Sababu za kutokumchagua Magufuli

Sababu za kutokumchagua Magufuli

Afande Fojuman

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2014
Posts
657
Reaction score
548
Hizi ndio Sababu zinazonifanya nisimchague Magufuli

1. Kwa sababu yeye na chama chake wameifanya Tanzania kuwa masikini kuliko wakati ule wa ukoloni.

2. Aliwadhihaki wakazi wa Kigamboni na kusema atakayeshindwa kulipa nauli ya 300,apige mbizi

3. Hawezi kuleta mabadiliko akiwa ndani ya chama kilekile kilichoifikisha nchi hapa ilipo.

4. Atafanya kazi na watu walewale

5. Yupo ndani ya nazi mbovu hivyo hawezi kuwa mzima kwenye mfumo huo

6. Kawekwa na kikundi cha watu kulinda maslahi yao

7. Hana sera, anaigaiga tu

8. Hana ukomav wa siasa nje ya nchi

9. Alisema watu wa Buziku watumie kinyesi Chao watengeneze lami

10. Ana maamuzi ya kukurupuka

11. Hajiheshimu.kwa maana ukiwa na akili timamu huwezi kufanya vitu vya kitoto jukwani

12. Hashauriki

13. Wanaompigia kampeni ndio waliosababisha maisha magumu na wimbi kubwa la umasikini pamoja na elimu na afya mbovu hivyo kumchagua nikuchagua shida na matatizo yanayolalamikiwa leo yaendelee.

14. Hajui hata takwimu, siamini juu ya takwimu zake kwa sababu wizara alizoziongoza ni vigumu sana kuhakiki
mfano samaki ziwani huwezi kuthibitisha.

15. Ni muongo maana ameshindwa kujua vitu vidogo kama rais Sadam Hussein kutudanganya kuwa ni wa Kuwait.

16. Anahatarisha Amani ya nchi kwa kusema wakipita wapinzani kutakuwa na vita

17. Ni muongo maana hana kumbukumbu vizuri mfano aliosema atatumia magari kuzunguka nchi yote leo hii nimeona chopper inaandaliwa.

ENDELEZA NYINGINE…
 
Tazama mabadiliko ya akili

Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa Milango 10 tayari kuhutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Kahama waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni za CCM.
Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiruka kutoka kwenye gari wakati akiwasili kwenye uwanja wa mkutano mjini Kahama.

Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli( wa tatu kutoka kushoto) akiongoza meza kuu kumuombea mapumziko mema mgombea wa Ubunge wa Jimbo la Ulanga Mashariki Mhe. Celina Kombani aliyefariki nchini India tarehe 25 Sept.
Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwachangamsha wakazi wa Kahama kwa kuimba nao nyimbo za hamasa wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Milango 10.
Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akienda sambamba na wakazi wa mji wa Kahama.
Wananchi wakiwa wamebanana kabisa kumuona Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli
Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa mji wa Kahama na kuwaahidi ataubadilisha mji huo na kuwa wa kisasa na wenye maendeleo zaidi.
Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwaambia wananchi wa Kahama kuwa atawafanyia kazi Watanzania wote bila kujali Itikadi zao za vyama.
Hivi ndivyo mkutano wa Kahama wa Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli ulivyofurika.
Wakazi wa Kahama mjini wakiwa wametosha kwenye mkutano wa kampeni za Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli
 
18 . aliuza nyumba za taifa
19.hawezi kutema yai
20.yeye ni mwalimu kitaaluma lakini bungeni hajawahi kuwatetea walimu zaidi anajisifia barabara mbovu alizosimamia
21.ana upara (inaaminika wenye vipara kichwani fate yao ni majanga)
22. Muongo
 
wasap mabadiliko ya akili kupiga push up jukwaani au?
 
Last edited by a moderator:
18 . aliuza nyumba za taifa
19.hawezi kutema yai
20.yeye ni mwalimu kitaaluma lakini bungeni hajawahi kuwatetea walimu zaidi anajisifia barabara mbovu alizosimamia
21.ana upara (inaaminika wenye vipara kichwani fate yao ni majanga)
22. Muongo
asante kwa kuongezea mkuu,
 
Kazikazini at work, hata useme nini Dr. Magufuli ndiye Rais wetu. Hatuwezi kuchagua mtu mwezi
 
Umesahau kuongezea yeye ni mwanaume pekee anayeweza kuumiza vichwa vya malofa mpaka wakashindwa kuhudumia wake na familia zao wakaishia kupeleka mahaba yao kwa Lowa hasa, ama kweli huyu ni mtu hatari
 
Back
Top Bottom