Japokuwa ramani haina vipimo vyote, nitaribu kuestimate kulingana na vipimo vilivyopo pamoja na assumptions.
Tutaangalia idadi ya tofali za msingi an idadi ya tofali za kuta
HATUA YA KWANZA
Kutafuta urefu wa ukuta tambarare/horizontally (lengths, L)
Nimepata L = 72.02m
Kutafuta urefu wa msingi/vertically (height, H). Assume msingi utaingia ardhini (deep) kwa urefu wa 0.4m na kutoka kwenye ground level mpaka ukuta unapoanzia ni 0.4m, kwa hiyo total height ya msingi itakuwa ni 0.4m + 0.4m = 0.8m
Hf = 0.8m
Kutafuta eneo la msingi (Area of foundation), Af = L x Hf = 72.02 x 0.8 = 57.62sqm
HATUA YA PILI
Size ya tofali za block (dimensions of block) = length, L x Height, H x widths, W = 0.46 x 0.23 x 0.15
Kwa sababu kwenye msingi tofali zitalala, dimension zake zitakuwa = H x W = 0.46 X 0.15 ili kupata eneo la tofali (area of block)
Kutafuta eneo la tofali zkiwa zimelala (Area of block) Ab = 0.46 x 0.15 = 0.069sqm
Kupata idadi ya tofali za msingi = area of foundation ÷ area of block = 57.62 ÷ 0.069 = 835
Idadi ya tofali za msingi ni 835
HATUA YA TATU
Urefu wa kuta kuanzia mwisho wa msingi mpaka kwenye paa (lenghs, L) kawaida inakuwa ni 3.1m.
L = 3.1m.
Area of walls = L x H = 72.02 x 3.1 = 223.3sqm (kumbuka katika hili eneo limejumuisha madirisha na milango)
Kwa hiyo tunatakiwa kutafuta eneo la milango na madirisha tuweze kutoa kwenye eneo letu la 223.3sqm
MADIRISHA,
Japokuwa hayana vipimo lakini nitaweka vipimo kulingana na uzoefu wangu na layout ya madirisha kwenye floor plan
Kuna madirisha 6 yanalingana, yaani madirisha matatu ya vyumbani, madirisha mawili ya dinning na dirisha 1 la living room, kwa hiyo nayapa herufi W1,
W1 = L x H = 2 X 1.5 = 3 x 6 (idadi ya dirisha) = 18sqm
Kuna madirisha mengine mawili yanalingana, yaani dirisha la jikoni na dirisha la living room. Kwa hiyo nayapa herufi W2,
W2 = L x H = 1 X 1.5 = 1.5 x 2 (idadi ya dirisha) = 3sqm
Kuna dirisha 1 la chooni, D3
W3 = L x H = 0.7 x 0.8 = 0.56sqm
Jumla ya eneo la madirisha W = W1 + W2 + W3 = 18 +3 + 0.72 = 21.56sqm
MILANGO
Kuna milango minne inalingana, yaani mlango wa jikoni na milango mitatu ya vyumbani, D1
D1 = L x H = 0.9 X 2.1 = 1.89 x 4 (idadi ya dirisha) = 7.56sqm
Kuna milango miwili ya chooni inalingana, D2
D2 = L x H = 0.8 X 2.1 = 1.68 x 2 (idadi ya dirisha) = 3.36sqm
Kuna mlango mmoja wa kuingilia living room, D3
D2 = L x H = 1 X 2.1 = 2.1sqm
Jumla ya eneo la milango D = D1 + D2 + D3 = 7.56 + 3.36 + 2.1 = 13.02sqm
Jumla ya eneo la milango na madirisha (total area occupied by windows and doors) = D + W = 21.56 + 13.02 = 34.58sqm
ACTUAL AREA OF WALLS (eneo halisi la ukuta) = eneo la kuta – jumla ya eneo la madirisha na milango = 223.3 – 34.58 = 188.72sqm
HATUA YA NNE
Eneo (area) la Size ya tofali za kuta zikiwa zimesimama/dimensions = L x H = 0.46 x 0.23 = 0.1058sqm
Idadi ya tofali za kuta (no. of blocks) AB = actual area of walls (eneo halisi la ukuta) ÷ eneo la tofali zikiwa zimesimama = 188.72 ÷ 0.1058 = 1784
Idadi ya tofali za kuta ni 1784
Jumla ya idadi ya tofali zote = tofali za msingi + tofali za kuta = 835 + 1784 = 2617
NB: Unaweza kuweka makadirio ya tofali 3,000 kwa sababu nyumba inaweza kuwa na anamu (roof gable) pamoja na kufidia matofali yatakayobomoka.
MWISHO
Kwa ujumla ramani ya nyumba ni nzuri lakini inamapungufu baadhi ambayo yanahitaji kurekebishwa wakati wa ujenzi.
1. Hakikisha choo cha kwenye master bedroom kinawekewa dirisha dogo kwa ajili ya mzunguko wa hewa (ventilation)
2. Hakikisha mlango wa public toilet unaangalia dinning, iwepo corridal ndogo ambayo mtu anaingia kabla hajaingia toilet ili kuzuia harufu kuja ndani, kwa hiyo mbele ya public toilet weka ukuta mwingine ili mtu anapokuwa dinning/living room asione moja kwa moja mlango wa kuingilia toilet, yaani iwekwe corridal ndogo (hayo ni mawazo yangu tu)
3. Lakini hakikisha unawekwa ukuta wa kutenganisha kitchen an dinning room ila linawekwa dirisha dogo pamoja na mlango wa kuingilia dinning, hii itasaidia kuwepo na privacy baina ya hizo sehemu mbili. (wazo tu)
Naomba kuwasilisha