RUKWA: Mwanafunzi anusurika kifo baada ya kumeza aina saba za dawa ili ajiue, kisa hataki shule

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
a962ba53b7a3c608853f53a00b66fa38.jpg
Mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya Sekondari Milundikwa iliyoko katika Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa mwenye umri wa miaka 15 (Jina limehifadhiwa), mkazi wa Kijiji cha Katani, amenusurika kufa baada ya kunywa aina saba za dawa kwa lengo la kujiua akidaiwa hataki shule

Akizungumza jana eneo la tukio, Mama mzazi wa mtoto huyo, Stella Hamis alisema juzi saa 2. 00 asubuhi, alimfokea mtoto huyo baada ya kumuona nyumbani badala ya kwenda shule

Stella alisema alimtaka mwanawe aende shule mara moja naye akaelekea Shambani. Hata hivyo alisema, baada ya muda mfupi, mtoto wake huyo alijifungia ndani na kunywa dawa za Hospitalini aina saba tofauti zilizokuwapo na kuandaa kamba kwa ajili ya kujinyonga

"Lakini kwa bahati mmoja wa wana familia, aliingia ndani ya nyumba hiyo na kumkuta mtoto huyo hajiwezi kutokana na dawa alizokunywa", alisema

Stella alisema taarifa zilisambaa kwa jirani ambao walifika eneo la tukio na kumchukua mtoto huyo na kumpeleka Zahanati ya Kijiji kwa matibabu

Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, Solana Kazikodi, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema Ofisi yake ilipata taarifa mapema juu ya tukio hilo na ndiyo waliofanya kazi ya ziada kuhakikisha mtoto huyo anakimbizwa haraka katika Zahanati yao ya Kijiji

Alisema mtoto huyo alifaulu kuendelea na masomo ya Sekondari baada ya kufanya vizuri kwenye mtihani wa darasa la saba katika shule ya msingi Katani

Hata hivyo, alisema tangu aripoti katika shule hiyo, mahudhurio yake yamekuwa hafifu kutokana na kutopenda kusoma

Mganga wa Zahanati hiyo, Godfrey Manga alithibitisha kumpokea Mwanafunzi huyo na kwamba alipatiwa matibabu na hakuathiriwa kwa kiwango kikubwa na dawa hizo kwa kuwa walimuwahisha Zahanati kupata huduma.


Chanzo: Nipashe
 
Sijaisoma yote maana ndefuu. Ila la msingi ni kujua kwanini mwanafunzi huyu hataki shule. Ikibidi aache tu shule maana sio lazima sana katika maisha
 
Kuna sababu nyingi zinazomfanya huyo mtoto akatae shule

Mzazi anatakiwa kuongea nae kwa ukaribu na kiurafiki zaid ili kujua sababu hizo
 
Mtaani kuña medical doctors wawili
Walimu 10
Wahasibu watatu
........
Wote hawana ajira
Enzi zao primary walikuwa na akili kuliko we we

Kwanini usiache shule?
 
Namfananisha huyo dogo na wanachama vijana wa ccm (uvccm) wengi hawakwenda shule na wengine wamefoji vyeti.. japo ukweli unauma!!!
 
sio kila mtu anayaweza mazingira ya masomo 9+ na fimbo kwa kila somo kwani kila mwalimu anataka ufaulu somo lake..
wamwache kama hataki ila watafute njia nyengine ya kumsaidia.. for sure kunawanafunzi wengine wanakataa shule coz wanajiona ktk kusoma ni 0.05 na hapo si kwamba anajifanyisha,wengine wanashindwa sbb ya mazingira n.k
 
a962ba53b7a3c608853f53a00b66fa38.jpg
Mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya Sekondari Milundikwa iliyoko katika Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa mwenye umri wa miaka 15 (Jina limehifadhiwa), mkazi wa Kijiji cha Katani, amenusurika kufa baada ya kunywa aina saba za dawa kwa lengo la kujiua akidaiwa hataki shule

Akizungumza jana eneo la tukio, Mama mzazi wa mtoto huyo, Stella Hamis alisema juzi saa 2. 00 asubuhi, alimfokea mtoto huyo baada ya kumuona nyumbani badala ya kwenda shule

Stella alisema alimtaka mwanawe aende shule mara moja naye akaelekea Shambani. Hata hivyo alisema, baada ya muda mfupi, mtoto wake huyo alijifungia ndani na kunywa dawa za Hospitalini aina saba tofauti zilizokuwapo na kuandaa kamba kwa ajili ya kujinyonga

"Lakini kwa bahati mmoja wa wana familia, aliingia ndani ya nyumba hiyo na kumkuta mtoto huyo hajiwezi kutokana na dawa alizokunywa", alisema

Stella alisema taarifa zilisambaa kwa jirani ambao walifika eneo la tukio na kumchukua mtoto huyo na kumpeleka Zahanati ya Kijiji kwa matibabu

Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, Solana Kazikodi, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema Ofisi yake ilipata taarifa mapema juu ya tukio hilo na ndiyo waliofanya kazi ya ziada kuhakikisha mtoto huyo anakimbizwa haraka katika Zahanati yao ya Kijiji

Alisema mtoto huyo alifaulu kuendelea na masomo ya Sekondari baada ya kufanya vizuri kwenye mtihani wa darasa la saba katika shule ya msingi Katani

Hata hivyo, alisema tangu aripoti katika shule hiyo, mahudhurio yake yamekuwa hafifu kutokana na kutopenda kusoma

Mganga wa Zahanati hiyo, Godfrey Manga alithibitisha kumpokea Mwanafunzi huyo na kwamba alipatiwa matibabu na hakuathiriwa kwa kiwango kikubwa na dawa hizo kwa kuwa walimuwahisha Zahanati kupata huduma.


Chanzo: Nipashe
Ndiyo aina ya wanafunzi wetu hii
 
Back
Top Bottom