mtzmweusi
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 8,698
- 9,051
HEKAHEKA - 1
Mtunzi: Japhet Nyang’oro
Phone: 0762204166
“Jacob, napenda kuolewa ila haiwezekani” Alisema ilhali mikono yake ikiwa bado inaminya minya misuli ya mwanaume huyu huku pia machozi yakiwa yanamtiririka.
“Kwa nini ishindikane Regina? Wewe ni msichana ambaye unaweza kumvutia kila mwanaume mwenye mpango wa kupata mwenza wa maisha?” Jacob aliuliza huku akihisi ubaridi uliokuwa ukipenya taratibu katika kifua chake kutokana na machozi yaliyokuwa yakitoka kwa wingi machoni kwa Regina.
“Hapana haiwezekani Jacob…” Regina alisisistiza kwa sauti ya chini, iliyokuwa na chembe chembe za huba na wasiwasi kwa wakati mmoja.
“Usiseme hivyo Regina!”
“Hata nisiposema, huo ndio ukweli na hali halisi Jacob”
“Naomba sababu ya huko kutowezekana…” Jacob alizidi kuhoji kwa shahuku.
“Hata nikikuambia huwezi badili hali na ukweli wa mambo”
“Umejuaje kama sitoweza?”
“Uko peke yako, wako jeshi, huwezi washinda wote....ni waovu sana!”
“Nakupenda Regina, niko tayari kufanya lolote ili kurejesha uhuru wako na Amani” maneno hayo ya Jacob ilikuwa kama sauti ya muziki mororo inayopenya kwenye kiza kinene na kuyafikia masikio ya mtu aliyesimama chini ya mti mukubwa baada ya kunyeshewa na na mvua nzito.
“Sijawahi kuwa huru na sijui amani ikoje Jacob” alisema Regina huku akimkazia macho Jacob, kamasi nyembamba na machozi vikiendelea kuchuruzika.
Wakati mahojiano hayo yakiendelea, sauti yake Bella wa Akudo Impact ilikuwa ikivuma ukumbini hapo huku yale mashairi ya wimbo wake ‘yako wapi mapenzi? ilimfanya kila aliyekuwepo kujishughulisha zaidi na mwandani aliyekuwa nae. Kwa kifupi hali ilikuwa ni ya kuvutia na utulivu katika ukumbi wa Miami Hoteli ambayo ni moja kati ya hoteli za kuvutia zilizoko kando kidogo ya jiji la Dar es salaam baada ya kupita mbezi beach.
Ni kawaida kwa Jacob Matata kutoka nyakati za jioni na kwenda katika mojawapo ya maeneo ya burudani katika jiji la Dar es salaam. Ukimuuliza mwenyewe kwa nini alipenda kwenda maeneo hayo, sababu nyingi angekupa. Lakini katika orodha yake asingesita kutaja, upweke, burudani na kusafisha macho. Lakini ana jingine ambalo kamwe usingelisikia akilitaja...........kazi....kazi yake ya upelelezi ilimtaka kuwa jirani na jamii, jamii iliyoko kwenye madaraja yote, daraja la juu, daraja la kati na daraja la chini.
Siku hiyo Jacob Matata alijikuta anavutiwa kwenda Miami hoteli. Alisikia Akudo Impact wanapiga huko, na kwa vile yeye ni mpenzi wa muziki wao akaona ni bora akaishibishe nafsi yake kitu inataka. Binafsi anamiliki magari mawili, lakini hakuwa anapenda kwenda sehemu za starehe akiwa anaendesha, hivyo alimtaarifu Abdul mmoja wa vijana wake ambao hupenda kuwakodisha akiwa kwenye mizunguko yake na wakati akiwa hataki kuendesha. Abdul alimpitia Jacob nyumbani kwake maeneo ya Sinza Mori mida ya saa tatu unusu usiku.
“vipi bosi, naona leo umekaa kiburudani Zaidi?” Abdul alimuambia Jacob ambaye alikuwa amevaa fulana ya blue na suluali ya jeans nyeusi.
“Si unajua wazee wa masauti Akudo wako Miami Hotel, sasa nataka nikakate kiu huko” Jacob alisema.
“Ahhh wale jamaa hata mie nawakubali sana” Abdul alijibu.
Saa nne na robo ilimkuta Jacob ameshatulia kitini katika ukumbi wa hoteli ya Miami. Akudo walikuwa wameshaanza kushambulia jukwaa taratibu. Alitafuta sehemu na kukaa, kabla ya kuagiza aletewe vinywaji. Vinywaji vililetwa na taratibu akaanza kujipigilia huku akiyapa fursa macho yake yaweze kutalii katika ukumbi mpana wa hoteli hiyo...kusafisha macho. Jacob aliamua aweke mbili-tatu ili wakati mambo yakichanganya nae awe kamili.
