Mdharuba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2011
- 824
- 521
RIWAYA: HISTORIA BATILI(Fake History)
MTUNZI: Jumaa Khatib Mdharuba (Jk)
+255 718 274 130
SEASON 01-EPISODE 01
★★★★★★★★★★★★★★★
"Mume wangu, huendi kazini leo??" Aliongea Sauda Ally ikiwa ni Majira ya saa 3:30 asubuhi, hii ilikua sio kawaida ya bwana Khatib Jumaa kuwa ndani mpaka muda ule.
"Leo sitoki" alijibu kifupi akiwa bado yupo kitandani akiwa busy na simu yake..
"Ok sawa, mi nipo uani nafua kidogo".
"sawa". Alijibu bwana Khatib na kuendelea na ubize wake..
"Haloo Nira Saire..mimi leo sitokuja kazini kabsaa..naomba muendlee na kazi kesho mtanipa ripoti kamili." alisema maneno hayo baada ya simu kupokelewa upande wa pili.
★★★★★★★★★★★★★
Jumaa Khatib Mdharuba, kama alivyofahamika, alikua akijulikana kama kijana aliyekulia katika maisha ya kitajiri sana, mtu ambaye hakuwahi kuonja ladha ya shida katika maisha yake. Kipindi hiki akiwa na umri wa miaka 27 tu alikua akimiliki yard kubwa sana ya magari iliyokuwepo mkoani Morogoro. Alikua akifanya kazi yake kwa ufanisi mkubwa kiasi cha kuwa na wateja wengi wa uhakika kuliko hata wale washindani wake ambao walimiliki yard hizo katika majiji makubwa kama Dar, Arusha, Tanga na Mwanza. Aliuza magari yake kwa bei nafuu na yalikua na warranty ya zaidi ya miaka mitatu. Alimudu kufanya kazi yake vizuri sana, akawa anaishi maisha safi sana. Mpaka sasa alishaweza kutoa ajira kwa vijana 15 ambao walikua wakishiriki ktika shughuli tofaut katika yard ile, wakiongozwa na Nira Saire kama kiongozi msimamizi wa wafanyakazi wa pale. Nira Saire alikua akimuheshimu sana bwana Khatib kwa sababu alikua akiishi nae vizuri na vilevile yeye ndiye aliyekua analipwa mshahara mkubwa zaidi kuliko wafanyakazi wote wa pale. Mara zote Khatib asipokuwepo majukumu ya kusimamia yalibaki kwa Nira.
Nira alijaribu kutengeneza urafiki wa karibu saana na Khatib nje ya kazi, lakini jambo hili linaonekana Khatib hakulipenda saana.. yeye alitaka awe anashirikiana nae zaidi kwenye kazi tu na kutoruhusu saana wazoeane nje ya mazingira ya kazi..Nira alilishtukia hili na akaamua awe mpole tu, kwanza aliamini watu wenye pesa walikuwa na dharau sana..
Sauda Ally, mke wa Khatib, alijitahidi sana kuweka mapenzi ya dhati kwa mumewe ambaye alikua na miaka miwili sasa kwenye ndoa, ingawa Khatib hakuonekana kujali sana. Alikua busy sana na mambo yake na mara nyingi akirudi nyumbani alikua akipanda kitandani na kulala..hakuwa na muda wa kupiga story na mkewe wala kuongelea maisha yao yanaendaje..
Matendo yake yalikua yakishangaza watu wengi saana, na kila mmoja alikua akimtafsiri tofauti. Alijitolea sana kusaidia masikini na yatima na walemavu ila hakutaka chombo chochote cha habari kihusike katika misaada hiyo. Alikua akitoa misaada kimyakimya na akitembelea kituo kimoja anatoa zaidi ya mil.50!! Alifanya hivyo kwa zaidi ya miaka mitano sasa..
★★★★★★★★★★★★★
Maelezo ya utajiri wa Khatib na mambo anayoyafanya yalishangaza watu wengi sana..hakua na dharau wala kiburi kwa mtu yeyote, ila swali kubwa lililokuwa akilini mwa watu wengi ni kuwa "Kwanini anafanya kwa siri sana?"
Mambo yake aliyaendesha kwa siri kubwa,licha ya kumiliki yard ya magari lakin tathmini ya utajiri wake ni zaidi ya hapa.!! hela zingine anatoa wapii?? Na watu wote walijua kuwa alikua akitokea katika familia ya kitajiri akimtambulisha Noor A Mdharuba kama baba yake mdogo na mlezi wake anayeishi naye hapa Tanzania wakati babayake mzazi alkua akiishi nchini Canada akiwa ni Manager wa benk moja ya biashara nchini humo.. Mara nyingi Khatib alikua akisafiri kwenda Canada kuonana na baba yke Mzazi Mzee Jumaa Mdharuba.
Ni Noor ndiye aliyemshawishi Khatib kuoa mapema ili awe na familia yake.
"Ila mimi sina hata mwanamke kwa sasa, ntamuoa nani?" Alihoji bwana Khatib kipindi hcho..
