ENDELEAâ¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦â¦..
Ni saa mbili za usiku familia nzima imekaa
sebuleni.Mzee Zakaria amekwisha toka
hospitali baada ya madaktari kuridhika na
maendeleo yake.Pamoja nao sebuleni
alikuwepo pia David ambaye alikuwa kimya
sana.
â David .! akaita mzee Zakaria na kumtazama
David
â Naam mzeeâ akaitika David na kuelekeza
shingo yake alipokuwa amekaa mzee Zakaria
âNapenda kwa niaba ya familia yangu
nikushukuru sana kwa msaada wako
mkubwa.Uliyaokoa maisha yangu.Bila wewe
sijui hivi saa ningekuwa katika hali
gani.Nadhani ilikuwa ni kwa maongozi ya
Mungu nipite njia ile ili nikutane nawe.Nasema
ahsante sanaâ akasema mzee zakaria
â Nashukuru mzee.Nilifanya jambo ambalo
linapaswa kufanywa na mtu yeyote mwemye
ubinadamuâ akasema David
â Jambo la pili ambalo nataka nikushukuru ni
kwa uaminifu wako mkubwa.Ulinifikisha
hospitali ukahakikisha nimepata
matibabu,ukawasiliana na familia yangu na
alipokuja Pauline ukamkabidhi kila kitu
ukiwemo mkoba uliokuwa na fedha zaidi ya
shilingi milioni themanini.Ni vigumu sana
kuamini lakini ni kweli ulifanya jambo
hili.Katika dunia ya sasa ni vigumu kuwapata
watu wenye uaminifu kama wako.Nasema
ahsante sana na ninakuomba uendelee na
uaminifu huo si kwangu mimi tu hata kwa
watu wengine .Ungeweza kuondoka na mkoba
ule wenye mamilioni ya fedha pamoja na gari
lakini hukufanya hivyo.Ahsante sana davidâ
akasema mzee Zakaria na David hakujibu kitu
akatabasamu.Vicky ambaye alikuwa amekaa
pembeni ya mumewe akiwa na glasi iliyoja
mvinyo akaweka glasi mezani na kuuliza
â David nasikia ulikuwa umefungwa gerezani?
David akawaangalia wote kwa zamu halafu
akasema
âNi kweli nilikuwa nimefungwa na siku
niliyokutana na mzee ni siku ambayo nilikuwa
nimemaliza adhabu yangu na nikaachiwa
huruâ akasema David
âPole sana david lakini tungependa kufahamu
ulifungwa kwa kosa gani? akauliza tena
Vicky.Mzee Zakaria na Pauline wote
wakamuangalia lakini hakujali akayaelekeza
macho yake kwa David
âMama ni historia ndefu sana na samahani
wkani sitaki kuyaongelea mambo ambayo
yamepita.â Akasema david
â jaribu kutueleza hata kidogo ili tupate walau
picha ni kitu gani hasa kilisababisha
ukapelekwa kule gerezani? Akauliza tena
Vicky.David alionyesha kutokupendezwa na
swali ile akainama chini na kuanza kufikiri.
â Naomba David asiulizwe jambo lolote
linalohusiana na matatizo yaliyomkuta.Nao
mba aachwe atulie na atatueleza yeye
mwenyewe kama akipenda kutueleza pale
atakapokuwa tayari kufanya hivyoâakasema
mzee Zakaria.Mke wake akamtazma usoni na
kuonyesha kutokuridhishwa na kauli ile ya
mume wake
â Honey ,sijamuuliza kwa ubaya , lengo langu
ni kumfahamu David kiundani ,ametoka
wapi,na nini malengo yake ya usoni baada ya
kutoka kifungoniâ akasema Vicky
â Naomba mjadala kuhusu David ufungwe
rasmi na sitaki kusikia mtu yeyote akimuuliza
kitu chochote kile kuhusiana na maisha yake
au wapi ametoka.Atatueleza pale
atakapokuwa tayari.â Akasema mzee Zakaria
halafu akamgeukia david
â David utakaa hapa nyumbani kwangu kwa
muda wote utakaouhitaji wewe
mwenyewe.Hapa ni nyumbani kwenu na usiwe
na hofu yoyote.Nitakulea kama mmoja wa
wanafamilia yangu kutokana na msaada wako
mkubwa ulionisaidia.Endapo una tatizo lolote
