Said Lugumi: Siyo kila jipu linatumbuliwa, acheni kufanya mambo kwa hasira

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Hatimaye mmiliki wa kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd ndugu Said Lugumi ameibuka kutoka mafichoni na kuonya kuwa siyo kila jipu linatumbuliwa.

Aidha bwana Lugumi amewahasa watanzania waache kufanya mambo kwa hasira kwani kila jambo limepangwa vyema kwa wakati wake. Hayo aliyasema jana wakati akifanya mahojiano na gazeti la Tanzania Daima.

Katika hatua nyingine waziri wa mambo ya ndani ndugu Charles Kitwanga ameonya kuwa mambo yote yanayohusu mkataba wa Lugumi yalitoka ngazi ya juu bila kufafanua ni ngazi ipi.

Ndugu Said Lugumi kupitia kampuni yake ya Lugumi Enterprises Ltd mwaka 2011 alipewa zabuni ya kusambaza vifaa maalum vya kuchukua alama za vidole kwenye vituo vyote vya jeshi la polisi nchini inayogharimu Tshs bilioni 37 ambapo tayari amelipwa Tshs bilioni 34 huku utendaji kazi wake ukiwa chini ya asilimia kumi.
 
Nilivyo ona neno Tanzania Daima..nikaona hii si habari bali ni taka taka tuu..!

Hakuna mwenye utimamu wa akili anaye weza kuamini Taka taka za Tanzania Daima.
 
Ninaomba sasa Watanzania, tuachane na episode ya majipu ambayo bila shaka imethibitika haina tija yoyote zaidi ya ku divert attentions za watu kutoka kwenye machungu ya ccm ya miaka 50+, na kuwapeleka cinema hall wakabadilishe mawazo. Cinema hall unaona jamaa kapiga deal, kafanikiwa na kuwa millionaire, anaona wake wazuri, anajenga nyumba safi na anamiliki kisiwa chake na ndege za kisasa, anamiliki jeshi lake, anaoa mke mzuri nk. Ukirudi nyumbani, unakuta bado kitanda chako cha teremka tukaze, maharage chukuchuku, kodi ya nyumba unadaiwa na bill ya maji iko mlangoni, hujui kesho itakuwaje.

Hii ya majipu ni sawa na wale wanaokula msoto jeshini halfu jioni wanapelekwe disco kuimba nyimbo ili angalau wasahau karinyekarinye za mchana tayari kwa fatiki za RSM na Ma Buriji ya dharura usiku kibao. Hii majipu episode kila mwenye ufahamu ameona namna ambavyo hayatransform chochote na hata kama kuna impact ni ya juu juu tu, kwa watu aina fulani na haina mzizi wowote wa kuleta sustainable changes zaidi ya show.

Ninaomba Watanzania wachache (ninajua ni wachache) watakaonielewa waniunge mkono kwa kutumia chochote Mungu alichowapa kama ni intellectual ability, influence, n.k tuanze seriously mkakati wa kudai katiba mpya. Katiba mpya ndiyo kitu pekee kitamkomboa Mtanzania. Katiba ya Wananchi na tuanzie pale tume ya warioba ilipoishia. Tusimame imara katika muundo wa bunge la maalumu la katiba ili lisitengenezwe na wabunge wa bunge la JmT.

Bila katiba mpya, ndugu zangu tutaendelea kuishi utumwani mwa ujanja wa watu wachache na hatutakuwa n ahatima yoyte sisi ni uzao wetu. Mwenye ufahamu bila shaka anaelewa kinachoendelea na malengo yake ni nini. Suala la katiba tulianze sasa tusisubiri dkaika za majeruhi ili kuwe na sababu zingine za muda hautoshi, tume iko busy, budget hatuna, tupige kura ya jumla n.k.

Mpumbavu hujifunza kwa maumivu ya makosa yake ambayo bila shaka tumeyaona na ninaomba tusirudie. Mwerevu hujifunza kwa makosa ya wenzake wala hakubali kufanya walipokosea wengine.

Mchana mwema.
 
Lugumi anasema kila jipu siyo la kutumbuliwa? Vizuri, hapo amempa changamoto mtumbua majipu kuwa kuna daraja la raia wanaostahili kutumbuliwa na wengineo hawastahili? Kama mtumbua majipu aiyeomba aombewe kwa Mungu ili aweze kuifanya kazi hii ya kutumbua majipu, tena na kujitanabaisha kuwa ataunda mahakama maalum ya mafisadi, leo mchana kweupe anaambiwa na Mheshimiwa Lugumi kuwa hatumbuliwi.

Kitwanga Waziri wa mambo ya ndani anayetegemewa kuwaagiza polisi wawakamate wahalifu anaonya mambo yote kuhusu mkataba wa Lugumi yametoka ngazi za juu, zipi hizo kuzidi wizara ya mambo ya ndani? Tena yeye Waziri aliyeteuliwa na Rais? Serikali za CCM haziishii maajabu, tunawasubiri watetezi wa mtumbua majipu waje watupe maelezo ya ziada , nishasema watatumbuliwa makarani, madaktari, mafundi basi.

Mfumo wa ufisadi umeasisiwa, umejengwa na kulindwa na CCM. Bahati mbaya mtumbua majipu amejengwa na kulelewa kwenye mfumo huo huo ndani ya CCM, mafisadi wamempa tiketi ya kuingia ikulu na wa naweza wakamnyang'anya akichanga hovyo karata zake, ufisadi na CCM? Uji na mgonjwa!

