RIWAYA MPYA: "Sikutegemea'' na Mdharuba J.K

RIWAYA MPYA: "Sikutegemea'' na Mdharuba J.K

Mdharuba

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2011
Posts
824
Reaction score
521
STORY: "SIKUTEGEMEA"
MTUNZI: Mdharuba J.K.
SEHEMU YA KWANZA.
★★★★★★★★★★★
"Ndo huyu huyu.. mi naona dawa yake ni kumpoteza kabisa duniani.." Alisema yule bwana aliyekuwa amevaa koti jeusi na suruali yake ya kijani kibichi, alionekana kabisa kuwa alipania mimi nife kikatili..
Yule mganga akaangalia vizuri kwenye lile dishi la maji na kumgeukia tena yule bwana, "Bwana Mbago hapa umefika, na huyu Kassim mimi ntafanya kama unavyotaka mwenyewe,, labda nikuulize tu kwa mara ya tatu na ya mwisho, "Kipi unakipendelea zaidi achanganyikiwe au tumuue kabisa?" Aliweka nukta hapo kwenye swali kisha akaendlea, "Hiki ni kitendo cha dakika moja tu, ukitoa jibu lako mimi namaliza na huko aliko anakua kama ulivyotaka". Baada ya Maelezo haya ya Mganga yule Maarufu kama "Dr Mwinyi" sikuona sababu ya kusubiri jibu la Mbago wala kuendelea kuwabakiza wawili hao duniani tena, nkaikoki vizuri bastola yangu kisha nikafyatua risasi mbili za haraka nkianzia kwenye kichwa cha Dr Mwinyi kisha nikamaliza na Mbago. Kisha nikarudisha bastola kiunoni na kuondoka haraka eneo lile..
"Kama mbwai mbwai tu, mmenifanyia mengi mabaya na mkanifanya nikateseka sana, kwa hakika hili liliwastahili" Nilijisemea moyoni nikiwasha gari na kugeuka kwa kasi saaana nikielekea nyumbani kwa babu yangu, Bagamoyo kumueleza yaliyojiri..
★★★★★★★★★★★★★★★★
Jina langu ni Kassim Omari Mkomwa, nimezaliwa katika kijiji cha Mkata wilayani Handeni mkoani Tanga miaka 35 iliyopita. Kutokana na umasikini uliokuwa unaikabili familia yetu, sikubahatika kusoma sana, niliishia darasa la saba tu, kwani baada ya matokeo kutoka na nikawa sijafanikiwa kuchaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari katika shule za serikali, hakuna aliyekua na uwezo wa kuniendeleza kielimu katika familia yetu, maisha yalikua duni sana familia nzima..
Nikawa nipo nipo nyumbani nikijihusisha sana na shughuli za Kilimo cha mahindi, angalau mwisho wa siku nipate walau cha kupeleka mdomoni kisha cha kujazia choo..ndio maisha ya kimasikini yalivyo, kwanza tunajaza tumbo halafu mambo mengine baadaee..
Nilijihusisha na kilimo mpaka nilipofikia umri wa miaka 20. Siku moja ambayo niliamka mapema kuliko kawaida, kwa sababu ya ndoto niliyoota, nilitoka nje nikakaa katika baraza ya pale nyumbani kwetu.. Ilikua ni saa 11 kasoro dakika 3 alfajiri.. Nakumbuka ilikuwa siku ya Jumanne, siku ambayo babu yangu alikua akiniambia kuwa sio siku nzuri..yeye aliita 'siku ya nuksi'. Pamoja na kuwa nilimuhoji sana kuhusiana na siku hii, lakini yeye alikua bado hajataka kunieleza kwa kina sana bali alikua akiniasa tu kuwa nisijihusishe na mambo mengi yanayoweza kuniletea mitafaruku na watu katika siku hii..Kwahiyo babu yangu huyu ambaye alikua akiitwa Mkomwa Omar Mwandeni alinikataza kukopa, kudai, kutongoza na hata kulipa madeni siku hii, yeye akinambia niiheshimu sana siku ya Jumanne kwani sio siku nzuri..
Nilikaa pale nje mpaka asubuhi jua lilipochomoza na watu wote walipoamka walikuwa wakishangaa kuniona pale nje kwani haikua kawaida yangu.
Mpaka alipotoka babu yangu huyu ambaye nilikua napenda sana kumsikiliza nasaha zake, yeye alinipachika jina la utani ambalo ndilo lilikua maarufu sana kipindi hiki..Aliniita Al'wattan..
