Etwege
JF-Expert Member
- Jul 4, 2018
- 5,753
- 15,227
Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Karatu kwa muda mrefu na balozi msitaafu Dkt. Wilbroad Slaa amesema baada ya kupiga kelele kuhusu mkataba wa Kimangungo kati ya serikali ya Tanzania kukabidhi bandari zote za Tanganyika kwa kampuni la DP world kutoka Dubai amepigiwa simu na kutishiwa na watu kutoka serikalini kwamba akae kimya na akiendelea kupiga kelele watamvua hadhi ya ubalozi mara moja!
Dkt. Slaa amesema kwenye swala linalohusu usalama wa mali za Tanganyika hatakaa kimya na yuko tayari kuvuliwa hadhi ya ubalozi hata leo. Slaa amewaita wanaotishia kuchukua ubalozi wachukue mara moja ili yeye aendelee kupigania taifa.
Dkt. Slaa amesema kwenye swala linalohusu usalama wa mali za Tanganyika hatakaa kimya na yuko tayari kuvuliwa hadhi ya ubalozi hata leo. Slaa amewaita wanaotishia kuchukua ubalozi wachukue mara moja ili yeye aendelee kupigania taifa.