Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Aliyekuwa mbunge wa viti maalum mkoa wa Geita, Rose Vicent Busiga leo Juni 30, 2025 amechukua na kurejesha rasmi fomu ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kupitishwa kugombea Ubunge wa Jimbo la Mbogwe katika uchaguzi mkuu Wa mwaka huu 2025.
Zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea nafasi ya Ubunge kupitia CCM linaendelea nchi nzima, ambapo wanachama mbalimbali wa chama hicho tawala wanaendelea kujitokeza kuomba ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM katika majimbo yao.
Hatua hii ya Mhe. Busiga ni ishara ya kuendeleza dhamira yake ya kulitumikia Taifa na wananchi wa Mkoa wa Geita kwa moyo wa uzalendo na uaminifu aliouonesha katika kipindi chake cha awali akiwa Mbunge wa Viti Maalum.
Zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea nafasi ya Ubunge kupitia CCM linaendelea nchi nzima, ambapo wanachama mbalimbali wa chama hicho tawala wanaendelea kujitokeza kuomba ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM katika majimbo yao.
Hatua hii ya Mhe. Busiga ni ishara ya kuendeleza dhamira yake ya kulitumikia Taifa na wananchi wa Mkoa wa Geita kwa moyo wa uzalendo na uaminifu aliouonesha katika kipindi chake cha awali akiwa Mbunge wa Viti Maalum.