?Nasikia leo umeamka mapema sana na kukaa hapa nje, imekuaje mjukuu wangu?? Babu, ambaye alikua amekalia kigoda kilichokua pembeni ya kile kigoda changu, aliniuliza huku akinitizama usoni..
?Kuna ndoto nimeota, nilikua nasubiri uamke hapa unieleze maana ya ndoto ile?
?Ndoto gani tena hiyo Al'wattan unayoota usiku wa kuamkia jumanne??
?Babu, nimeota nakula Komamanga lililoonekana kuiva vizuri sana na lilikua limenivutia, Komamanga hili nililetewa na mtoto mdogo ambaye alinambia ameagizwa na dada mmoja ambaye yeye hamfahamu, baada ya kulila, nikagundua kuwa lile komamanga lilikua na mdudu katikati..naye nilimtafuna..nilipogundua nimetafuna mdudu nikatema haraka, ndipo nikashtuka kutoka usingizini..Nikaangalia saa yangu nikagundua tayari ilishaingia alfajiri, nilipata fazaa kwakweli na wewe ulishanambia kuwa ndoto za alfajiri zinakua za kweli.. Ndo maana nikakosa kabisa usingizi?
?Laahaulaaa..mjukuu wangu Al'wattan.. Ndoto asali katika siku shubiri? Babu alishangaa na kuongea kwa mafumbo kama kawaida yake..
?Unamaanisha nini babu unaposema ndoto asali katika siku shubiri?? Nilimuuliza, maana kiukweli sikumuelewa..
?Ndoto hiyo inatafsirika hiviii...? Babu aliamua sasa kunieleza tafsiri ya ndoto, alishapotezea kunipa maana ya maneno "ndoto asali katika siku shubiri" na hii ndio ilikua kawaida yake, alikuwa hanipi maana ya mafumbo yake mara nyingi, nilijitahidi kuzoea lakini babu alikuwa akinipa wakati mgumu sana kusema ukweli..
?Enheee..? Nilifanya 'Verbal following' kama wanavyotutaka wataalamu wa mambo ya communication.
?Wewe umeamka na bahati leo, lakini siku yenyewe ni mbaya, kwahiyo bahati yako itakukuta leo lakini baadae utapata tabu sana kwa bahati hiyo utakayoipata, kama hutokuwa makini unaweza ukajikuta hata umekuwa muuaji.. , natamani sana ningekuwepo kipindi hicho ili nikupe nasaha nzuri usifikie pabaya, kwa sababu ninavyokujua Al'wattan wewe moyo utakushinda?
Babu aliyaeleza haya kwa hisia kubwa sana, akinisihi nisije kufanya ubaya..
?Babu sijakuelewa, ni bahati gani hiyo inayoweza kunipelekea mpaka kuua?? Niliuliza kwa hamaki..sikuwa naelewa kabisa anachokisema babu yangu mzee Mkomwa Omari Mwandeni.
?Al'wattan, nilitamani sana uwe na hekima na busara kama zangu mjukuu wangu, lakini umezaliwa muda ambao umri wangu umeenda sana.. Utashindwa kujifunza mengi? Babu alianza tena kunizungusha kama kawaida yake, siku zote hakuwa akienda straight kwenye maelezo yake. Baada ya nukta fupi aliendelea tena babu, mimi nilikua namtizama tu wakati huu..
?Bahati utakayokutana nayo leo ni kubwa sana kwa mujibu wa ndoto yako, na hayo matatizo hayatatokea sasa..ni mpaka hapo utakapokuwa umenufaika na bahati husika tena kwa muda mrefu, hapo ndipo utakaposhawishika kufanya chochote kama mtu yeyote ataingilia kuleta kikwazo? Babu alikuwa amenishika mgongoni muda huu anaponieleza maneno haya..
?Babu, nifanyeje ili nisiingie katika kipindi kigumu, yaani namaanisha nifanyeje ili nisifikie huko kwenye mauaji?? Niliuliza kwa shauku, nilitamani kujua cha kufanya kabla babu hajafa..
?Huwezi kuzuia hayo yasitokee kwa mujibu wa ndoto yako, ila mimi nakuasa tu kuwa UKITAKA KULA HARAMU, BASI KULA VINONO? Babu alinijibu swali langu na kunifanya nibaki mdomo wazi..Maana hapa, hata hili fumbo la mwisho ambalo ndio ushauri wake SIKUELEWA.
★★★★★★★★★★★★★★★★★
Itaendelea...