"Kazi ndogo mwanangu, hiyo kazi ntamwachia Bi Nuro Ahmed aniangalizie nani anaweza kuwa mke wa kuolewa na wewe.." Alipangua hoja bwana Noor na kumfanya Khatib akubaliane nae..
Bi Nuro Ahmed ambaye alikua ni mmiliki wa kituo kikubwa cha malezi na shule kwa watoto wadogo, alikuwa na wafanyakazi wote wa kike katika kituo kile. Hivyo alikuwa akiwafaham vizuri tabia zao na misimamo yao katika maisha. Aliweza kufanikisha zoezi na kufanya bwana Khatib amuoe Sauda Ally ambaye Nuro ndiye aliyempendekeza.
★★★★★★★★★★★★★★
"Mama, Khatib yupo huko kwako?" Alikua ni Sauda akiongea baada ya salamu kumuulizia Mama yake Mzazi Khatib ambaye alikua akiishi Mbezi jijini Dar..
"Hapana mwanangu, kwani vipi hajakuaga alipotoka?"
"Aliniaga kuwa anaenda kazini, lakini sio kawaida yke kutorudi mpaka sasa.."
"Ucjali mwanangu, si wajua wanaume tena wanakutana na mengi sana katika kutafuta" Mama Mdharuba Alijaribu kumliwaza mkwe wake licha ya kuwa hakujua Sauda alikua anajickiaje..
Kwa miaka miwili aliyoishi nae alishamfaham vizur Khatib ni mtu wa aina gani, mwanzo ilikua ngumu lakin baadae alizoea tabia ya Khatib kutoka na baadae kupiga simu kuwa yupo sehemu tofaut na aliyoaga.. lakini leo ni tofaut, haijawahi kutokea akatoka na kuchelewa kurudi kias kile na mbaya zaidi simu yake haipatikani!! Sauda alijawa na wasiwasi sana na kupiga simu sehemu zote ambazo mumewe angeweza kupatikana.. lakini hakufanikiwa..chakula cha jioni pia kilimshinda kula..sasa ilikua yapata majira ya saa 6:48 usiku, haelewi nini afanye..!!
Akajaribu kukumbuka matukio ya siku hyo tangu asubuhi, akakumbuka kitu ambacho kilimshtua kidogo!!
Akanyanyuka pale kitandani na kwenda katika meza ndogo iliyokuwepo chumbani mle..akavuta droo yake na kutoa kibunda cha pesa na kuanza kuhesabu.
Akagundua zilikua ni milioni moja na laki moja!! Akatafakari kwa muda na kuishirikisha akili yake katika kufikiri, akajikuta anaangua kilio!!.
★★★★★★★★★★★★★★
Don't Miss Episode 02
MTUNZI: Jumaa Khatib Mdharuba (Jk)
+255 718 274 130
SEASON 01-EPISODE 01
★★★★★★★★★★★★★★★
"Mume wangu, huendi kazini leo??" Aliongea Sauda Ally ikiwa ni Majira ya saa 3:30 asubuhi, hii ilikua sio kawaida ya bwana Khatib Jumaa kuwa ndani mpaka muda ule.
"Leo sitoki" alijibu kifupi akiwa bado yupo kitandani akiwa busy na simu yake..
"Ok sawa, mi nipo uani nafua kidogo".
"sawa". Alijibu bwana Khatib na kuendelea na ubize wake..
"Haloo Nira Saire..mimi leo sitokuja kazini kabsaa..naomba muendlee na kazi kesho mtanipa ripoti kamili." alisema maneno hayo baada ya simu kupokelewa upande wa pili.
★★★★★★★★★★★★★
Jumaa Khatib Mdharuba, kama alivyofahamika, alikua akijulikana kama kijana aliyekulia katika maisha ya kitajiri sana, mtu ambaye hakuwahi kuonja ladha ya shida katika maisha yake. Kipindi hiki akiwa na umri wa miaka 27 tu alikua akimiliki yard kubwa sana ya magari iliyokuwepo mkoani Morogoro. Alikua akifanya kazi yake kwa ufanisi mkubwa kiasi cha kuwa na wateja wengi wa uhakika kuliko hata wale washindani wake ambao walimiliki yard hizo katika majiji makubwa kama Dar, Arusha, Tanga na Mwanza. Aliuza magari yake kwa bei nafuu na yalikua na warranty ya zaidi ya miaka mitatu. Alimudu kufanya kazi yake vizuri sana, akawa anaishi maisha safi sana. Mpaka sasa alishaweza kutoa ajira kwa vijana 15 ambao walikua wakishiriki ktika shughuli tofaut katika yard ile, wakiongozwa na Nira Saire kama kiongozi msimamizi wa wafanyakazi wa pale. Nira Saire alikua akimuheshimu sana bwana Khatib kwa sababu alikua akiishi nae vizuri na vilevile yeye ndiye aliyekua analipwa mshahara mkubwa zaidi kuliko wafanyakazi wote wa pale. Mara zote Khatib asipokuwepo majukumu ya kusimamia yalibaki kwa Nira.
