Tresor Mandala
JF-Expert Member
- Aug 20, 2010
- 45,391
- 95,845
Bila shaka utakuwa umeshaiona tofauti, wananchi wa Rwanda wanatafuta maendeleo wao wenyewe while watanzania wanasubiri serikali iwaletee
Yeah kaka..hakuna askari kumsumbua mtu...na huwezi kukuta wanazozana...
Angalia boda boda zao jamaa walivyo kuwa wanajari usalama wa abiria....
angalia mabasi yao hakuna kusimama....
Mkuu tena pitia pale Ferwafa..ukaone zile ofc zilivyo...kisha tazama za kwetu TFF..
Nitakufahamisha mengi...we ucjari leo mpira wa man city na liverpool..katazame pale Alpha Palace VIP....utajifunza mengi sana kuhusu Rwanda..karibu mkuu
walitokea Huku:
Yirukanywe mu nzu ye ,irasenywa , ngo ni uko ari nyakatsi , atuzwa muri iyi "Burende" ! Ngaya amajyambere FPR yatuzaniye !
sasa wapo huku:
Boda boda dereva na abiria lazima wavae kofia.
Ngoja na mimi nipange safari nikajionee kwa macho yangu..
Ngoja na mimi nipange safari nikajionee kwa macho yangu..
Tanzania iko maneno meeengi,kila kitu naingisa siasa ndani yake halafu ile neno utiifu wa sheria na utoaji wa adhab amemeswa na ile gonjwa kubwa naitwa KITU KIDOGO
Tanzania ya baada ya Baba wa Taifa, inayo mengi ya kuwatenganisha Watanzania kuliko kuwaunganisha. Maendeleo makubwa yanayoweza kutarajiwa kwa mfumo wa sasa ni jua kuchwa na kuzama. Mengine kama barabara nzuri, maji safi na salama, elimu bora ni yatokanayo; yanatokea kwa nasibu na hayajali ubora. Siasa zimekuwa za chuki, udini, ukanda, wenye nacho, ushirikina, n.k Wakuu wa Serikali na chama tawala wamepotea dira. Nchi inakwenda tu bila kujua inaelekea Kaskazini na je ndiko ilikopanga kwenda au inashuka kusini zaidi na kujipongeza! Hata tukifarakana, tukapigana, tukakatana mapamnga, Tanzania haitoweza kuamka na kusimama ili ianze kufuata vema njia ya maendeleo kama Rwanda. Sababu ziko nyingi lakini za haraka ni uwepo wa makundi kinzani mengi (udini, siasa, maskini na matajiri) ambayo chuki zake zimejengeka taratibu na kwa muda mrefu na sababu ya pili uwepo wa rasilimali (mafuta, uranium, gas achana na dhahabu) zilizoadimika katika ulimwengu wa mabeberu na ambazao faida yake kubwa haipatikani kama uchimbwaji wake unafanyika katika jamii yenye amani. Hivyo kiberiti kikiwaka, hawa mabeberu watakuja haraka sana kusaidia pande hasimu kuingia vitani ili wao wauze silaha, nyinyi muendelee kumwaga damu, na wao waendelee kuvuna rasilimali kwa urahisi zaidi.
Naijionea huruma siku hiyo ikinikuta ningali hai......
Bila shaka utakuwa umeshaiona tofauti, wananchi wa Rwanda wanatafuta maendeleo wao wenyewe while watanzania wanasubiri serikali iwaletee
Umeongea vyema tu, ila hapo kwenye BOLD napenda kukukumbusha kuwa Tanzania haitakuja kupigana vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa namna yoyote ile. Waambie na wenzio pia maana hili ndilo mnalotumia kuwatisha wapenda mabadiliko. Tanzania haitakuja kupigana vita ya wenyewe kwa wenyewe hatuna utamaduni huo toka enzi za mababu, KEEP ON MIND BRO!
usisahau pia Kagame hana utani, huweka sahihi zake si kwa kutumia kalamu tu hata bunduki. (no nonse in Rwanda kama TZ)
Binafsi siamini katika kupigana wenyewe kwa wenyewe kutokana na kudorora kwa maendeleo ya nchi pamoja na kuwa na rasilimali nyingi (watu, ardhi, maji baridi/bahari, madini, gesi, uranium). Lakini, ni lazima tubadilishe mambo kwani fujo nyingine zinaweza kuchochewa na wataka rasilimali zetu kwa kutumia mtindo wa "Tawanya utawale- Divide and Rule". Omutwale naona kama ana sababu ya kusema hayo aliyosema.
Umeongea vyema tu, ila hapo kwenye BOLD napenda kukukumbusha kuwa Tanzania haitakuja kupigana vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa namna yoyote ile. Waambie na wenzio pia maana hili ndilo mnalotumia kuwatisha wapenda mabadiliko. Tanzania haitakuja kupigana vita ya wenyewe kwa wenyewe hatuna utamaduni huo toka enzi za mababu, KEEP ON MIND BRO!
Ngoja na mimi nipange safari nikajionee kwa macho yangu..