Sababu za kushindwa biashara

Reagan Carima

Member
May 20, 2015
44
194
Nimepata wasaha wa kuingia kwenye tasnia ya biashara na kwakuwa mimi ni kijana bado basi nimetumia muda wangu kufanya tafiti mbalimbali juu ya biashara.

Leo nataka kuzungumzia suala la biashara kufeli.
Watu wengi wamekuwa na ndoto ya kumiliki biashara lakini kwa namna moja au nyingine wanashindwa kufikia malengo yao kutokana na vikwazo mbalimbali ambavyo wanakutana navyo.

Sababu kuu zinazowafanya watu kushindwa kutimiza ndoto hiyo ni pamoja na:-

1- Kutojua historia ya biashara husika
Hapa namaanisha kuna wale wanaoanzisha biashara either kwakuwa ameona fulani alifanya akafanikiwa au kwakuwa sasa nina pesa ngoja niweke kwenye biashara

2- Kukosa management
Asikudanganye mtu yeyote biashara yoyote ile kama haina management nzuri basi tegemea kuanguka na kufa au kugaragara kwa muda mrefu bila mafanikio. Hii ni kutokana na kuwa wewe unaanzisha biashara ukiwa na malengo fulani kisha unampa mtu mwenye malengo tofauti na yakwako aisimamie. Ni ngumu sana

3- Kutaka faida kwa haraka
Watu wamekuwa wakiweka matarajio yao kwenye kupata faida kubwa tena kwa haraka. Hii kwenye biashara ni mbaya sana, ila amini nakwambia wapo watu wamefanya biashara miaka mitano bila kuchukua chochote kama faida na mida wote wamekuwa wakitengeneza tu hivyo kwa wageni hapo wanafeli

4- Kutokuwa na uzoefu
Biashara ni kama mchezo ni lazima angalau uwe na uzoefu kidogo ili uweze kukabiliana na changamoto za humo ndani. Mfano ikiwa mtu anaanzisha biashara ya kuuza maziwa ni lazima awe na uzoefu namna ya kuyatunza na mazingira yakuishi nayo.

Mtu mzoefu atajua kuwa ili niuze maziwa fresh lazima pia nijuane na wanaouza maziwa ya mtindi au namna ya kusindika ili pale maziwa yanapokuwa yanafikia kipindi cha kukaribia kuharibika basi ayasindike au ayatume kwa mwenzake ambaye ni mhusika.

Mfani mimi nina rafiki zangu wameingia kwenye kilimo kwa sababu ya kuelimishwa ila wameshindwa.
Wanashindwa kwakuwa hawana uzoefu. Hawajui namna ya kuendesha kilimo ila katika darasa walielewa na wakaziona pesa kibao mbeleni.

Nitaendelea wakati mwingine ikiwa mada hii itakuwa na mashiko
 
Tunajifunza kupitia makosa. Ukiwa unaogopa kufanya kitu kwa kuhofia kuwa utafeli, hutafanya chochote maishani mwako. Failure is a learning experience. period.
 
Nimepata wasaha wa kuingia kwenye tasnia ya biashara na kwakuwa mimi ni kijana bado basi nimetumia muda wangu kufanya tafiti mbalimbali juu ya biashara.

Leo nataka kuzungumzia suala la biashara kufeli.
Watu wengi wamekuwa na ndoto ya kumiliki biashara lakini kwa namna moja au nyingine wanashindwa kufikia malengo yao kutokana na vikwazo mbalimbali ambavyo wanakutana navyo.

Sababu kuu zinazowafanya watu kushindwa kutimiza ndoto hiyo ni pamoja na:-

1- Kutojua historia ya biashara husika
Hapa namaanisha kuna wale wanaoanzisha biashara either kwakuwa ameona fulani alifanya akafanikiwa au kwakuwa sasa nina pesa ngoja niweke kwenye biashara

2- Kukosa management
Asikudanganye mtu yeyote biashara yoyote ile kama haina management nzuri basi tegemea kuanguka na kufa au kugaragara kwa muda mrefu bila mafanikio. Hii ni kutokana na kuwa wewe unaanzisha biashara ukiwa na malengo fulani kisha unampa mtu mwenye malengo tofauti na yakwako aisimamie. Ni ngumu sana

3- Kutaka faida kwa haraka
Watu wamekuwa wakiweka matarajio yao kwenye kupata faida kubwa tena kwa haraka. Hii kwenye biashara ni mbaya sana, ila amini nakwambia wapo watu wamefanya biashara miaka mitano bila kuchukua chochote kama faida na mida wote wamekuwa wakitengeneza tu hivyo kwa wageni hapo wanafeli

4- Kutokuwa na uzoefu
Biashara ni kama mchezo ni lazima angalau uwe na uzoefu kidogo ili uweze kukabiliana na changamoto za humo ndani. Mfano ikiwa mtu anaanzisha biashara ya kuuza maziwa ni lazima awe na uzoefu namna ya kuyatunza na mazingira yakuishi nayo.

Mtu mzoefu atajua kuwa ili niuze maziwa fresh lazima pia nijuane na wanaouza maziwa ya mtindi au namna ya kusindika ili pale maziwa yanapokuwa yanafikia kipindi cha kukaribia kuharibika basi ayasindike au ayatume kwa mwenzake ambaye ni mhusika.

Mfani mimi nina rafiki zangu wameingia kwenye kilimo kwa sababu ya kuelimishwa ila wameshindwa.
Wanashindwa kwakuwa hawana uzoefu. Hawajui namna ya kuendesha kilimo ila katika darasa walielewa na wakaziona pesa kibao mbeleni.

Nitaendelea wakati mwingine ikiwa mada hii itakuwa na mashiko
Kuandika ni rahisi mno. Shida iko kwenye vitendo. Wewe mwenyewe ulishajaribu kwa vitendo?
 
Kuandika ni rahisi mno. Shida iko kwenye vitendo. Wewe mwenyewe ulishajaribu kwa vitendo?

Kha! Mbona kasema hapo kuwa yupo kwenye biashara? Mbona watu tupo kupingapinga tu? Na hii hoja yako kaieleza humo, kashauri tufanye utafiti wa tunachotaka kufanya, pia ameshauri kuwa wavumilivu na kutopenda faida ya haraka. Sasa unataka asemeje labda au asingeandika? Duh!
 
Kama kwenye kilimo hakuna pesa ,je ziko wapi tuzifate?
'Wanashindwa kwakuwa hawana uzoefu. Hawajui namna ya kuendesha kilimo ila katika darasa walielewa na wakaziona pesa kibao mbeleni.'

Hao wameenda kujitafutia umaskini tu huko kwny kilimo.
 
Biashara zingine zinakera kwelikwel unakuta umefungua kibiashara chako na mtaji was kuokoteza ile sasa ndo unaanza kunyanyuka anakuja mbabe anajaza takataka zote hapa sasa kichwa lazima kiume
 
Back
Top Bottom