naomba usisite kunieleza mimi au mama yako
hapa au mweleze Pauline lakini ningependa
kama una tatzio lolote uje unione mimi
mwenyewe.Sihitaji kufahamu umetoka wapi na
ulifanya nini ukafungwa gerezani ila
ninachofahamu nikwamba umenifanyia jambo
ambalo sijawahi kufanyiwa katika maisha
yangu na ambalo sioni kitu ninachoweza
kukufanyia ambacho kinaweza kulingana na
jambo ulilonifanyia.Jisikie amani hapa
nyumbani.â Akasema mzee Zakaria.Vick
akaingilia kati na kusema
â Baba Pauline sioni kama unafanya
sawa.Huyu ni mtu ambaye umekutana naye
mtaani na hujui ametoka wapi,ndugu zake
wako wapi.Itakuwaje iwapo atapatwa na
matatizo akiwa nyumbani kwetu? Akauliza
Vicky
âNimekwisha sema kwamba David atakaa
hapa nyumbani kama mwanafamilia na sitaki
maswali juu yake yaendelee kuulizwa.Ndugu
zake ni sisi hapa.Ndugu yake ni mimi hapa
aliyenisaidia na kuniokoa.â Akasema mzee
Zakaria akionyesha kukerwa na tabia ile ya
mke wake.David aliyekuwa akiyashuhudia
mabishano yale kati yam zee zakaria na mke
wake akasimama na kusema
â Samahani mzee wangu.Nashukuru sana kwa
msaada wako mkubwa na kunisaidia niweze
kuishi hapa nyumbani kwako. Ni kweli
nilipotoka gerezani sikuwa na sehemu ya kula
wala kulala na sikujua ningeelekea
wapi.Sikuwa na mwelekeo wowote wa maisha
lakini mlinipokea katika familia
yenu.Mmenilea kama mwanafamilia
yenu.Pamoja na hayo mzee wangu ningeomba
nisiwe chanzo cha mvurugano katika familia
yako.Ningeomba uniruhusu niondoke
nikaendelee na maisha yangu mahala
pengine.. â akasema David
â David nimekwisha sema kwamba wewe ni
mmoja wa wanafamilia hii na utaishi hapa na
kauli yangu ni ya mwisho.Hutakwenda
sehemu yoyote ile.Utakaa hapa hapaâ
akasema mzee Zakaria kwa ukali kidogo
halafu akainuka na kuelekea chumbani kwake
na kisha mke wake naye akainuka na
kumfuata
â Pauline inaonekana mama yako
hajapendezwa kabisa na mimi kuwepo hapa
numbani.Sipendi niwe chanzo cha
matatizâ¦â¦â¦â¦â¦.â David hakumaliza sentensi
yake Pauline akamkatisha
â Shhhhhhhhhhhhhh..!! usiseme chochte
David.Baba amekwisha sema na utaendelea
kukaa hapa hapa kwetu.â Akasema Pauline na
kimya kifupi kikapita halafu akasema
â David kesho kuna mzigo nitaupokea dukani
kwangu.Ningeomba uambatane nami
ukanisaidie kuupakuaâ akasema Pauline
â Pauline unafanya biashara gani? akauliza
David
â Nina fanya biashara ya nguo.Nina duka la
nguo â akasema Pauline kisha wakaendelea
kuangalia filamu
**********************************
Saa tatu za asubuhi siku iliyofuata David na
Pauline wakaingia garini na kuelekea katika
ofisi za kampuni moja ya usafirishaji ambayo
walimsafirishia mizigo yake.Baada ya kulipa
pesa aliyokuwa anatakiwa kuilipa,mizigo yake
ikapakiwa katka gari la mizigo na kupelekwa
dukani kwake ikashushwa na kuhifadhiwa
katika chumba cha kuhifadhia mizigo.Baada
ya kumaliza kazi ile ya kuhifadhi mizigo
ile,Pauline akaendelea kuangalia hesabu za
duka lake na baadae wakaelekea katika hoteli
moja nzuri kwa ajili ya kupata chakula cha
mchana.
â Hongera Pauline,duka lako zuri sana.Lina
nguo nzuri â akasema David .Pauline
akatabasamu na kusema
â Ahsante sana David umenisaida mno siku ya
leo.â
Wakaendelea kula kimya kimya halafu Pauline
akauliza
â David umewahi kufanya biashara?
