Riwaya ya angamizo 15

Feb 5, 2016
16
4
RIWAYA YA KIPELELEZI: ANGAMIZO
MWANDISHI: HALFANI SUDY
SIMU 0674 395733
WHATSAPP 0757 633010

SEHEMU YA KUMI NA TANO

Hakuwa mvutaji hata wa sigara. Lakini hakuruhusu hata kukohoa. Alijua kukohoa tu ataonekana dhaifu mbele ya watu wale. Safari isiyojulikana ilifika mwisho. Ilikuwa nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam. Kulikuwa na kibanda kidogo porini. Kibanda kilichojitenga na nyumba za watu. Walimuweka kwenye kibanda hicho.
Daniel alishuhudia migongo ya Kerspersky na Zwangendaba ikitokomea. Daniel walimfungia kwenye kibanda hicho! Kilikuwa kibanda kidogo chenye mlango mmoja tu. Hakukuwa na madirisha wala sehemu yoyote ya kutolea au kuingiza hewa. Walimfungia kinjenje. Alisikia muungurumo wa gari, jamaa walitoweka kwa kasi kwa gari yao. Kwenda kumalizia mpango wao hatari wa Angamizo!.
Hawakutaka kumuua Daniel. Nia yao Daniel ashuhudie Angamizo litakaloikumba Serikali yake. Walimuacha hai ili ateseke kwa kuona Angamizo hilo!
*****
Abdul aliendelea kukaa kule kwenye chumba cha siri cha Polisi Arusha. Alikuwa ameshachoka sasa. Alikuwa anautamani sana uhuru wake. Hakumuona Daniel ndani ya siku tatu. Alikuwa anatamani kumuona Daniel. Maana yeye ndio alikuwa tumaini lake pekee la kuurudisha Uhuru wake tena. Alianza kukonda kwa mawazo.
Upande wa jeshi la Polisi nao ulichanganyikiwa sana. Kutoonekana kwa Daniel kwa siku tatu bila mawasiliano yoyote lilikuwa jambo la kushangaza sana. Wakahisi huenda Daniel yuko katika matatizo makubwa. Walimtafuta kila sehemu waliyoifikiria bila mafanikio yoyote.
Ndani ya kibanda kile Daniel aliteseka sana. Kulikuwa na joto kali kupita kiasi. Ukijumlisha na njaa pamoja na kiu kikali alichokuwa nacho, yalikuwa mateso makubwa sana.
Alivyoachwa tu Daniel siku ileile alitafuta njia ya kujiokoa bila mafanikio. Mlango ulikuwa ni geti gumu la chuma. Ukuta wa tofali ulikuwa mrefu wa kunyooka juu, mgumu kuupanda. Kwa juu ziliezekwa bati za udongo. Ndani kulikuwa na giza kiasi cha kutotambua kwamba ilikuwa usiku au mchana. Hakukuwa na madirisha kabisa katika kibanda kile.
Dakika ya kwanza tu aliyowekwa Daniel alianza kutafuta namna ya kujiokoa, kutoka ndani ya chumba kile. Hadi leo, siku ya tatu hakuipata. Na wala hakuwa na dalili ya kuipata.
Alidhohofika sana kwa mawazo.
Alidhohofika sana kwa njaa. Sasa alikuwa amelala chini akiwa amekata tamaa. Alikuwa anakisubiri kifo!
Huku akisikitika siyo tu kwa kutozitimiza harakati alizozianzisha duniani. Hapana, alisikitika kwa kutofanikiwa angalau kujua watu wale walikuwa na siri gani wakiyoilinda namna ile. Alikuwa amelala chini huku akikoroma sasa.
Hakuwa na nguvu sasa.
Ndipo likamjia tumaini.
Akakumbuka kitu pekee kinachoweza kumuokoa mahali pale, ni Mungu. Daniel alipiga magoti kwa shida na kuanza kumuomba Mungu. Hakuwa mhudhuriaji kabisa wa nyumba za ibada. Lakini leo alikuwa amekwama kweli. Alimuomba Mungu kitu kimoja tu. Amuokoe katika mdomo wa mauti ili akaitetee nchi yake, akaitete Tanzania, akawatetee waTanzania. Atutetee mimi na wewe. Aliomba ndani ya nusu saa.
Hakikutokea kitu.
Sasa aliamua kulala akiwa amekosa matumaini kabisa. Daniel alimuona malaika mtoa roho akimsogelea!
Alikata mawasiliano na dunia.
Alilala usingizi wa kifo huku akikoroma !
*****
Ni siku ya nne leo mke wa mzee Washiro hakwenda kuchuuza samaki mtaani. Alikuwa anamhudumia mtu aliyemuokota mumewe, Mzee Washiro. Katika mizunguko yake ya kutafuta matunda ya mabungo porini ili akayauze sokoni Bagamoyo apate pesa ya nauli ili aende Arusha kumwangalia mwanae aliyekuwa mikononi mwa Polisi. Mzee Washiro alikutana na kitu cha ajabu.
Ni mwezi sasa tangu mwanae mpendwa, Abdul, alipompigia simu na kumueleza kuwa amepatwa na matatizo makuu huko Arusha. Mwanawe alikuwa amekamatwa Kwa kosa la kumuua mtoto wa makamu wa Raisi wa Zanzibar, Mayasa Ally.
Siku ya tatu baada ya kuacha kazi yake ya uvuvi ambayo aliona inamuingizia pesa pole pole aliamua kuingia msituni kutafuta matunda hayo ya porini na kwenda kuyauza sokoni Bagamoyo. Kidogo ilimpa matumaini biashara hiyo. Sasa alikuwa na akiba ya elfu kumi na tano ndani.
Lakini siku ya nne aliyoenda msituni kutafuta mabungo, hakurudi na mabungo. Alirudi na mwili wa mtu aliyepoteza fahamu!

JE MZEE WASHIRO KUMTOA WAPI HUYO MTU, NA ILIKUWAJE HADI AKAKUTANA NAE, TUKUTANE SEHEMU YA KUMI NA SITA...
 
Amekosa sehemu ya kwenda kuchabo mana wengine tulisha isoma yote na imeisha coz kuna mtu anakundi watsap la simulizi
 
west2016point naomba kama unayo nirushie mkuu.au niunge na hilo group la whatsapp..nina ugonjwa sana wa hizi hadithi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom