mwinjuma alijitokeza hadharani mara tatu kutaka mechi lazima ichezwe".
"Ukiangalia chanzo cha mechi hiyo kutokuchezwa Machi 08 ni Naibu Waziri aliyeagiza geti lisifunguliwe. Haya yote aliyafanya kutokana na Usimba wake. TFF nao wakabariki ukiukwaji wa kanuni wa Simba", alisema.
"Karia na MwanaFA ni Simba damu. Pia wote wanatoka Tanga. Suala la dabi liliwapalia mpaka imebidi likaamuliwe na mamlaka za juu. Hili peke yake lingetosha kuwajibika. Lakini gharama zote hizi wanazipata kwa sababu ya Simba yao."
"Sasa hili suala la uchaguzi wa TFF nalo lilikuwa linaelekea huko huko. Waziri Kabudi ameona aingilie kati mapema lisije likawa gumu kama dabi. Kabla ya wiki ijayo atakuwa ameshalitolea maelekezo", alisema.
Uchaguzi mkuu wa TFF unepangwa kufanyika Agosti 16 mwaka huu lakini mchakato wa uchaguzi ni kama umepata ganzi baada ya Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi kushindwa kusikiliza rufaa za wagombea wanne wiki mbili baada ya rufaa kukatwa.
Hivi karibuni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Wakili Kiomoni Kibamba alisema maendeleo ya mchakato wa uchaguzi yanasubiri Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi wanaotakiwa kusikikiza na kutoa matokeo ya rufaa ya wagombea waliokata rufaa.
"Kamati ya Rufaa wakimaliza kazi yao ndipo sisi tutaendelea na mchakato. Lakini kabla ya kuendelea na mchakato sekretarieti ya TFF inatakiwa kutuandalia kikao. Kwa sasa sekretarieti wanaonekana wako busy na CHAN"
Haikufamika mara moja kwanini Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi imeingia ubaridi kusikiliza rufaa za wagombea.
"Hauwezi kusema Kamati ya Rufaa nayo imeathiriwa na CHAN kwa sababu wajumbe wake sio wajumbe wa Kamati ya CHAN, labda uwatafute TFF wenyewe wanaweza kukuelezea" alisema.
Taarifa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo zinasema kuwa, Naibu Waziri Hamis Mwinjuma ameshindwa kulitolea maelekezo suala la mchakato wa uchaguzi baada ya kupokea uchambuzi wa kitaalamu na mapendekezo ya BMT.
"Suala hilo lilipofika BMT wataalamu walifanya uchambuzi wa kitaalamu na kutoa mapendekezo kwa Naibu Waziri kwa ajili ya maelekezo."
"Mapendekezo ya BMT ni kuwa baadhi ya viongozi wa TFF, vyama vya mikoa, wilaya na vyama shiriki wamezidisha muda wa kukaa madarakani, hawastahili kuwepo muhula wa tatu kwa mujibu wa Sera ya Maendeleo ya Michezo ya Taifa, lakini Naibu Waziri alikosa maamuzi akaamua kufungia faili kabatini kusikilizia upepo"
"Jambo hilo ndio limemsukuma Waziri Kabudi kuingilia kati. Ameitisha faili na limefikishwa kwake wiki hii, ufumbuzi wa sakata la uchaguzi mkuu wa TFF huenda ukatoka kabla ya wiki ijayo kuisha.", chanzo kilidokeza.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) lilikuwa linapata kigugumizi kuchukua hatua dhidi ukiukwaji wa Sera ya Taifa ya Michezo kutokana ukinzani kutoka kwa Naibu Waziri, Hamis Mwinjuma "MwanaFA"
"Sera ya Michezo ya Taifa inamuondoa Karia kwenye mchakato. MwanaFA na Karia ni marafiki hivyo Naibu Waziri alishindwa kuchukua hatua stahili kwa kuhofia maamuzi yanayomuathiri swahiba wake"
Suala la mgongano wa Katiba ya TFF na Sera ya Maendeleo ya Michezo ya Taifa lilifikishwa BMT zaidi ya mwezi mmoja uliopita na baadhi ya wagombea urais wa TFF na wanasheria na kutokana na unyeti wake BMT walifanya uchambuzi wa kitaalamu na kulifikisha kwa Naibu Waziri, lakini ameshindwa kulitolea maelekezo kwa BMT ili wachukue hatua stahili.