David akatabasamu kidogo na kusema
âNina shahada ya biashara na nina uzoefu
katika masuala ya biasharaâ akasema david
na kumfanya Pauline amshangae
â kweli? Akauliza Pauilne
â Kweli Pauline.Nina shahada ya biashara
toka katika chuo kikuu cha dare s salaam na
nina uzoefu katika biashara na masoko.â
akasema David
âWow ! basi ni maongozi ya Mungu amekuleta
kwetu.Nadhani baba atafurahi sana akisikia
kwamba una elimu ya biashara.Kwa muda
mrefu amekuwa akitafuta mtu
atakayemuamini wa kumsaidia katika
biashara zake.â
â baba yako anajishughulisha na biashara
gani?
â ana miradi mingi tu.Ana maduka ,miradi ya
mbao,vituo vya mafuta n.k
â Ouh kumbe baba yako ni tajiri sanaâ
akasema David
â Siwezi kukataa kwamba baba yangu ana
utajiri mkubwa lakini kwa siku za hivi karibuni
ameingia katika mgogoro mkubwa wa kifedha
baada ya kumuoa mama mdogo.Biashara
zake zimekuwa zikiyumba sana na kuna
biashara zake imemlazimu kuzifunga
kutokana na kuendeshwa kihasara.â
â Nini hasa tatizo la mama yako mdogo?
â mama mdogo ana matatizo
makubwa.Kwanza si muaminifu na ni mfujaji
sana wa fedha na nina wasi wasi anaficha
fedha kwa siri.Niliwahi kumueleza baba
kuhusu jambo hili lakini likazua matatizo
makubwa na nikaamua kuachana na biashara
za familia nikaanzisha biashara yangu.Toka
wakati huo baba amekosa mtu wa karibu wa
kumuamini.Lakini kwa siku za karibuni
ameanza kukubaliana na maneno yangu
kuhusiana na mama mdogo.â Akasema
Pauline
âPauline nasikitika sana kwamba sintakubali
kufanya kazi kwa baba yako na kukutana na
mtu mwenye tabia kama za mama yako
mdogo.Sitaki kuingia katika mgogoro
mwingine hasa kwa wakati huu ambao
nahitaji kuyajenga upya maisha yanguâ
akasema David
âDavid tafadhali naomba usikatae.Nitaongea
na baba ili uweze kumsaidia na
utakapomsaidia baba utakuwa umenisaidia na
mimi vile vile.Iâm your friend ..right? akasema
Pauline
â Ndiyo Pauline mimi nawe ni marafiki lakini
najaribu kuyakwepa matatizo hasa kwa wakati
huu ambao ninaanza kuyajenga upya maisha
yangu.â
â David tafadhali naomba usikatae.Kama
huwezi kufanya kazi kwa baba do it for
me.Nisaidie mimi.Familia yangu inakuhitaji
sana na Mungu amekuelekeza kwetu ili uweze
kutusaidia.Tafadhali naomba usiseme
hapana.Baba kwa sasa anaumwa na anahitaji
mtu wa kuweza kumsaidia katika kazi zake
hasa kwa wakati huu ambao hana imani tena
na mama mdogo kutokana na vitendo vya
ufujaji wa fedha alivyovionyesha.Alinitaka
mimi nirudi kuisimamia miradi ya familia ili
kumpa yeye nafasi ya kupumzika lakini wakati
nikitafakari nitawezaje kufanya hivyo
umetokea wewe .David naomba usikatae
kutusaidiaâ akasema Pauline.David akainama
akaonekana kuzama katika mawazo mengi.
â Nataka kujiingiza tena katika matatizo
ambayo ninajaribu kuyakimbia lakini nahisi
kushindwa kukataa kuwasaidia akina Pauline
katika kuisimamia miradi yao.Ni watu wazuri
wenye roho nzuri na moyo wa
ukarimu.Wamenikaribisha nyumbani kwao na
wananitunza kama mmoja wa
wanafamilia.Mzee zakaria ameonyesha
kuniamini lakini tatizo liko kwa mke
wake.Anaonekana kutokufurahishwa na uwepo
wangu pale katika familia yao na ndiyo
maana jana usiku alikuwa akijaribu kutaka
kuyachimba maisha yangu.Endapo mzee
Zakaria ataridhika nami na kuniomba
nimsaidie katika majukumu itanilazimu
kukubali na pengine hii inaweza kuwa ni fursa
yangu ya kuyatengeneza upya maisha yangu
yaliyopoteza mwelekeo.â Akawaza David
halafu akamtazama Pauline wote
wakatabasamu
â Toka nilipokutana naye niliamini kuna kitu
ambacho kimejificha kwa david.Kumbe bi
kijana msomi na ana shahada ya
biashara !!..Kuna mambo mengi ambayo
yamejificha nyuma yake ambayo hataki
kuyaweka wazi.Kwa nini hataki kuiweka wazi
historia yake? Ametoka wapi na famili yake
iko wapi? Kwa nini alifungwa gerezani?