MDHARUBA J.K pia ni Mtunzi wa Riwaya ya HISTORIA BATILI ambayo kwa sasa ipo kitabuni. Vitabu vitaanza kuuzwa rasmi kuanzia tarehe 1/11/2015.
Wasiliana nami kwa simu 0718274130
 
Umerudi na uongo uongo wako mdharuba, malizia zile za mwanzo kwanza rafiki
 
Umerudi na uongo uongo wako mdharuba, malizia zile za mwanzo kwanza rafiki

Mwambie tu azipeleke clouds tutakuwa tunasikiliza...mtu gani anadanganya wakubwa wenzie
 
Atukuamini! Atukukubali !atukuherewi!! Chonde! chonde! Mdharuba usijisumbuwe tena ukapoteza mdaa wako wa kutuandikia stori zako za kukopi sehemu furani wakati ujui lolote . Hatua za kisheria zitachuwa mkondo wake.kwa kifupi uwe mwanzo na mwisho kutumia akili za wezio.
 
Atukuamini! Atukukubali !atukuherewi!! Chonde! chonde! Mdharuba usijisumbuwe tena ukapoteza mdaa wako wa kutuandikia stori zako za kukopi sehemu furani wakati ujui lolote . Hatua za kisheria zitachuwa mkondo wake.kwa kifupi uwe mwanzo na mwisho kutumia akili za wezio.

hahahaaha
 
RIWAYA ya Kusisimua: SIKUTEGEMEA
MTUNZI & MWANDISHI: Jumaa Khatib Mdharuba (Jk)

+255718274130

EPISODE O2
★★★★★★★★★★★★★★★★★
ILIPOISHIA...
"Babu, nifanyeje ili nisiingie katika kipindi kigumu, yaani namaanisha nifanyeje ili nisifikie huko kwenye mauaji?" Niliuliza kwa shauku, nilitamani kujua cha kufanya kabla babu hajafa..
"Huwezi kuzuia hayo yasitokee kwa mujibu wa ndoto yako, ila mimi nakuasa tu kuwa UKITAKA KULA HARAMU, BASI KULA VINONO" Babu alinijibu swali langu na kunifanya nibaki mdomo wazi..Maana hapa, hata hili fumbo la mwisho ambalo ndio ushauri wake SIKUELEWA.

