Rufaa vyeti feki/utata hadharani

Rufaa vyeti feki/utata hadharani

usiniguse

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
1,725
Reaction score
1,194
Wizara ya utumishi imetoa maelekezo kwaa maafisa utumishi kuhakikisha waatumishi wote ambao wamekutwa hawana hatia baada ya kukata rufaa kufuatia kadhia ya vyeti vyenye utata na vyeti feki wanarudishwa kwenye payroll ya mwezi wa saba haraka kabla haijafungwa.Nimejaribu kutafuta hayo majina bila mafanikio.
Naomba mwenye List ya hao wahanga atusaidie tafadhali
 
Mkuu hujasima gazeti la TANZANIA DAIMA LA LEO
mkuu inaonesha Tanzania Daima hawajui wanachokiandika ,nimelazimika nilitafute kwenye mtandao.Binafsi Afisa Utumishi kanithibitishia kupata maelekezo kutoka Wizara na Majina wametumiwa
 
s

sijasoma mkuu nisaidie wanasemaje

Nashindwa kuliweka hapa, lakini kwa kifupi.

RUFAA VYETI NDIO BASI
Na Nasra Abdallah

Unaweza kusema watumishi wa umma waliokutwa na vyeti feki kisha kukata rufaa, hatma yao kurudi kazini ipo shakani.

Utata huo unatokana na serikali kushindwa kutangaza matokeo ya rufaa zao huku ikitangaza ajira lukuki kuziba nafasi zilizoachwa wazi na watumishi waliong'olewa kwa kukutwa na vyeti feki, bila bila kujali kwamba baadhi yao waliondolewa kimakosa.

Hadi jana serikali imeshindwa kutangaza matokeo ya rufaa zao kama ilivyoahidi kufanya hivyo juni 30, mwaka huu.

Majibu yaliyotolewa jana na waziri mwenye dhamana na utumishi wa umma, Angela Kairuki, yaliongeza giza na utata juu ya hatma ya watumishi hao waliokata rufaa huku wengi wao wakiwa na imani ya kurudishwa kazini.

Waziri Kairuki alipoulizwa na gazeti hili ili kujua nini kimesababisha ukimya wa hatma ya rufaa za watumishi hao, alijibu kwa kifupi kuwa mchakato wa kupitia rufaa zao haujakamilika na utakapokuwa tayari umma utajulishwa.

Alipoulizwa kama mchakato haujakamilika kwa nini wametangaza ajira mpya:"Ndugu mwandishi nimekuambia kuwa tukishakuwa na taarifa zote kuhusu suala hilo tutawaiteni, kwa sasa sina majibu yoyote kwa hayo unayoniuliza naomba unielewe.

KWA KIFUPI NI HAYO, ZAIDI TAFUTA GAZETI USOME.

Lakini kama habari yako ni ya uhakika ni vyema sana
 
mkuu inaonesha Tanzania Daima hawajui wanachokiandika ,nimelazimika nilitafute kwenye mtandao.Binafsi Afisa Utumishi kanithibitishia kupata maelekezo kutoka Wizara na Majina wametumiwa

Kwa maana hiyo kila ofisi husika imetumiwa orodha yake? kama amekuhakikishia ni vyema, maana utumishi hawajaweka katika tovuti yao, Jumatatu sio mbali itajulikana.

Pia kama gazeti limeandika uzushi inabidi liombe radhi huu ni uchochezi wa wazi
 
kwa mtu ambae alikuwa kwenye kadhia hii akiwasiliana na afisa utumishi wake atapata majibu ya nini wameelekezwa ,wameambiwa wahakikishe hao watumishi wanarudishwa kwenye payroll kabla hazifungwa mwezi huu.Shida ni kupata hayo majina
Nashindwa kuliweka hapa, lakini kwa kifupi.

RUFAA VYETI NDIO BASI
Na Nasra Abdallah

Unaweza kusema watumishi wa umma waliokutwa na vyeti feki kisha kukata rufaa, hatma yao kurudi kazini ipo shakani.

Utata huo unatokana na serikali kushindwa kutangaza matokeo ya rufaa zao huku ikitangaza ajira lukuki kuziba nafasi zilizoachwa wazi na watumishi waliong'olewa kwa kukutwa na vyeti feki, bila bila kujali kwamba baadhi yao waliondolewa kimakosa.

Hadi jana serikali imeshindwa kutangaza matokeo ya rufaa zao kama ilivyoahidi kufanya hivyo juni 30, mwaka huu.

Majibu yaliyotolewa jana na waziri mwenye dhamana na utumishi wa umma, Angela Kairuki, yaliongeza giza na utata juu ya hatma ya watumishi hao waliokata rufaa huku wengi wao wakiwa na imani ya kurudishwa kazini.

Waziri Kairuki alipoulizwa na gazeti hili ili kujua nini kimesababisha ukimya wa hatma ya rufaa za watumishi hao, alijibu kwa kifupi kuwa mchakato wa kupitia rufaa zao haujakamilika na utakapokuwa tayari umma utajulishwa.

Alipoulizwa kama mchakato haujakamilika kwa nini wametangaza ajira mpya:"Ndugu mwandishi nimekuambia kuwa tukishakuwa na taarifa zote kuhusu suala hilo tutawaiteni, kwa sasa sina majibu yoyote kwa hayo unayoniuliza naomba unielewe.

KWA KIFUPI NI HAYO, ZAIDI TAFUTA GAZETI USOME.

Lakini kama habari yako ni ya uhakika ni vyema sana
 
Kwa maana hiyo kila ofisi husika imetumiwa orodha yake? kama amekuhakikishia ni vyema, maana utumishi hawajaweka katika tovuti yao, Jumatatu sio mbali itajulikana.

Pia kama gazeti limeandika uzushi inabidi liombe radhi huu ni uchochezi wa wazi
utakumbuka wakati wanasimamisha mishahara waliambiwa maafisa utumishi kufanya kazi hiyo,wamepelekewa majina yanayostahili kurejeshwa kwenye payroll
 
Kwa maana hiyo kila ofisi husika imetumiwa orodha yake? kama amekuhakikishia ni vyema, maana utumishi hawajaweka katika tovuti yao, Jumatatu sio mbali itajulikana.

Pia kama gazeti limeandika uzushi inabidi liombe radhi huu ni uchochezi wa wazi
huyu mwandishi wa hili gazeti inaonesha kaandika hisia zake tu
 
utakumbuka wakati wanasimamisha mishahara waliambiwa maafisa utumishi kufanya kazi hiyo,wamepelekewa majina yanayostahili kurejeshwa kwenye payroll

Nakumbuka sana, ila gazeti la TANZANIA DAIMA lilikuwa limeharibu siku yangu yote, ukipata taarifa zaidi tufahamishamishane Mkuu, asante kwa taarifa.
 
Back
Top Bottom