Amekuwa akiyakwepa kabisa maswali
haya.Kuna haja ya kumfahamu huyu
kijana.Niliwahi kusoma katika simulizi mbali
mbali kwamba kuna watu ambao hujiweka
katika hali kama hii ya David kumbe ni
wapelelezi .Nina wasi wasi sana na huyu
kijana.Kuna nyakati ninaanza kuingiwa na
wasi wasi naye lakini hata hivyo kuna ulazima
wa kumfahamu undani wake na ili
kumfahamu vizuri inabidi kujiwa naye karibu
sana.â Akawaza Pauline
Wakati david na Pauline wakipata chakula cha
mchana,Robin na mfanyakazi wake wa ndani
walikuwa katika pilika pilika za kufanya
manunuzi kwa ajili ya maandalizi ya ujio wa
mwalimu Lucy nyumbani kwao siku
itakayofuata yaani jumamosi.Walifanya
manunuzi ya vitu vingi ambavyo waliona
vingefaa kwa ajili ya siku muhimu kama
ile.Baada ya kuridhika na manunuzi
waliyoyafanya wakarejea nyumbani ambako
maandalizi kabambe yalianza ikiwa ni katika
kuiweka nyumba katika hali ya usafi na
unadhifu wa kipekee kabisa.
***************************************
Vicky alimuaga mumewe mzee Zakaria
kwamba kuna mahala anakwenda na
asingechelewa kurudi.Aliingia katika gari lake
la kifahari na kuondoka na breki ya kwanza
ilikuwa nyumbani kwa rafiki yake kipenzi
Safia.
âVicky umerudi lini ? si uliniambia umekwenda
Morogoro na Yule kijana Danny? Imekuaje
umerudi mapema namna hii? Akauliza Safia
baada ya Vicky kuingia sebuleni kwake.Vicky
akautupa mkoba wake sofani na kuketi halafu
akavuta pumzi ndefu
â Ouh Safia mimi sijui nina mkosi gani
jamani..!! akalalama Vicky ambaye
masikio,shingona vidole vyake vilipambwa
kwa vito vya thamani kubwa
âKwa nini unasema hivyo Vicky? Akauliza
safia huku akimuita mfanyakazi wake wa
ndani na kumuomba awaletee vinywaji
âNilikuwa na Danny katika hifadhi ya
Udzungwa tukila raha za dunia mara kila kitu
kikatibukaâ akasema Vicky
âIlikuaje Vicky? Nini kilitokea? Akauliza Safia
âNilipigiwa simu na Pauline akaniambia
kwamba Yule mzee amepatwa na shinikizo la
damu na amelazwa hospitali.Ikanilazimu
niahirishe kila kitu na kurudi mara
moja.Nimerudi jana mchana .Nimechukia
sana Safia kwa kukatishwa katika starehe
zangu.Nilikuwa nikipata raha za dunia na
Danny na sikupanga kama ningerejea mapema
namna hii.Nimemchukia sana Yule
mzee.Hanikuni nitakavyo lakini ninapompata
mtu anayenikuna kisawasa kinaibuka
kikwazo.Naona ingekuwa vyema kama
angekufa tu ili niendelee na maisha yangu ya
starehe.Nimechoshwa na maisha haya ya
kufungwa ndani kama njiwaâ akasema Vicky
â Dah ! pole sana shoga.Kwa hiyo
anaendeleaje mzee? Akauliza Safasi
â Linaendelea vizuri tu..â akajibu Vicky huku
akibetua midomo yake
âPole sana shoga yangu.Usisikitike sana
.Jaribu kupanga tena miadi na Danny ili
mkutane tena na muendelee na mambo
yenu.Nafahamu ugumu unaoupata kwa yule
mzee .Jitahidi usije ukazeeka shiga
yangu.wewe bado mtoto mbichi kabisaâ
â Safia sijui kama nitaweza kumpata tena
Danny hivi karibuni.tayari amerudi kazini
kwake Botswana.Alikuja kwa dharura ya wiki
mbili na kumuona tena itachukua muda
mrefu.Sijui nitafanyaje mimiâ¦!! Akalalama
Vicky halafu kimya kikapita
âNinavyokwambia mimi nina bahati mbaya
,nimerudi kwagu na kumkuta Pauline
amemuokota muhuni mmoja na kumleta aishi
pale nyumbani kwangu.â
â Muhuni ..!!!? Safia akashangaa
â Mzee Zakaria anaweza kweli kukubali kuishi
na muhuni kwa ninavyomfahamu mzee Yule
alivyo na sheria kali?
