tikotiko
Member
- Jul 9, 2010
- 26
- 0
Mimi nikiwa kama mpiga kura, nimeamua kutomchagua KIKWETE, hata kama kura yangu haitasaidia kitu bado nitafurahi kuweka alama ya NO kwake!! Sabau zangu ni hizi hapa:-
1. Chini ya uongozi wake uchumi umeshuka na thamani ya shilingi dhidi ya dola imezidi kuporomoka zaidi
2. Ameshindwa kuboresha maisha ya mtanzania wa kawaida (tofauti na kauli mbiu yake "maisha bora kwa kila mtanzania". Amepiga kelele ya KILIMO KWANZA huku tunaona dhahiri hana nia yoyote kukuza kilimo! Ni msaliti
3. Ameshindwa kuboresha miundombinu (barabara etc)
4. Chini ya uongozi wake, amefanya uteuzi wa aibu kwa Mkurugenzi wa ATC ambaye ni mshikaji wake, matokeo yake ameua kabisa ATC…Tanzania (kama nchi) inashindwa hata na mfanyabiashara binafsi anayendesha Precision Air kwa mafanikio
5. Akiwa rais wa Tanzania ameshindwa kusimama imara kutetea maslahi ya nchi dhidi ya wizi wa mali ya umma na kashfa ya mabilioni ya shilingi ya Richmond...JE NAYE ALIHUSIKA? PCB NA USALAMA MNAJUA WENYEWE...ENDELEENI KULINDA MASLAHI YENU!!
6. Yeye kama kiongozi wa Nchi amewakebehi hadharani wafanyakazi wa Tanzania na viongozi wao pale TUCTA ilipotaka kuitisha mgomo. Yeye kama kiongozi mkuu wa nchi hakuwa na taarifa sahihi kutoka kwa watendaji wake, akawanawa viongozi wa wafanyakazi mbele ya wazee wa CCM, cha ajabu yeye ndiye alikuwa hana taarifa sahihi! Kama kiongozi alitakiwa kuwajibika mara moja. URAIS NA USWAHILI WAPI KWA WAPI?
7. Katika kipindi chake cha uongozi amefanya uteuzi wa viongozi wasiokuwa na uwezo, wakiwemo baadhi ya mawaziri (washkaji) ambao wamekuwa wakiweka mbele maslahi binafsi na kutojali wananchi.
8. Katika kipindi chake cha uongozi RUSHWA IMEONGEZEKA na hakuna hatua madhubuti alizochukua zaidi ya kuwa msemaji saaaaana bila vitendo.
9. Katika kipindi chake cha uongozi matimizi mabaya ya fedha katika manunuzi ya magari ya kifahari na fanicha kwa viongozi wa serikali, wakiwemo wakuu wa mikoa, mawaziri na yeye mwenyewe AKIONGOZA UOZA HUO KWA KUNUNUA BMW X-5 kwa matumizi yake.
10. Ni kiongozi aliyesafiri mara nyingi zaidi ya waliomtangulia (katika awamu ya kwanza ya uongozi wao), safari hizi zimetumia mabilioni ya feadha za watanzania lakini hakuna faida tunayoiona kutokana na safari zake.
TUUNGANE KUSEMA NO KWA KIKWETE
1. Chini ya uongozi wake uchumi umeshuka na thamani ya shilingi dhidi ya dola imezidi kuporomoka zaidi
2. Ameshindwa kuboresha maisha ya mtanzania wa kawaida (tofauti na kauli mbiu yake "maisha bora kwa kila mtanzania". Amepiga kelele ya KILIMO KWANZA huku tunaona dhahiri hana nia yoyote kukuza kilimo! Ni msaliti
3. Ameshindwa kuboresha miundombinu (barabara etc)
4. Chini ya uongozi wake, amefanya uteuzi wa aibu kwa Mkurugenzi wa ATC ambaye ni mshikaji wake, matokeo yake ameua kabisa ATC…Tanzania (kama nchi) inashindwa hata na mfanyabiashara binafsi anayendesha Precision Air kwa mafanikio
5. Akiwa rais wa Tanzania ameshindwa kusimama imara kutetea maslahi ya nchi dhidi ya wizi wa mali ya umma na kashfa ya mabilioni ya shilingi ya Richmond...JE NAYE ALIHUSIKA? PCB NA USALAMA MNAJUA WENYEWE...ENDELEENI KULINDA MASLAHI YENU!!
6. Yeye kama kiongozi wa Nchi amewakebehi hadharani wafanyakazi wa Tanzania na viongozi wao pale TUCTA ilipotaka kuitisha mgomo. Yeye kama kiongozi mkuu wa nchi hakuwa na taarifa sahihi kutoka kwa watendaji wake, akawanawa viongozi wa wafanyakazi mbele ya wazee wa CCM, cha ajabu yeye ndiye alikuwa hana taarifa sahihi! Kama kiongozi alitakiwa kuwajibika mara moja. URAIS NA USWAHILI WAPI KWA WAPI?
7. Katika kipindi chake cha uongozi amefanya uteuzi wa viongozi wasiokuwa na uwezo, wakiwemo baadhi ya mawaziri (washkaji) ambao wamekuwa wakiweka mbele maslahi binafsi na kutojali wananchi.
8. Katika kipindi chake cha uongozi RUSHWA IMEONGEZEKA na hakuna hatua madhubuti alizochukua zaidi ya kuwa msemaji saaaaana bila vitendo.
9. Katika kipindi chake cha uongozi matimizi mabaya ya fedha katika manunuzi ya magari ya kifahari na fanicha kwa viongozi wa serikali, wakiwemo wakuu wa mikoa, mawaziri na yeye mwenyewe AKIONGOZA UOZA HUO KWA KUNUNUA BMW X-5 kwa matumizi yake.
10. Ni kiongozi aliyesafiri mara nyingi zaidi ya waliomtangulia (katika awamu ya kwanza ya uongozi wao), safari hizi zimetumia mabilioni ya feadha za watanzania lakini hakuna faida tunayoiona kutokana na safari zake.
TUUNGANE KUSEMA NO KWA KIKWETE