SASA ENDELEA...
Nilikaa na babu pale nje na kuzungumza nae mambo mengi sana yanayohusu maisha yangu ya baadae, babu aliniusia sana niwe naamua kwa kutumia busara na hekima kubwa sana. Alinisisitiza pia nisiwe na hasira za haraka na nifanye uchunguzi wa kina sana kabla ya kuamua jambo lolote.
"Al' wattan kwakweli mimi nakupenda sana, wewe ni katika wajukuu zangu ninaowategemea sana, na najua nikifa utakua ndio babu wao wa baadae ambaye atakua na hekima na busara kama zangu... Nategemea sana hilo kutoka kwako" Babu alionyesha ni jinsi gani ambavyo alikua akiniamini na jinsi gani alivyopenda nirithi nafasi yake vizuri.
"Babu usitie shaka, tegemea mengi mazuri kutoka kwangu" Niliamua kumpa moyo babu, ingawa kwa jinsi alivyokua akiishi babu yangu, ilikua Haiwezekani kufuata nyendo zake.. Labda baadhi tu ya mambo, lakini si yote.
Hiki kilikua ni kipindi cha mavuno, tulikua tukiuza sana mahindi kutoka kwa wageni haswa waliokua wakipita njia hii kuu inayounganisha mikoa mingi kama Dar, Arusha, Tanga, Moro na hata wale wanaotokea Tanga kwenda Dodoma, Mbeya au hata Iringa..
Kipindi hiki cha mavuno tulikua hatukai sana shambani, tulipanga viroba vya mahindi barabarani na sisi tukiwa nyumbani tukisubri wateja, nyumba yetu haikuwa mbali na barabara kuu.
Kwahiyo, baada ya kumaliza maongezi yale na babu, nilienda moja kwa moja barabarani kuweka mambo sawa, kisha nikarudi kusubiri kama mteja atajitokeza.. Wapo pia wateja waliokuja moja kwa moja nyumbani na wale waliochukulia mahindi shamba.
Saa 6:14 mchana, honi ya gari ilikua ikipiga mfululizo kule barabarani usawa wa nyumba yetu, hiyo ilikua ishara ya kuwa kuna mteja. Nikatoka mbio kutoka ndani ambapo nilikua naweka betri mpya katika redio yetu ya mbao, kwani siku hii kulikua na mechi ya Ligi kuu kati ya Simba na Yanga, na babu yangu Mzee Mkomwa mwenyewe alikua akijiita "simba dume" asingeweza kukosa kusikiliza mpira huu ambao utatangazwa redioni ifikapo saa 10, kwahiyo niliamua kumfurahisha.. Nilimpita pale nje mbio, nikielekea barabarani..
"Al' waaattaaaniiiii..." babu aliniita baada ya kuona jinsi nilvyotoka mbio pale, na kunifanya nigeuze..
"Babu, nachelewaa..husikii kuna mteja hukoo..!?"
" Hapana Al' wattan..maisha yako ni ya thamani zaidi kuliko huyo mteja huko unakoenda.. Hebu njoo ukae hapa" Babu alinikata maini, akanifanya nipoteze nguvu.
"Sasa babuu..ina maana leo hata wateja tusiwasikilize?" Nilihoji huku nikishangaa..nimeshika kiuno kwa mikono miwili.
"Ndoto yako uliyoota ndani ya usiku wa kuamkia Jumanne, napaswa kukuchunga sana ili usikutane na mabalaa siku ya leo" Babu aliyasema haya huku akinipa ishara kuwa nikae chini ili anipe maelezo zaidi.
"Sasa hivi ni saa sita, hizi ni saa za Zohari, muda huu na siku hii ya Jumanne ukijumlisha na ndoto uliyoota, siwezi kukuruhusu kwenda kufanya biashara na watu hao wanaopiga honi saa hizi huko, najua mimi siwezi kukuzuia usikutane na bahati yako ya leo, lakinii... Ninao uwezo wa kuzuia angalau usikutane na mambo mazito zaidi kuliko unayoweza kuyabeba hapo baadae.." Babu aliniacha mdomo wazi..
"Kwa sasa usiende kufanya mauzo mpaka itakapofika saa 9 alasiri..hii kazi ataifanya dadaako Mwanauzi kwa muda huu.."
" Duuh, babu mimi SIKUTEGEMEA kuwa ndoto hiyo inaweza kuwa na maana kubwa kiasi hiki." Nilimshangaa Mzee Mkomwa.
"Nasikitika sana Al'wattan, maisha yako yote yametafsiriwa kwenye ndoto hii.." Babu 'alikazia' msumari.
★★★★★★★★★★★★★★★★★
"Yaah true mum, mimi napenda saana mwanaume mchapakazi, msomi, mtanashati na mwenye upeo wa kufikiri mbali..mi mwanaume mzigo huwa sipendi kabisa... Afu pia napenda awe amepanda hewani, afu kama kawa awe anapenda kutoka kwenda sehemu za starehe, kama ulivyonizoesha mum" Naima Daudi, msichana mdogo mwenye umri wa miaka 20 alikua akimueleza mamaake maneno haya wakiwa kwenye gari wakitokea Mombo walipokwenda kusalimia, wakirudi nyumbani kwao wanakoishi Jijini Dar..
"Mwanaume wa sifa hizo yupo mwanangu kweli?! Mchapakazi halafu anapenda starehe?? Mbona maelezo yanagongana mwanangu?"
" Aaah..mama hujanielewa, yani namaanisha awe anapenda 'outings' na awe pia anafanya kazi kwa bidii sana..asiwe lelemama"
"Mmh..haya mwanangu, ila tatizo mapenzi hayana kanuni maalum, hivyo vigezo baki navyo mwenyewe tu kichwani, ila utakuja kujikuta unapenda sehemu ambayo HUKUTEGEMEA.."