Tangu alipoingia hotelini hapo, Jacob Matata alionekana kuwa mtulivu, japo utulivu ni hali ya kujifunza tu kwake, asili yake ni mtu mchangamfu sana na mtundu unaweza sema. Hata ukienda mitaa aliyokulia pale Mwanza mjini maeneo ya Kirumba mwaloni, ambapo nyumba ambayo wazazi wake walikuwa wamepanga ilikuwa jirani na msikiti wa Taqwa, siku hizi kuna shule ya sekondari ya kiislamu pale, ukiuliza utaambiwa wakati Jacob anakuwa miaka ile ya 1991, wazazi walikuwa wakiwazuia watoto wao wasicheze pamoja nae. Alikuwa mtundu balaa.
Kadri masaa yalivyokuwa yakizidi kukatika, ndivyo ukumbi huo ulivyokuwa ukipungua watu. Pamoja na kuwa kulikuwa na watu wengi wa umri na maumbile tofauti, lakini macho ya Jacob Matata yaligota kwa msichana mmoja aliyekuwa ametulia tuli juu ya kiti upande wa kulia wa ukumbi huo. Alipozidi kumtazama, Jacob aliweza kubaini uzuri wa msichana huyo. Hivyo mara kwa mara macho yake yakawa yanapendelea kuangalia upande alipokuwa amekaa kiumbe huyo wa kike. Dakika kumi baadae Jacob alitupia macho kwa yule msichana mrembo na kubaini kuwa hakuwepo sehemu ile aliyokuwa amekaa.
Wakati anageuza macho katika jitihada za kujaribu kuangaza ili aweze kuona kama bado msichana huyo alikuwepo ukumbini hapo, ndipo macho yake yalipogongana moja kwa moja na yale ya msichana mrembo akiwa amekaa hatua chache tu kwa nyuma yake. Macho yao yalipogongana, yule msichana aliachia tabasamu la kukaribisha. Kuona hivyo, Jacob aliachia lake la mwitikio kisha akasita kidogo. Aliangalia saa yake ya mkononi na kubaini kuwa tayari ilikuwa inaelekea kuwa saa tano na robo usiku. Jacob alisimama, kabla ya kupiga hatua yoyote alizungusha macho yake huku na huko ili kuona kama kulikuwa na lolote, alipooona hakuna aligeuka na kuanza kuelekea alipokuwa amekaa yule mrembo.
Haikuwachukua muda mrefu wakajikuta wameshatambulishana. Muda si muda wakakubaliana kumalizia muda uliobaki kwa kucheza muziki pamoja. Na wakati huo huo ule wimbo maarufu wa ‘yako wapi mapenzi? ulikuwa ukiimbwa kwa ustadi mkubwa nae Bella. Haikuwa siri kuwa kila mmoja katika watu hawa alikuwa amevutiwa na mwenzie.
Sijui kama ndio ilikuwa kosa au la, pale Jacob alipomuuliza msichana huyu kama alikuwa na mtu yeyote. Jibu alilolipata lilikuwa ni lile ambalo Jacob alikuwa anaombea apewe. Kule kusikia kuwa Regina hakuwa na mtu kulimfurahisha sana Jacob. Hapo ndipo akauliza swali la kichokozi na ambalo hata hivyo ndilo liloleta kizaa zaa kinachoendelea.
Wakati huu walikuwa bado wamekumbatiana katika hali ya mapenzi huku Jacob akiwa anasisitiza kutaka kujua sababu ya mrembo huyu, aliyejitambulisha kama Regina kusema kuwa haiwezekani yeye kuolewa.
“Kweli haitawezekana, hata kitendo cha mimi kukumbatiana na wewe kiasi hiki ni ujasiri tu nilio nao, haikutakiwa mimi nikukumbatie kiasi hiki, nimeshindwa kujizuia Jacob nimeshindwa..........umenivutia, nimekupenda Jacob. Naomba niondoke maana najua kuwa muda wangu wa kukaa hapa umeisha na nahitajika mahali” Regina alisema huku akitaka kujitoa kifuani kwa Jacob, ambaye mpaka hapo alikuwa na hamu ya kujua ni kitu gani kimemsibu binti mrembo kama huyo.