Tafuteni swagger nyingine hii ya kutumbua majipu tayari imeshachuja mapemaaaa!!!!
 
Hatimaye mmiliki wa kampuni yaLLugumi Enterprises Ltd ndugu Said Lugumi ameibuka kutoka mafichoni na kuonya kuwa siyo kila jipu linatumbuliwa.

Aidha bwana Lugumi amewahasa watanzania waache kufanya mambo kwa hasira kwani kila jambo limepangwa vyema kwa wakati wake. Hayo aliyasema jana wakati akifanya mahojiano na gazeti la Tanzania Daima.

Katika hatua nyingine waziri wa mambo ya ndani ndugu Charles Kitwanga ameonya kuwa mambo yote yanayohusu mkataba wa Lugumi yalitoka ngazi ya juu bila kufafanua ni ngazi ipi.

Ndugu Said Lugumi kupitia kampuni yake ya Lugumi Enterprises Ltd mwaka 2011 alipewa zabuni ya kusambaza vifaa maalum vya kuchukua alama za vidole kwenye vituo vyote vya jeshi la polisi nchini inayogharimu Tshs bilioni 37 ambapo tayari amelipwa Tshs bilioni 34 huku utendaji kazi wake ukiwa chini ya asilimia kumi.
Lugumi hayuko sahihi. Kila jipu lazima litumbuliwe ni moja ya hatua za matibabu yake. Angalau angesema siyo kila "ugonjwa" ni jipu, tungemwelewa!
 
Tulikwishaonya ngazi aliyopandia Magufuli ni ya mabua... Hatua yoyote ya kufurukuta itaanguka!!!
Lakini mimi nimependa sana hili suala lilivyoibuliwa. Sina haraka na wala wasiwasi. Ila naangalia na kusikiliza kwa makini Magufuli atakavyocheza hii ngoma. Ni kipimo tosha na kutokana na matokeo tunaweza kabisa kuhukumu kama anachukia ufisadi au ni msanii kama mafisadi wenyewe.
 
Lakini mimi nimependa sana hili suala lilivyoibuliwa. Sina haraka na wala wasiwasi. Ila naangalia na kusikiliza kwa makini Magufuli atakavyocheza hii ngoma. Ni kipimo tosha na kutokana na matokeo tunaweza kabisa kuhukumu kama anachukia ufisadi au ni msanii kama mafisadi wenyewe.

Huyo ni msanii tu aliyeiba agenda ya ufisadi kupata political mileage!! Angekua mchukia ufisadi tungeona alivyowajibisha walioshiriki kununua vivuko vibovu na zile bilion 240 zilizopotea bila maelezo wizara ya ujenzi...
 
Lugumi hayuko sahihi. Kila jipu lazima litumbuliwe ni moja ya hatua za matibabu yake. Angalau angesema siyo kila "ugonjwa" ni jipu, tungemwelewa!
Umesoma kuhusu elimu yake ya shuleni? Ukiipata hiyo habari utajua kwa nini ametoa kauli kama hii.
 
Lugumi..
Yupo safarini kufuata vifaa vilivyo salia..baada yakua kwenye matengenezo ya zaidi ya miaka mitano..
Lugumi ukivuka hili wewe ni janja zaidi ya bwana sungura...
 
Hatimaye mmiliki wa kampuni yaLLugumi Enterprises Ltd ndugu Said Lugumi ameibuka kutoka mafichoni na kuonya kuwa siyo kila jipu linatumbuliwa.

Aidha bwana Lugumi amewahasa watanzania waache kufanya mambo kwa hasira kwani kila jambo limepangwa vyema kwa wakati wake. Hayo aliyasema jana wakati akifanya mahojiano na gazeti la Tanzania Daima.

Katika hatua nyingine waziri wa mambo ya ndani ndugu Charles Kitwanga ameonya kuwa mambo yote yanayohusu mkataba wa Lugumi yalitoka ngazi ya juu bila kufafanua ni ngazi ipi.

Ndugu Said Lugumi kupitia kampuni yake ya Lugumi Enterprises Ltd mwaka 2011 alipewa zabuni ya kusambaza vifaa maalum vya kuchukua alama za vidole kwenye vituo vyote vya jeshi la polisi nchini inayogharimu Tshs bilioni 37 ambapo tayari amelipwa Tshs bilioni 34 huku utendaji kazi wake ukiwa chini ya asilimia kumi.
Yaani bure kabisa,Siipendi kasha ya Lugumi,ila nasikitika vijana kutengeneza FB page ya Lugumi fake kisha kuanza kupost kejeli kwa watanzania.Tanzania daima wanatumia hiyo...lazima wahusika wa akaunti hiyo feki ni vijana wa DJ.
 
Nilivyo ona neno Tanzania Daima..nikaona hii si habari bali ni taka taka tuu..!

Hakuna mwenye utimamu wa akili anaye weza kuamini Taka taka za Tanzania Daima.
Ficha ujinga wako.Ni gazeti kama mengine yalivyo, kama unaamini mzalendo na uhuru kwanini ushindwe kuamini Tanzania daima?
 
Back
Top Bottom