"Mwanzoni kabisa suala hilo lilifika moja kwa moja kwa Waziri kwa kuwa barua ya mmoja wa wadau wa sheria ilielekezwa kwake. Waziri akaitisha kikao cha Msajili, Katibu Mkuu BMT na Naibu Waziri lakini MwanaFA hakuhudhuria, Waziri akaamua kuahirisha kikao.", alisema.
Taarifa kutoka ndani ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo zinaeleza kuwa BMT walishapeleka mapendelezo ya kumng'oa Karia kwenye mchakato wa uchaguzi lakini Naibu Waziri Mwinjuma 'alilifungia kabatini faili' ili lisisogee kokote.
"BMT walilileta hili suala mapema sana. Mapendekezo yao ilikuwa ni kusimamia Sera ya Michezo ya Taifa, jambo ambalo lilikuwa linamuathiri Rais wa TFF,l Karia. Kutokana na athari hizo kwa Karia, MwanaFA alikosa maamuzi akalifungia faili kabatini", chanzo kilisema.
"Unajua Karia na MwanaFA ni maswahiba na wote wanatokea Tanga. Na Karia kupitia influence yake katika mpira wa miguu, kuna namna anamsaidia kwa hali na mali MwanaFA kule jimboni Muheza", kilieleza chanzo.
Mnyetishaji wa habari hizi anaeleza kuwa imekuwa ni kawaida kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Palamagamba Mwaluko Kabudi kumuachia Naibu Waziri wake ashughulikie masuala ya sanaa na michezo lakini katika suala hili la Karia, Naibu Waziri anaathiriwa na maslahi binafsi.
"Kikawaida masuala ya Sanaa na Michezo yanashughulikiwa na Naibu Waziri moja kwa moja ndio maana sakata hilo lilikuwa mezani kwa MwanaFA lakini sasa Waziri kaona alishughulikie mwenyewe"
Taarifa zinaeleza kuwa Naibu Waziri anashindwa kusimamia sheria linapokuja suala ambalo ana maslahi nalo akitolea mfano pia sakata la mechi ya Simba na Yanga lililomalizika hivi karibuni.
"Angalia hata suala la dabi ya Simba na Yanga, Waziri Kabudi alikuwa very smart, alieleza masuala hayo hayawezi kushughulikiwa na serikali lakini Naibu Waziri Mwinjuma alijitokeza hadharani mara tatu kutaka mechi lazima ichezwe".
"Ukiangalia chanzo cha mechi hiyo kutokuchezwa Machi 08 ni Naibu Waziri aliyeagiza geti lisifunguliwe. Haya yote aliyafanya kutokana na Usimba wake. TFF nao wakabariki ukiukwaji wa kanuni wa Simba", alisema.
"Karia na MwanaFA ni Simba damu. Pia wote wanatoka Tanga. Suala la dabi liliwapalia mpaka imebidi likaamuliwe na mamlaka za juu. Hili peke yake lingetosha kuwajibika. Lakini gharama zote hizi wanazipata kwa sababu ya Simba yao."
"Sasa hili suala la uchaguzi wa TFF nalo lilikuwa linaelekea huko huko. Waziri Kabudi ameona aingilie kati mapema lisije likawa gumu kama dabi. Kabla ya wiki ijayo atakuwa ameshalitolea maelekezo", alisema.
Uchaguzi mkuu wa TFF unepangwa kufanyika Agosti 16 mwaka huu lakini mchakato wa uchaguzi ni kama umepata ganzi baada ya Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi kushindwa kusikiliza rufaa za wagombea wanne wiki mbili baada ya rufaa kukatwa.
Hivi karibuni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Wakili Kiomoni Kibamba alisema maendeleo ya mchakato wa uchaguzi yanasubiri Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi wanaotakiwa kusikikiza na kutoa matokeo ya rufaa ya wagombea waliokata rufaa.
"Kamati ya Rufaa wakimaliza kazi yao ndipo sisi tutaendelea na mchakato. Lakini kabla ya kuendelea na mchakato sekretarieti ya TFF inatakiwa kutuandalia kikao. Kwa sasa sekretarieti wanaonekana wako busy na CHAN"
Haikufamika mara moja kwanini Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi imeingia ubaridi kusikiliza rufaa za wagombea.
"Hauwezi kusema Kamati ya Rufaa nayo imeathiriwa na CHAN kwa sababu wajumbe wake sio wajumbe wa Kamati ya CHAN, labda uwatafute TFF wenyewe wanaweza kukuelezea" alisema.