â hata mimi sielewi imetokeaje.Yaani Yule
mzee humuelezi kitu kuhusu huyo kijana.
Kijana mwenywe ametoka gerezani na
hajulikani hata kwao ni wapi ,ukitaka
kumuuliza ametokea wapi hajibu na mzee
Zakaria anakuwa mkali kama nini.Shoga
yangu nimekereka sana kwa sababu kwa
namna mzee anavyomuamini Yule kijana
kama hirizi yake ,nina wasi wasi akizoea sana
baadhi ya mambo yangu yanaweza yasiende
sawa.â
â Dah ! hili sasa ni janga â akasema Safia
â janga si kidogo shoga ! yaani akili yangu
haifanyi kazi vizuri.Nataka nimalize nyumba
yangu haraka haraka ili ikiwezekana niachane
na Yule marehemu mtarajiwa.Unajua hata
kama akifariki hivi sasa sintakuwa na changu
pale kwa sababu sijazaa mtoto na Yule mzee
na siwezi kuzaa naye mtoto hata iwe vipiâ
akasema Vicky
âKwa hiyo umepanga nini shoga? Akauliza
safia
â Kuhusu nini safia? Akauliza Vicky
âKuhusu huyo kijana. Utamuacha aendelee
kukaa hapo nyumbani kwako?
â Thubutu !!..labda siyo mimi Vicky
madhahabu..â akasema Vicky na kisha wote
kwa pamoja wakacheka kicheko kikubwa na
kugonganisha mikono.
â namvutia kasi kwanza ili nimsome vizuri
nyendo zake kwa sababu kwanza anaonekana
ni mzubavu na asiyefahamu chochote.Ukimuo
na ni kama aliwahi kuchukuliwa msukuleâ
akasema Vicky halafu wote wakacheka tena
kicheko kikubwa sana
â Lakini Vicky mimi nina wazo moja kuhusu
huyo kijanaâ
â wazo gani Safia?
âHuyo kijana usimfukuze.anaweza akawa ni
mtaji mkubwa sana kwako.â
â Kivipi? Akauliza Vicky
âKama mzee zakaria anamuamini basi
unachotakiwa kukifanya ni kumuweka karibu
yako ili hata kama kuna jambo unalifanya
basi lisimfikie mzee Zakaria au Pauline.Wakati
mwingine wewe ni binadamu na una mahitaji
na hali ya mzee ndiyo kama hivyo
tena,unaweza ukamtumia huyo kijana
akakuliwazaâ akasema Safia halafu Vicky
akacheka sana.
â Ama kweli Safia umenichoka shoga
yangu.Yaani mimi Vicky madhahabu nilale na
Yule kinyago.!!? Hata kama nina hamu ya
namna gani na mwanaume lakini siwezi
kuthubutu kumvulia nguo Yule
kijana.Nakwambia ukimuona utashangaa
utafikiri ni msukule uliotoroka.Hana mbele wa
nyuma.Lakini kuhusu hilo la kwanza
ulilolisema kwamba naweza kuwa naye karibu
nitalifikiria lakini sina hakika kama anaweza
akakubali kushirikiana nami.â akasema Vicky
â Vicky hakuna kitu kinachoshindikana hapa
duniani.Pesa ndiyo inayowezesha kila
kitu.Ukiwa na pesa utaweza kufanya lolote
unalotaka.Hata huyo kijana endapo ataonja
pesa atakuwa tayari kushirikiana
nawe.Inawezekana huko alikotoka alikuwa
kibaka kwa hiyo endapo ataonja maisha
mazuri na ukampatia fungu la kutosha basi
atakufanyia kila unachokitaka.Kuhusu
kumtumia huyo kijana kingono sikuwa na
maana mbaya na wala sikutaka kukushusha
thamani shoga yangu lakini nilikuwa nakupa
tu wazo kwamba endapo unaweza ukazidiwa
na ukahitaji mtu wa kukupa raha basi
unaweza mara moja moja ukamtumia huyo
kijana tena ukiwa hapo hapo kwako bila hata
ya kwenda mbali .Kuhusu muonekano wake
isikupe shaka.Muonekano ni kitu ambacho
kinaweza kubadilishwa wakati wowote.Huyo
huyo unayemuona leo kama msukule akipata
fedha na kujibadilisha ataitwa mheshimiwa.â
Akasema Safia na Vicky akatabasamu na
kusema
