Sababu za waTanzania wengi kushabikia timu Kigeni

Kyakya

JF-Expert Member
Apr 24, 2009
398
23
Huwa nina sikitika sana ninapokuta watu, wabantu kabisa wa Tandika, Gairo, Mlalakuwa na sehemu nyingi nyingine za Tanzania wakijiita mara mimi Arsenal, yule Liverpool, mara ManU zaidi, tena unakuta wanafikia hatua ya kutaka kupigana.

Tatizo kubwa nadhani TFF wanachangia kwa kutozirusha mechi zetu zote za league hapa Tanzania, kwa kuhofia eti mapato yatakuwa madogo. Unajua mtu aliyezoea kwenda mpirani ata ukionyesha kwenye Luninga na tena umpe hela asiende uwanjani, ataenda tu.

Nashauri Msimu ujao watuonyeshe mechi sio lazima zote ata zile zinazousisha timu kama Simba, Yanga, Mtibwa na nyingine ambazo ni kubwa kwa mtazamo wetu na sehemu mbali mbali zitokazo. Tuwazoeshe watu wetu mpira wetu namna unavyocheza, naamini wanacheza vizuri sana, asa tukiwa na kamera pande zote za uwanja tutawaona vizuri tu. Unajua uduni wa vifaa uwanjani unaweza kukufanya uamini soka linalochezwa ni baya, alikadhalika ubora ukakufanya udhani soka linalochezwa ni safi.

Tuache kulea Ukoloni Mamboleo huo.
 
Huwa nina sikitika sana ninapokuta watu, wabantu kabisa wa Tandika, Gairo, Mlalakuwa na sehemu nyingi nyingine za Tanzania wakijiita mara mimi Arsenal, yule Liverpool, mara ManU zaidi, tena unakuta wanafikia hatua ya kutaka kupigana.

Tatizo kubwa nadhani TFF wanachangia kwa kutozirusha mechi zetu zote za league hapa Tanzania, kwa kuhofia eti mapato yatakuwa madogo. Unajua mtu aliyezoea kwenda mpirani ata ukionyesha kwenye Luninga na tena umpe hela asiende uwanjani, ataenda tu.

Nashauri Msimu ujao watuonyeshe mechi sio lazima zote ata zile zinazousisha timu kama Simba, Yanga, Mtibwa na nyingine ambazo ni kubwa kwa mtazamo wetu na sehemu mbali mbali zitokazo. Tuwazoeshe watu wetu mpira wetu namna unavyocheza, naamini wanacheza vizuri sana, asa tukiwa na kamera pande zote za uwanja tutawaona vizuri tu. Unajua uduni wa vifaa uwanjani unaweza kukufanya uamini soka linalochezwa ni baya, alikadhalika ubora ukakufanya udhani soka linalochezwa ni safi.

Tuache kulea Ukoloni Mamboleo huo.

Mkuu Kyakya,

Mambo ya utandawazi. Chema chajiuza.
 
Hili sio tatizo la Tanzania tu, its everywhere in the world na haya ni matokeo ya utandawazi, football is not immune to globalisation. Ni ubora wa kile watu wanachotaka ndo unatuvuta huku kwenye PL, La Liga, Serie A na Bundesliga- would you really bother kwenda kuona JKT Ruvu akicheza na Polisi Dodoma wakati kwenye luninga kuna Arsenal V Man U? No way! Utaona wakati local games zinagongana na mechi kubwa za ugenini jinsi viwanja vinavyokuwa tupu huku mabaa yanayoonyesha mipira kwenye luninga yameshona mtu kichizi!
Mwaka jana baada ya mechi ya Chelsea na Man U kwenye Champions league, kule Nigeria yaliiibuka mapigano baina ya mashabiki wa timu hizo na watu saba walipoteza maisha!
 
Mambo ya fweza hayo Mkuu. Wenzetu uchumi wao uko juu hivyo tutaendelea kuwashabikia tu
 
Lakini ndugu zangu tungezoeshwa hadi mwanzo kuwa tunaziona kwenye luninga timu zetu nadhani tusingeweza kuzishabikia timu za kigeni. Hivi unaanzaje kuipenda timu iliyoko katika vitongoji vya Liverpool wakati wala ndoto ya angalau kufika uko una, wala hawana mpango na wewe, they dont even know if you exist? Acheni jamani kutetea Ukoloni
 
Hili sio tatizo la Tanzania tu, its everywhere in the world na haya ni matokeo ya utandawazi, football is not immune to globalisation. Ni ubora wa kile watu wanachotaka ndo unatuvuta huku kwenye PL, La Liga, Serie A na Bundesliga- would you really bother kwenda kuona JKT Ruvu akicheza na Polisi Dodoma wakati kwenye luninga kuna Arsenal V Man U? No way! Utaona wakati local games zinagongana na mechi kubwa za ugenini jinsi viwanja vinavyokuwa tupu huku mabaa yanayoonyesha mipira kwenye luninga yameshona mtu kichizi!
Mwaka jana baada ya mechi ya Chelsea na Man U kwenye Champions league, kule Nigeria yaliiibuka mapigano baina ya mashabiki wa timu hizo na watu saba walipoteza maisha!

Mkuu umesema yote sina haja ya kuongeza.

Halafu mkuu siku hizi upo namba 10?

AU ndio masuala ya equal opportunities kwa kila raia?

Lol
 
Sababu ni kwamba timu za kigeni zimeendelea kimpira na kiuendeshaji wa mchezo wa mpira huo na huwa hakuna longolongo sana kama nnavyomkumbuka mshika kibendera Nchimbi wa Mbeya. yeye alikuwa anahakikisha wachezaji wa timu pinzani na Tukuyu Stars wanakuwa offside kila wanapokuwa eneo la penalty la timu hio.

Sasa ukiangalia kwa mfano Premier League ya UK ambayo inajulikana kuwa ndio " elite club competition in the world" na jinsi ya uendeshaji wake ulivyo hutaweza kugeuka kuangalia ligi zingine labda tu kama utaangalia tena La Liga, Serie A, na Bundesliga.

Pia jua kwamba Premier League kwa mfano ilianzishwa miaka ya tisini tu na inamilikiwa na wabia 20 ambao ni timu shiriki za ligi hio na kila mwenyekiti wa timi hizi ndie mwakilishi kule.

FA ni kama mwamvuli wa kuangalia jinsi mchezo wa mpira unavyoendelezwa na ni jinsi gani vipaji vinakuzwa katika nchi nzima.

Thats it.
 
Huwa nina sikitika sana ninapokuta watu, wabantu kabisa wa Tandika, Gairo, Mlalakuwa na sehemu nyingi nyingine za Tanzania wakijiita mara mimi Arsenal, yule Liverpool, mara ManU zaidi, tena unakuta wanafikia hatua ya kutaka kupigana.

Tatizo kubwa nadhani TFF wanachangia kwa kutozirusha mechi zetu zote za league hapa Tanzania, kwa kuhofia eti mapato yatakuwa madogo. Unajua mtu aliyezoea kwenda mpirani ata ukionyesha kwenye Luninga na tena umpe hela asiende uwanjani, ataenda tu.

Nashauri Msimu ujao watuonyeshe mechi sio lazima zote ata zile zinazousisha timu kama Simba, Yanga, Mtibwa na nyingine ambazo ni kubwa kwa mtazamo wetu na sehemu mbali mbali zitokazo. Tuwazoeshe watu wetu mpira wetu namna unavyocheza, naamini wanacheza vizuri sana, asa tukiwa na kamera pande zote za uwanja tutawaona vizuri tu. Unajua uduni wa vifaa uwanjani unaweza kukufanya uamini soka linalochezwa ni baya, alikadhalika ubora ukakufanya udhani soka linalochezwa ni safi.

Tuache kulea Ukoloni Mamboleo huo.

Si ukoloni mambo leo bali ni kuchoshwa na timu zetu ambazi miaka nenda miaka rudi zina underperform na migogoro isiyokwisha kila kukicha. Na kwa taarifa yako tu timu kama MANU, Arsenal, Chelsea, BARC, Real Madrid zina wapenzi kila kona ya dunia na si Tanzania tu. Ukienda nchi mbali za Europe, Asia, South America na hata North America ambako mpira hauna wapenzi wengi bado utakutana na wapenzi wa timu hizo maarufu duniani.
 
mkuu kyakya,

watu wanapenda raha sio shida........unamwambia mtu aende taifa kuangalia mechi ya simba na yanga wakati viwango viko chini.........mie hata huniambii nakwenda taifa kama sina la kufanya..lakini premier siwezi kuikosa wachezaji wote wazuri duniani wanacheza ligi hiyo.usilalamike mzee waache tff waweke professional football then uone kama kila mtu hatoangalia hii ligi....lakini ss hv labda niwe sina kazi.
 
Back
Top Bottom