"Aaah waapi.. Ni bora nisiwe kwenye mapenzi forever mum,but sio kuwa na mtu asiye na vigezo hvyo"
"Ok sawa mwanangu, omba Mungu kwani yeye ndo kila kitu"
"Ok mum, as i alwayz do..yaaaniii..i wish u could see my first boyfriend..Mungu akuweke mamaangu"
"Aaamiin.."
Mama Naima aliendesha gari kwa kasi sana kwani walikua wamechelewa, na alitaka wafike jijini Dar kabla ya saa 3 usiku.. Muda huu walikua Korogwe na ilishafika saa 10:30 jioni.
Mazungumzo kuhusu mapenzi na mahusiano kati yake na mwanawe yaliendelea.
"Mimi babaako SIKUTEGEMEA kabisa kuwa ndiye angekua mume wangu..unajua ilikuaje?" Mama Naima alianza kufunguka juu ya uhusiano wake na mumewe, walipoanzia.
"Yaani yeye alikua ndiye kiranja wa nidhamu shuleni kwetu, wakati huo mimi nilikua dada mkuu.. Na nilikua na uhusiano wa kimapenzi na kaka mkuu wetu, maana ilikua shule ya mchanganyiko halafu ni 'day'.. Kila mtu alikua anajua kuhusu uhusiano wetu mimi ni kaka mkuu, lakini cha ajabu sasa.. Akinikorofisha kesi zote nilikua nazipeleka kwa Kiranja wa nidhamu ambaye ndiye babaako, maana yeye ndiye alikua rafiki yake wa karibu sana. Basi babaako yeye akawa kazi yake kunifariji tu na kunisihi nimvumilie, kiukweli alikua ananiliwaza sana. Mpaka baadae yule kaka mkuu alipoamua kunisaliti akawa na mwanamke mwengine ndo mimi nikaliwazwa mpaka nikaliwazika na babaako ndo mpaka leo tumefika hapa" Mama Naima aliweka kituo na kumfanya mwanawe acheke. Maneno yake ya mwisho yalimchekesha sana Naima, akaanza kumfikiria babaake jinsi alivyokua na busara na anavyopangilia maneno yake katika maongezi, akajikuta amejawa na furaha.
"Duuh, mama kwahiyo yule unayedhani ndiye mume kumbe anaweza kuwa siye kabisaa??"
"Yaani hata kidogo, mume ni siri ya Mungu mwenyewe ndo anajua.."
"Ok, sawa mama, tuzidi kuomba dua"
"Hicho ndo cha msingi"
"Halafu tukifika Mkata nikumbushe tununue mahindi mwanangu, maana kule nyumbani unga umeisha, halafu si unamjua babaako anavyopenda ugali tena?!"
"Sawa mama wala usijali"
Naima aliitikia na wakaendelea kupiga story zingine na mamaake yule mpendwa.. Ingawa hakuwa mtu mzima sana, lakini Mama Naima alikua mama mwenye heshima na busara nyingi, licha ya kuwa pesa za mumewe zilimfanya akafeli kwenye baadhi ya vitu katika malezi ya huyu mwanae,, alimzoesha maisha ya juu sana, alijua zaidi kutumia kuliko kutafuta, na kutokana na malezi haya pia alikuwa na dharau ya ndani..alikuwa akiwadharau sana watu wasio na kipato kikubwa.
"Mama, Mkata ndio hapa, maana najua utakua ushasahau" Naima alimkumbusha mamaake, Tayari ilishafika saa 11:20 jioni..
"Ok, ngoja nitafute sehemu nzuri ya kuegesha gari ili tununue hayo mahindi"
"Ok sawa mum"
Mama Naima akatafuta sehemu iliyokaa vizuri pembeni ya barabara akapark gari yake kisha wote wakashuka, moja kwa moja mpaka katika kiroba kimoja ambacho kilikua kimeegeshwa karibu na walipopark gari yao..
"Kaka, mahindi kama haya kiroba kizima bei gani?" Naima alimuuliza kijana mmoja ambaye alikuwa jirani na kiroba kile, amesimama akiwa amevaa jeanz yake ya bluu na t-shirt nyeupe na chini alikua na viatu vya wazi.. Mkononi akiwa ameshika mfuko mweusi wa rambo. Hakuonekana kuwa anahusika na kiroba kile, lakini kwakuwa alisimama karibu nacho basi kwa Naima yeye aliona kinamuhusu tu, ndio maana akaamua kumtupia swali lile tena bila hata salamu. Naima aliitikia na wakaendelea kupiga story zingine na mamaake yule mpendwa.. Ingawa hakuwa mtu mzima sana, lakini Mama Naima alikua mama mwenye heshima na busara nyingi, licha ya kuwa pesa za mumewe zilimfanya akafeli kwenye baadhi ya vitu katika malezi ya huyu mwanae,, alimzoesha maisha ya juu sana, alijua zaidi kutumia kuliko kutafuta, na kutokana na malezi haya pia alikuwa na dharau ya ndani..alikuwa akiwadharau sana watu wasio na kipato kikubwa.
"Mama, Mkata ndio hapa, maana najua utakua ushasahau" Naima alimkumbusha mamaake, Tayari ilishafika saa 11:20 jioni..
" Mhh mwanangu kwa uzee gani nilokua nao mpka nisahau mara moja hii..mtoto bado beauty kabisa nalipa" alitania Mama Naima huku wote wakiangua vicheko..
"Ok, ngoja nitafute sehemu nzuri ya kuegesha gari ili tununue hayo mahindi"
"Ok sawa mum"
Mama Naima akatafuta sehemu iliyokaa vizuri pembeni ya barabara akapark gari yake kisha wote wakashuka, moja kwa moja mpaka katika kiroba kimoja ambacho kilikua kimeegeshwa karibu na walipopark gari yao..
"Kaka, mahindi kama haya kiroba kizima bei gani?" Naima alimuuliza kijana mmoja ambaye alikuwa jirani na kiroba kile, amesimama akiwa amevaa jeanz yake ya bluu na t-shirt nyeupe na chini alikua na viatu vya wazi.. Mkononi akiwa ameshika mfuko mweusi wa rambo. Hakuonekana kuwa anahusika na kiroba kile, lakini kwakuwa alisimama karibu nacho basi kwa Naima yeye aliona kinamuhusu tu, ndio maana akaamua kumtupia swali lile tena bila hata salamu. Yule kijana akamuangalia bila kumjibu chochote.. Mama yake ambaye alikua nyuma yake kidogo, alipomfikia yule kijana alisalimiana nae vizuri..
"Za saa hzi kaka?"
"Nzuri tu, hali yako?"
"Safi tu, samahani wewe ndo muhusika wa hapa?"
"Hapana, yupo kijana ambaye anakaa nyumba ilee pale juu, unahitaji niwaitie?"
"Yaah, naomba umshtue kakaangu, ninahitaji haya mahindi"
Baada ya hapa yule kijana akaniita, nilikuja nikiwa na nywele nyingi kichwani ambazo hazijapata kuonana na kitana kwa muda mrefu, na singlend yangu iliyochoka sana.. Nikasalimiana nao, Naima yeye muda huo alikua amekodolea macho suruali yangu ya kitambaa cheusi kilichopauka na yeboyebo zangu zilizochoka sana nilizovaa mguuni.
"Kwanini unakaa mbali sana na biashara yako inayokuingizia kula yako?" swali aliloniuliza Naima kabla ya kuongea chochote.. Kwa jinsi alivyokua ananiangalia kwa dharau, nilitamani kumjibu ovyo sana, lakini bado nilikumbuka sana maneno ya babu, nikaamua kuwa mpole, nikatoa tabasamu la meno yangu ambayo kila siku yalipigwa na mswaki wa mti na mkaa..
"Watu wengine banaa...yaaniii you are not serious, kwanini msizijali biashara zenu ambazo ndizo zinazowaweka mjini?" Naima aliendelea kukazia baada ya kuona nimetabasamu..
"Bei gani haya mahindi?" Mama Naima alimkatiza mwanae ambaye alionekana bado alikuwa na hamu ya kuendelea kunishambulia.
"Hiki kiroba cha kg 30 ni shilingi elf 15 tu mama" nilijibu kwa unyenyekevu.
Wala Mama Naima hakuuliza mara mbili, akatoa pesa na kunikabidhi..Nikawapelekea kiroba chao hadi kwenye gari yao. Kabla sijaondoka, Naima akaonekana kama anataka kusema jambo.
"Samahani kaka, hivi haya ndio maisha uliyochagua kuishi?" Aliniambia Naima baada ya kuona nimemtazama. Sikuwa na jibu la haraka la kumpa, nikaona niendelee kutabasamu. Akaniangalia sana, halafu akaamua kwenda mbali zaidi..
"Hivi kwa maisha haya hata kuoa utaoa kweli wewe? Kuna mtu anaweza kukukubali kwa hivyo ulivyo? Halfu sikuelewi, kila ninachoongea wewe unacheka tu.." Bado sikuona sababu ya kumjibu chochote, nilimkumbuka sana Mzee Mkomwa.
Nikageuka na kurudi nyumbani.
"Babu, nimekutana na mtu amenitolea maneno ya kejeli sana mpaka nikatamani kulia, amenidharau sana, hivi sisi masikini tumemkosea nini Mungu? Babu..hivi kweli mtoto yule mdogo kweli ndio wa kunidharau mimi??" Nilimuhoji babu Mzee Mkomwa baada ya kufika nyumbani, maswali ambayo yalikua kichwani mwangu. Mzee Mkomwa hakuonekana kushangaa sana, bali alinishika mkono na kuniambia..
" Tafsiri ya ndoto yako ndio imeanzia hapo, shukuru sana haikuwa mida ya Zohari, hiyo ndo nafuu yako, na ndo maana nilikuzuia..lakini ungegongwa hata na gari leo" Maneno yaliyonifanya nianze kuduwaa..
"Kitu pekee kinachofanya mkaa uendelee kuthaminiwa ni kwa sababu unatoa moto na watu wanapikia, lakini unafikiri kuna anayependa kuchafuka?" Babu alianza mafumbo kama kawaida yake.
"Al'wattan utasumbuka sana mjukuu wangu, yule mwanamke atakusumbua sana, ila nakuusia sana tuliza akili sana katika maisha yako,, SIKUTEGEMEA kuwa ndoto hii utaiota wewe kwenye siku mbaya kama hii" Babu alionekana kuongea kwa hisia sana..alinipa wakati mgumu.
"Mwanamke gani tena huyo atakayenisumbua babu?" Niliuliza, maana maneno ya babu yalikua magumu kuyaelewa..hakuwa muwazi sana.
"Huyo uliyekutana nae, aliyekudharau" Alinijibu.
"Yule si nishaachana nae, na wameshaondoka, usumbufu unatoka wapi teena babu?"
"Ulishawahi kutembea barabarani kwenye lami halafu ukaona maji mbele lakini ukifika hakuna maji?" Babu aliniuliza badala ya kunijibu, kama ilivyo kawaida yake, ni kama mtu ambaye hajasikia swali langu.
"Ndio babu, mara nyingi tu" Nilimjibu haraka kutaka kujua atasema nini..
"Upeo wako wa kuona mambo ni dhaifu kama ulivyo upeo wako wa kuona vitu vya kawaida..andika tarehe ya leo katika kumbukumbu zako, siku Munnawar iliyojaa Zohali.., " Babu alimalizia maelezo yake yenye utata, mimi nilibaki nimeshika kichwa tu.
★★★★★★★★★★★★★★★★★
+255718274130
Dont Miss Episode 03
 