â Ok Safia tuachane na hayo ya nyumbani
kwangu, vipi kuhusu mafundi waliendelea na
kuweka milango ? akauliza Vicky
â Ndiyo na hata hivi sasa wako jengoni
wanaendelea na kazi.â
â Nashukuru sana shoga yangu kwa kunisaidia
kusimamia nyumba yangu.Nataka iende
haraka kwa sababu nina mipango mikubwa
sana ndani ya muda mfupi ujao.â Akasema
Vicky huku akilifungua pochi lake
âMipango gani Vicky? Mbona hunishirikishi
mimi shoga yako? Akauliza Safia
â Usihofu safia.Wewe ni mtu wa kwanza
ambaye nitakufahamisha lakini si sasa hivi
hadi hapo kila kitu kitakapokuwa tayari.Kimya
kingi kina mshindo mkuu.Nimekuwa kimya
kwa muda mrefu sasa subiria kusikia mshindo
wake.â Akasema Vicky huku akitabasamu na
kutoa kitita cha dola za marekani na kuanza
kuhesabu kiasi Fulani halafu akampatia Safia
â kamata hizo shoga zitakusaidia kwa mambo
madogo madogoâ akasema Vicky
âDah ! shoga ama kweli wewe si mwenzetu
tena. Siku hizi hutumii tena haya madafu
yetu.Ni mwendo wa madola tuâ akasema Safia
huku akitabasamu
âToka nimezaliwa nilikuwa natumia
shilingi.Kwa hivi sasa nataka nibadili maisha
yangu na kuanza kutumia dola tu.â Akasema
Vicky huku akiinuka sofani
â Safia,mimi si mkaaji nimepita tu kukujulia
hali na kukufahamisha kwamba
nimesharudi.Nataka nielekee mjengoni
nikaangale mafundi wanavyoendelea kisha
nirejee nyumbani kwani lile zee lisiponiona
linaweweseka kama linakata roho.Nitawasili
ana nawe baadae shoga yanguâ akasema
Vicky huku akipiga hatua kuelekea katika gari
lake akaondoka
âSafia amenipa wazo japo la kijinga lakini
linaweza likawa na msaada kwangu.Natakiwa
kumsoma Yule kijana na kumuweka upande
wangu.Endapo nikimtia mkononi anaweza
akanisaidia sana katika mipango yangu
mbalimbali.Nina hakika atakapoonja fedha
hatakuwa na kauli kwangu na nitampeleka
nitakavyo.Hili ni wazo zuri sana.Lakini hili la
kumtumia kingono Yule kijana mhhhh !
inataka moyo sana.Lakini safia yuko sahihi
Yule kijana anaweza akanisaidia kuikata kiu
yangu pale ninapokuwa na hamu.Nina kila
kitu kwa sasa,maisha mazuri,nina fedha za
kutosha na nilichokosa ni kuridhishwa tu
kimwili na Yule mzee kwa sasa kutokana na
hali yake hawezi akanikuna nitakavyo.Mimi ni
mwanamke wa shoka nahitaji dozi ya maana
ili niridhike kitu ambacho Yule mzee hakiwezi
sasa hivi.Danny ananifikisha nitakapo lakini
naye yuko mbali ,laiti kama angekuwa karibu
ningekuwa nakwenda kwake kila siku kupata
huduma .Natakiwa kutafuta namna ambayo
nitakuwa nikijiridhisha.Ninaweza kumtumia
yule kijana lakini mhh ! â akawaza Vicky
wakati akielekea mji mdogo wa Usa river
anakojenga jumba lake la ghorofa mbili
â Kijana mwenyewe mchafu mchafu namna ile
ana thamani kweli ya kuweza kuuona utupu
wangu? Lakini kama alivyosema Safia
ninaweza nikambadili muonekano na akawa ni
kijana nadhifu kabisa.Ngoja nianze kulifanyia
kazi jambo hili.Sitaki mipango yangu
ivurugike.Nitafanya kila niwezalo ili kila kitu
nilichokipanga kiende kinavyotakiwa â
akawaza Vicky
MAMBO YANAZIDI KUKOLEA..DAVID NI NANI
NA KWA NINI HATAKI KUWEKA WAZI KUHUSu
MAISHA YAKE? VICKY ANA MIPANGO GANI?
ATAFANIKIWA LENGO LAKE LA KUMTUMIA
DAVID? TUENDELEE KUWA PAMOJA