Riz king
JF-Expert Member
- Dec 30, 2018
- 275
- 547
Ilikuwa 2019 maeneo ya kwa sadala wilayani Hai kule kilimanjaro. Baada ya mkutano wa sambaratisha CHADEMA akiwa na wenzake Sabaya huenda alinifananisha na adui yake kisiasa. Aliniita kwenye gari lake pindi alivyomaliza mkutano. Aliniuliza maswali kadhaa kuhusu mikakati inayofanyika na CHADEMA huko maeno ya boma Ng'ombe, sasa nilikataa maana sikuwa najua lolote.
Ile sijakaa sawa aliniziba kibao cha usoni huku baadhi ya watu wakishangaa. Sikuwahi kuwa CHADEMA wala kujihususha na siasa. Nilisikitika na kulaani hilo tukio la kuaibishwa mbele ya umati. Sabaya akawasha ndinga lake v8 nyeusi huyo akatokomea.
Sabaya alivyokamatwa nilishangilia sana na kushukuru mtesi wangu huyu sasa apate cha moto kwa uonevu. Lakini hivi sasa nimejikuta namuonea huruma sana Sabaya, tumeumbwa kutolipiza. Koroho safi namuombea Sabaya anusurike na haya matatizo, kwani naamini kashajifunza sana na anayajutia aliyowahi yatenda.
Nimemsamehe kabisa kwa moyo mweupe Sabaya.
Ile sijakaa sawa aliniziba kibao cha usoni huku baadhi ya watu wakishangaa. Sikuwahi kuwa CHADEMA wala kujihususha na siasa. Nilisikitika na kulaani hilo tukio la kuaibishwa mbele ya umati. Sabaya akawasha ndinga lake v8 nyeusi huyo akatokomea.
Sabaya alivyokamatwa nilishangilia sana na kushukuru mtesi wangu huyu sasa apate cha moto kwa uonevu. Lakini hivi sasa nimejikuta namuonea huruma sana Sabaya, tumeumbwa kutolipiza. Koroho safi namuombea Sabaya anusurike na haya matatizo, kwani naamini kashajifunza sana na anayajutia aliyowahi yatenda.
Nimemsamehe kabisa kwa moyo mweupe Sabaya.