Crucifix
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 1,651
- 588
Baada ya kushuhudia ugumu wa magamba ya EL na AC, nimefikia kujiuliza endapo RA alikurupuka kwa hasira kujiuzulu au alishinikizwa? Endapo RA naye angegoma kujiuzulu, sidhani kungekuwa na tofauti yoyote kama ilivyo sasa. Au labda alijazwa woga kuhusu uhai wa biashara zake. Inaonekana pia hakuna umoja fulani miongoni mwa watuhumiwa wa ufisadi CCM bali kila mmoja anapigana kivyake ili kujiokoa. Wakati Chenge akishindwa kupata uspika, Lowassa aliukwaa uenyekiti wa kamati ya mambo ya nje na kumpa fursa za kujijenga. Rostam alisemwa kufadhili ili Sitta asirejee uspika na cheo kikaangukia kwa Makinda ambaye hasemekani kuwa katika mtandao wa Lowassa mwenye malengo ya urais '15. Hivyo naona japo hawa wanatuhumiwa kwa pamoja lakini wao hawana huo umoja wala msimamo wa pamoja.