Riwaya ya Kusisimua: SIKUTEGEMEA
Mtunzi/Mwandishi: Mdharuba, J.K (Mr.).

+255718274130

*SEHEMU YA TATU*
★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Nilibaki nikitafakari juu ya lile tukio na mafumbo ya babu Mzee Mkomwa. Kwakweli nilikua katika wakati mgumu sana.
Vipi Mzee Mkomwa anihusishe moja kwa moja na mwanamke yule kiburi? Jeuri kiasi kile? Ni nini haswa tafsiri sahihi ya ndoto yangu ambayo Mzee Mkomwa alionekana kuijua vizuri ila tu aliamua kunificha?!.
Kila swali lililokuja katika kichwa changu lilikosa majibu.
Ilipofika saa mbili usiku, baada ya kumaliza tu kula chakula cha usiku, nikamuomba Mzee Mkomwa leo tutoke wote katika safari yake ya kila siku mara baada ya kupata chakula.
Mzee Mkomwa alikuwa na kawaida ya kutembea, mwenyewe aliita 'kunyoosha miguu' kila baada ya chakula cha usiku. Safari hii humchukua nusu saa kabla hajarudi nyumbani na kulala, sikujua ni kwa ajili ya nini, lakini nilizoea kumuona akifanya hivyo.
“Leo umeona nini hadi kuamua kutembea na mimi katika safari yangu hii ya kunyoosha miguu?” Aliuliza babu tukiwa ndo tunatoka nje ya nyumba yetu..
“Nataka kujifunza vitu vingi zaidi kutoka kwako, nimegundua kadri ninavyokuweka mbali ndivyo ninavyozidi kuwa mjinga wa mambo mengi” Nilijibu kwa kirefu, maelezo ambayo yalionekana kumfurahisha Mzee Mkomwa.
“Vizuri sana, sasa umekuwa Al'Wattan, mimi nakupenda sana, na natamani sana ujue vitu vingi sana katika hii dunia, lakini wewe ulikua hujagundua hilo, ila kwa sasa unaonekana kujifunza kitu, utafaidi sana.. Niombee Mungu nisife mapema japo umri wangu ndo hivyo umesonga sana” Mzee Mkomwa alijibu kwa kirefu na kunipa matumaini sana. Nilikua najaribu 'kumchombeza' ili baadae nimuulize maswali yangu yote ambayo yalikosa majibu.
“Babu hivi ni kwanini unapenda kutembea kila baada ya chakula cha usiku?” Niliamua kuanzia mbali.
“Sisi masikini, mara nyingi huwa tunajikuta tunakula vyakula vizito usiku kabla ya kulala, tiba yake ili usipate maradhi ni kutembea walau kwa muda wa hatua 200 ili ukidasaidie chakula kilainike vizuri huko tumboni kwa sababu usiku huna kazi ngumu uifanyayo...”. Akawaka nukta ndogo Mzee Mkomwa kabla ya kuendelea..
“Ukila tu chakula kama ugali usiku huu na kuamua kulala, ni hatari sana Al'Wattan na nakuomba ubadilishe utaratibu kuanzia leo”. Aliweka nukta Mzee Mkomwa kwa maelezo yenye kushawishi nami nikawa sina budi kuitikia "Sawa".
Sasa ukawa ni muda muafaka wa mimi kumuuliza Mzee Mkomwa kuhusu yule msichana na kwanini alinihusianisha nae na ndoto yangu. Nikajaribu kutafuta swali zuri ambalo lingemshawishi kunijibu, nikalikosa, nikaamua niulize moja kwa moja lakini kimitego..
“Kwahiyo babu umenambia yule mwanamke atanisumbua sana, eti?”
“Sana” Mzee Mkomwa akajibu kifupi. Nikatulia kwa dakika nzima kujua labda ilkuwa ni nukta fupi, lakini sikuona ishara za Mzee Mkomwa kuendelea na maongezi yake. Nikaona nitafute swali jingine.
“Kwahiyo nitakuwa nae karibu ina maana yule huko mbeleni?”
Swali hili lilimfanya Mzee Mkomwa kusimama, akaniangalia kisha akaniambia..
“Unatakiwa uwe mwanaume shupavu, kabiliana na kila tatizo unalokutana nalo, usiwe muoga wa mambo, maisha hayataki papara. Wao matajiri na sisi masikini wote tupo katika dunia hiihii.. Hutakiwi kujenga uoga, jiamini.. Na ukipata fursa itumie kwa kuamini ulistahili kuwa nayo, turudi nyumbani Al'Wattan muda umekwenda sana”. Babu alimaliza maelezo yake, kama kawaida yake, mafumbo ndio majibu ya maswali ninayomuuliza. Mpaka sasa sikujua kuwa alimaanisha nini?!! Na kwanini hanielezi kwa undani?!.
Tukageuza na kurudi nyumbani na kulala.

