Rungwe tuna wabunge bubu!

Nasikia mkulu anazindua hospital tena kijijini kabisa Isange unazungumziaje hilo? Acheni lawama zisizojenga kubwabwaja bungeni siyo kipimo cha maendeleo jimboni kuna wabunge hawakosi kuchangia kule bungeni but still jimboni kwao hoi kimaendeleo.. Go go Atupele 2020 is loading.....! Believe me the guy is very smart na atapita bila kupingwa.
 
Mkuu si umesikia?
Niambie hospitali iliyozinduliwa.
 
"unaweza kuwa pandikizi la kuingiza mfarakano kati ya wana rungwe,tabia ambayo haikubaliki"

KWA NINAVOKUPENDA KWETU SIWEZI FANYA HIVO MKUU HAPA NILIPO NATAMANI HATA SHUGHULI ZANGU ZINGEHAMIA RUNGWE ILI NIFIE KATIKA ARDHI YA KWETU NA NINA MIAKA MITANO TU YA KUISHI DAR BAADA YA HAPO NARUDI KWETU TUNZA COMMENT YANG MPAKA 2025 HARAF UNIKUMBUSHE
 
Mkuu kama wameingia madarakani kwa kubebwa na vyombo vya dola watahoji nini, wao kazi yao ni kuunga mkono itakacho serekali kama sehemu ya kulipa fadhila.
Yani mbunge wa rungwe uku tunamwita ' ghost mp' haonekani bungeni wala jimboni yani poor critical analysis, hana confidence mweee!!! anatudharirisha sana uyu standard seven aliepata madaraka kwa kuvujisha damu za watu

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
Nafikiri kuna shida furani haswa kwa hawa viongozi wetu, wengi tunaowachagua hawajitambui kabisa, na leo hata Mheshimiwa amelizungumzia hili kwa uchungu sana, kwa maneno yake Ndugu Rais anashangazwa sana kila kitu kinaelekezwa kwake hata kile ambacho mtendaji wa kata ama mkuu wa wilaya anaweza kutatua.

Katika ziara zake za hivi karibuni kuanzia Mara mpaka Mtwara, Ruvuma Mpaka Mbeya kote huko walikuwa wanamuomba hiki mara kile, huku wanafunzi wanaomba hiki, kule Mbuge anaomba kile, yaani leo ndiyo nikashaangaa kabisa Mheshimiwa Naibu Spika anamumba Mheshiwa Rais Maji na barabara, Je hakuna sehemu yoyote ile ambayo inaweza onyesha tumefanikiwa japo kumpatia hata Zawadi ya Mkungu wa ndizi?

Nazungumza hili kwasababu kuna sehemu ambazo Ndugu Rais hajapata nafasi za kuzitembelea na zina shida pia, je maeneo haya shida zao wazielekeze wapi wakati viongozi wenyewe ndiyo kama hawa wao wenyewe hawana utatuzi wa matatizo yetu? Je inakuwaje Rais anamwambia Mkuu Mkoa/Wilaya, Mbunge, Diwani na Mtendaji kuwa wawatembelee wananchi na kujua shida zao. Je wao hawajuhi kwamba wanatakiwa kufanya hivyo bila kufuatiliwa?

Viongozi wetu tambueni majukumu yenu,
 
Binafsi huwa siamini kama kelele za mbunge zinaweza kushawishi miradi ya maendeleo katika jimbo lake.

Labda Waziri anaweza, naye akiwa na ushawishi wizara ya fedha - Idara ya mipango au apate favour ya Rais.
Wandali bwana weusii hadi akili
 
ukwel upo mana kabila la wandali(wilaya ileje ) wakataa ili rungwe isiwe mkoa mana ndo wilaya ambayo ilitakiwa iamue kuwa nan apewe na iungane nae ndo wakaenda songwe kwa kisingizio wanyakyusa wababe

Sent using Jamii Forums mobile app
Wanyakyusa walididimiza makabila Mengine kwa kuyanyima huduma muhimu, tukumbuke kuwa wakoloni waliweka miundombinu ya shule na hospital sana katika wilaya ya Rungwe. Wanyakyusa malitumia fursa hiyo kama silaha ya kutawala makabila mengine. Wakabila mengine yalishaliona hilo kwasasa watabaki na Rungwe na Kyela yao
 
Ndiyo fundisho mkome kuwachagua wabunge kutoka ccm maana wao wanenda kuitetea serikali
 
Kumbuka bado mpaka leo katika mikoa ya mbeya na songwe wanyakyusa ndo wanashikilia katika elimu vizazi na vizazi shilingi haiji kupinduka
 
Nazan adhabu aliyoipata nassari inamuhusu uyu bwana anahudhuria bunge lipi mbona haonekani
Mzoefu mzee Mwandosya kaongea makubwa na kwa kujishusha mbele ya Rais, na Magufuli kamsikia, barabara tumepata.

Hawa wabunge jamaa zetu ni mabubu kweli.
 
Aisee leo nimeshangaa sana!!
Kumbe S H AMON ni mbunge!!!???
Yaani kumilik maduka na Hotel tu mkaona ni bonge la mjanja mkatupia na kaubunge!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…