Nira alijaribu kutengeneza urafiki wa karibu saana na Khatib nje ya kazi, lakini jambo hili linaonekana Khatib hakulipenda saana.. yeye alitaka awe anashirikiana nae zaidi kwenye kazi tu na kutoruhusu saana wazoeane nje ya mazingira ya kazi..Nira alilishtukia hili na akaamua awe mpole tu, kwanza aliamini watu wenye pesa walikuwa na dharau sana..
Sauda Ally, mke wa Khatib, alijitahidi sana kuweka mapenzi ya dhati kwa mumewe ambaye alikua na miaka miwili sasa kwenye ndoa, ingawa Khatib hakuonekana kujali sana. Alikua busy sana na mambo yake na mara nyingi akirudi nyumbani alikua akipanda kitandani na kulala..hakuwa na muda wa kupiga story na mkewe wala kuongelea maisha yao yanaendaje..
Matendo yake yalikua yakishangaza watu wengi saana, na kila mmoja alikua akimtafsiri tofauti. Alijitolea sana kusaidia masikini na yatima na walemavu ila hakutaka chombo chochote cha habari kihusike katika misaada hiyo. Alikua akitoa misaada kimyakimya na akitembelea kituo kimoja anatoa zaidi ya mil.50!! Alifanya hivyo kwa zaidi ya miaka mitano sasa..
★★★★★★★★★★★★★
Maelezo ya utajiri wa Khatib na mambo anayoyafanya yalishangaza watu wengi sana..hakua na dharau wala kiburi kwa mtu yeyote, ila swali kubwa lililokuwa akilini mwa watu wengi ni kuwa "Kwanini anafanya kwa siri sana?"
Mambo yake aliyaendesha kwa siri kubwa,licha ya kumiliki yard ya magari lakin tathmini ya utajiri wake ni zaidi ya hapa.!! hela zingine anatoa wapii?? Na watu wote walijua kuwa alikua akitokea katika familia ya kitajiri akimtambulisha Noor A Mdharuba kama baba yake mdogo na mlezi wake anayeishi naye hapa Tanzania wakati babayake mzazi alkua akiishi nchini Canada akiwa ni Manager wa benk moja ya biashara nchini humo.. Mara nyingi Khatib alikua akisafiri kwenda Canada kuonana na baba yke Mzazi Mzee Jumaa Mdharuba.
Ni Noor ndiye aliyemshawishi Khatib kuoa mapema ili awe na familia yake.
"Ila mimi sina hata mwanamke kwa sasa, ntamuoa nani?" Alihoji bwana Khatib kipindi hcho..
"Kazi ndogo mwanangu, hiyo kazi ntamwachia Bi Nuro Ahmed aniangalizie nani anaweza kuwa mke wa kuolewa na wewe.." Alipangua hoja bwana Noor na kumfanya Khatib akubaliane nae..
Bi Nuro Ahmed ambaye alikua ni mmiliki wa kituo kikubwa cha malezi na shule kwa watoto wadogo, alikuwa na wafanyakazi wote wa kike katika kituo kile. Hivyo alikuwa akiwafaham vizuri tabia zao na misimamo yao katika maisha. Aliweza kufanikisha zoezi na kufanya bwana Khatib amuoe Sauda Ally ambaye Nuro ndiye aliyempendekeza.
★★★★★★★★★★★★★★
"Mama, Khatib yupo huko kwako?" Alikua ni Sauda akiongea baada ya salamu kumuulizia Mama yake Mzazi Khatib ambaye alikua akiishi Mbezi jijini Dar..
"Hapana mwanangu, kwani vipi hajakuaga alipotoka?"
"Aliniaga kuwa anaenda kazini, lakini sio kawaida yke kutorudi mpaka sasa.."
"Ucjali mwanangu, si wajua wanaume tena wanakutana na mengi sana katika kutafuta" Mama Mdharuba Alijaribu kumliwaza mkwe wake licha ya kuwa hakujua Sauda alikua anajickiaje..
Kwa miaka miwili aliyoishi nae alishamfaham vizur Khatib ni mtu wa aina gani, mwanzo ilikua ngumu lakin baadae alizoea tabia ya Khatib kutoka na baadae kupiga simu kuwa yupo sehemu tofaut na aliyoaga.. lakini leo ni tofaut, haijawahi kutokea akatoka na kuchelewa kurudi kias kile na mbaya zaidi simu yake haipatikani!! Sauda alijawa na wasiwasi sana na kupiga simu sehemu zote ambazo mumewe angeweza kupatikana.. lakini hakufanikiwa..chakula cha jioni pia kilimshinda kula..sasa ilikua yapata majira ya saa 6:48 usiku, haelewi nini afanye..!!
Akajaribu kukumbuka matukio ya siku hyo tangu asubuhi, akakumbuka kitu ambacho kilimshtua kidogo!!
Akanyanyuka pale kitandani na kwenda katika meza ndogo iliyokuwepo chumbani mle..akavuta droo yake na kutoa kibunda cha pesa na kuanza kuhesabu.
Akagundua zilikua ni milioni moja na laki moja!! Akatafakari kwa muda na kuishirikisha akili yake katika kufikiri, akajikuta anaangua kilio!!.
★★★★★★★★★★★★★★
Don't Miss Episode 02