Kulipokucha asubuhi, nikakaa pale nje ambapo Mzee Mkomwa alinikuta jana na kunieleza tafsiri ya ndoto yangu, haukupita muda Mzee Mkomwa akaja, tukakaa na kuongea mambo mengi ya kimaisha.. Aliniusia vitu vingi, na nikajifunza vingi sana kutoka kwake.
Jua lilitukuta pale, na muda wa kupanga mahindi barabarani ulifika. Nikamuaga babu na kuelekea barabarani na viroba, Mzee Mkomwa hakutia neno kama ilivyokuwa jana.
Nilipofika barabarani tu na kuweka viroba, gari moja nzuri yenye namba za kiserikali ikasimama pale pembeni yangu.
“Habari yako kijana?” aliuliza dereva ambaye alikuwa peke yake kwenye gari ile mara baada ya kushusha vioo vya mbele ambapo alikuepo.
“Nzuri Mzee shikamoo” nilimkadiria umri wake na kumuona alistahili heshima yangu.
“Marahaba, naomba viroba vyote hivyo hapo..” Alisema kisha akashuka na kunisaidia kubeba kupandisha nyuma kwenye gari ile.
“Ni bei gani?”
“Elfu thelathini vyote viwili”
Baada ya jibu hili, aliingiza mkono mfuko wa shati lake na kutoa noti za elfu kumi kumi tatu na kunikabidhi.
“Ni mahindi mazuri?” Aliuliza mara baada ya kunikabidhi zile noti.
“Sana Mzee, na karibu tena” nilijibu huku nikitabasamu.
“Ok, hebu nipatie namba yako ya simu huenda nikahitaji tena wakati narudi nyumbani, maana kwa sasa naenda kikazi huko mkoani” alisema Mzee yule na kunifanya nishtuke kidogo.
“Sina simu mzee, ila wewe ukipita hapa mimi nipo tu siku zote yani wala usihofie, wewe ukifika hapa piga honi tu” Nilijisemesha huku nikikenua meno kama ambaye nilipata taarifa kuwa naenda peponi.
“Hapana, hatuendi hivyo katika dunia ya leo, shika simu hii, nitakutafuta nikiwa narudi.. Cha msingi hakikisha haizimi tu” Alisema yule Mzee na kunikabidhi simu, kisha kabla sijamshukuru alishawasha gari na kuondoka.. Nikajikuta napayuka kwa sauti kubwa “ASSSAAAANTEEE MZEEE” kisha nikaondoka mbio hadi kwa Mzee Mkomwa.
“Babuuu babuuu..” Niliita huku nikiwa nahema sana kutokana na mwendo niliokuja nao. Nilishangazwa na muonekano wa babu ambaye nilimkuta amekodoa macho pale kwenye kigoda alichokuwa amekalia, mdomo ukiwa wazi huku akihema kwa nguvu. Macho yake meupe yalionesha ishara kama yamegeuka upande.
Nikaingia ndani mbio kumuita bibi ambaye alikuja na kumuangalia vizuri, nikamuona anaanza kumwagikwa na machozi.
“Tumpeleke ndani haraka” Bibi aliniomba na kumbeba Mzee Mkomwa hadi ndani.
“Tumpeleke hospitali basi bibi” Nilitoa wazo mara baada ya kufika pale ndani.
“Tumpeleke maiti hospitali kwani kuna makaburi kule?” Bibi aliniuliza na kuniacha nimeduwaa.
Nikamtazama tena babu kwa umakini sana, nikagundua kuwa pumzi zilishakata. Nikajaribu kumtingisha, nikashtukia kofi zito kutoka mgongoni.
“Babu yako ameshafariki huyo, tuandae mazingira tu humu ndani yawe safi, kisha tuanze kutoa taarifa” Alisema bibi na kumfunika babu shuka.
Ikanibidi nijikaze ili nianze kufanya usafi wa nyumba kabla hatujaanza kulia kwa nguvu na watu kujaa mle ndani. Nikashika fagio na usafi ukaanza mara moja.
Tulifanikiwa kusafaisha nyumba yote nikisaidiana na bibi na dada yangu Mwanauzi. Kisha nikatoka na kuanza kutoa taarifa kwa majirani na wanafamilia. Watu wakaanza kukusanyika nyumbani, wengi wakishangazwa na kifo cha ghafla cha Mzee Mkomwa.
“Mimi nimetoka msikitini asubuhi nikamkuta hapa nje, tukasalimiana na akaniambia yeye ni mzima kabisa.. Sasa ninapoambiwa amefariki, nashangaa” Alisema Mzee Mmoja ambaye alikuwa rafiki sana na Mzee Mkomwa.. Yeye aliitwa Mzee Mtindi. Nikatoa mikeka na majamvi yaliyokuwa mle ndani, nikaweka chini ya miti pale nje ya nyumba yetu, watu wakawa wamekalia huku wakizidi kuongezeka.
Katika harakati za kupita pita huku na kule kuhakikisha taarifa zinasambaa na kuona mambo yote yanaenda sawa, nikajikuta nimekutana uso kwa uso na sura ngeni ambayo sikuwahi kuiona pale kijijini. Tukaangaliana, kisha akanishika mkono na kunivutia pembeni kabisa mbali na nyumbani bila kusema chochote. Tulipokuwa tupo mbali na watu, huku nikiwa muoga na sijui hatma yangu, yule Mzee akaanza kuniambia..
“Naitwa Subiani, rafiki wa Mzee Mkomwa” Alianza kueleza yule Mzee. Nilibaki nimeduwaa, nikaamua niulize swali maana Mzee Mkomwa alinisiisitiza sana kutokuwa muoga.
“Subiani, ??!! Kwani wewe jini? Hayo si majina ya kijini mzee wangu?” Niliuliza kwa hamaki lakini kwa kujiamini.
“Hujakosea hata kidogo, mimi ni jini, nina maelekezo yako muhimu kutoka kwa Mzee Mkomwa, ukimaliza msiba nitakuja kukupatia.. Ila kwa sasa shika hii..” Alisema yule Mzee na kunikabidhi kikaratasi kidogo kilichozungushiwa uzi mweusi.
“Ya nini hii?” Niliuliza.
“Hiyo ni kinga yako, hapa kwenye msiba kuna maadui wengi sana ambao wanataka kuvunja matokeo yote ya ndoto yako..Mimi nitakuja tena Ijumaa” Alisema yule Mzee mimi nikiwa nimekodolea macho kile kikaratasi kilichoonekana mfano wa hirizi.
“Sawa” niliitikia nikinyanyua shingo kumuangalia, lakini cha ajabu sikuona mtu.

★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★
USIKOSE SEHEMU YA NNE
 
Back
Top Bottom