ROCKET YA FALCON 9 IMERUKA KUELEKEA KWENYE KITUO CHA ANGA CHA KIMATAIFA

ROCKET YA FALCON 9 IMERUKA KUELEKEA KWENYE KITUO CHA ANGA CHA KIMATAIFA

Theorist Mosses

JF-Expert Member
Joined
Jul 16, 2022
Posts
345
Reaction score
253
FB_IMG_16691887135866294.jpg


Kampuni ya spaceX inayo milikiwa na mtu namba moja tajiri duniani "Elon musk" kwa kushirikiana na NASA wamefanikiwa kurusha rocket yao ya falcon 9 kwenye mission ya CRS-26 Cargo ambayo rocket hiyo imeruka kutokea duniani nchini marekani kwenye eneo la NASA's Kennedy space center Florida jana jumanne Nov.22 at 3:54 p.m EST.

Rocket hiyo ya falcon 9 iliruka kuelekea kwenye kituo cha anga cha kimataifa
International Space Station kwaajili ya kuwapelekea wanaanga waliopo kwenye kituo icho chakula pamoja na vifaa vya kiuchunguzi.

Aidha, Elon Musk ambaye ni mtu tajiri zaidi duniani ambaye pia ni mmiliki wa kampuni hiyo ya spaceX, anatarajia kufungua kampuni ya mawasiliano ya gharama nafuu nchini Tanzania kupitia satellite zake aina ya "starlink" zenye kasi zaidi ya internet ukiwa ni mpango wa kukuza uchumi wa kidijitali.

Unaweza kutembelea ukurasa wangu wa facebooki Войдите на Facebook

Join us Tanzania Space Mission "WE CAN"​
 
Aidha, Elon Musk ambaye ni mtu tajiri zaidi duniani ambaye pia ni mmiliki wa kampuni hiyo ya spaceX, anatarajia kufungua kampuni ya mawasiliano ya gharama nafuu nchini Tanzania kupitia satellite zake aina ya "starlink" zenye kasi zaidi ya internet ukiwa ni mpango wa kukuza uchumi wa kidijitali.
Hatakimbia kweli baada ya miaka miwili?
 
Alete hio kampuni haraka, wezi walioko biasharani tushawachoka. Sema nina wasiwasi na mikodi watakayokuja kumjazia huenda akaghairisha😂😂😂
 
Alete hio kampuni haraka, wezi walioko biasharani tushawachoka. Sema nina wasiwasi na mikodi watakayokuja kumjazia huenda akaghairisha😂😂😂
Itabigwa kodi kubwa na yeye ili apate japo kifaida kidogo itabidi apandishe bei na akipandisha bei wateja watakuwa wachache sana hivyo soko litadoda na atafungasha virago
 
Back
Top Bottom