“Hapana Regina kabla haujaondoka naomba unijulishe tatizo lako, kwani siamini kuwa swali langu ndilo lilosababisha wewe utokwe na machozi mengi kiasi hiki, niko tayari kukusaidia kwa namna yoyote ile kama nitakayoweza” Jacob alisema huku akizidi kumvuta Regina ili atulie zaidi katika kifua chake.
“Jacob, nakuonea huruma sana kwani hata hapa tu najua maisha yako yatakuwa mashakani” Alisema Regina huku akiinua Kichwa chake na kuangaza hapa na pale ukumbini hapo.
“Hatarini kivipi Regina? Mbona sikuelewi?”
“Kuna watu Jacob, watu wasiotaka niolewe kwa faida yao. Kama ni kuolewa basi inamaanisha kifo chang………” Kabla Regina hajamalizia, Jacob alishitukia anapigwa na kitu kizito kisogoni na papo hapo akajikuta anapoteza uwezo wa kupambanua mambo, hata mashairi ya wimbo wa ‘safari sio kifo’ wa Akudo Impact akawa anasikia yakipotelea hewani, akapoteza fahamu na hivyo kutojua ni nini kilikuwa kinaendelea.
Mtunzi: Japhet Nyang’oro
Phone: 0762204166
“Jacob, napenda kuolewa ila haiwezekani” Alisema ilhali mikono yake ikiwa bado inaminya minya misuli ya mwanaume huyu huku pia machozi yakiwa yanamtiririka.
“Kwa nini ishindikane Regina? Wewe ni msichana ambaye unaweza kumvutia kila mwanaume mwenye mpango wa kupata mwenza wa maisha?” Jacob aliuliza huku akihisi ubaridi uliokuwa ukipenya taratibu katika kifua chake kutokana na machozi yaliyokuwa yakitoka kwa wingi machoni kwa Regina.
“Hapana haiwezekani Jacob…” Regina alisisistiza kwa sauti ya chini, iliyokuwa na chembe chembe za huba na wasiwasi kwa wakati mmoja.
“Usiseme hivyo Regina!”
“Hata nisiposema, huo ndio ukweli na hali halisi Jacob”
“Naomba sababu ya huko kutowezekana…” Jacob alizidi kuhoji kwa shahuku.
“Hata nikikuambia huwezi badili hali na ukweli wa mambo”
“Umejuaje kama sitoweza?”
“Uko peke yako, wako jeshi, huwezi washinda wote....ni waovu sana!”
“Nakupenda Regina, niko tayari kufanya lolote ili kurejesha uhuru wako na Amani” maneno hayo ya Jacob ilikuwa kama sauti ya muziki mororo inayopenya kwenye kiza kinene na kuyafikia masikio ya mtu aliyesimama chini ya mti mukubwa baada ya kunyeshewa na na mvua nzito.
“Sijawahi kuwa huru na sijui amani ikoje Jacob” alisema Regina huku akimkazia macho Jacob, kamasi nyembamba na machozi vikiendelea kuchuruzika.
Wakati mahojiano hayo yakiendelea, sauti yake Bella wa Akudo Impact ilikuwa ikivuma ukumbini hapo huku yale mashairi ya wimbo wake ‘yako wapi mapenzi? ilimfanya kila aliyekuwepo kujishughulisha zaidi na mwandani aliyekuwa nae. Kwa kifupi hali ilikuwa ni ya kuvutia na utulivu katika ukumbi wa Miami Hoteli ambayo ni moja kati ya hoteli za kuvutia zilizoko kando kidogo ya jiji la Dar es salaam baada ya kupita mbezi beach.
Ni kawaida kwa Jacob Matata kutoka nyakati za jioni na kwenda katika mojawapo ya maeneo ya burudani katika jiji la Dar es salaam. Ukimuuliza mwenyewe kwa nini alipenda kwenda maeneo hayo, sababu nyingi angekupa. Lakini katika orodha yake asingesita kutaja, upweke, burudani na kusafisha macho. Lakini ana jingine ambalo kamwe usingelisikia akilitaja...........kazi....kazi yake ya upelelezi ilimtaka kuwa jirani na jamii, jamii iliyoko kwenye madaraja yote, daraja la juu, daraja la kati na daraja la chini.
Siku hiyo Jacob Matata alijikuta anavutiwa kwenda Miami hoteli. Alisikia Akudo Impact wanapiga huko, na kwa vile yeye ni mpenzi wa muziki wao akaona ni bora akaishibishe nafsi yake kitu inataka. Binafsi anamiliki magari mawili, lakini hakuwa anapenda kwenda sehemu za starehe akiwa anaendesha, hivyo alimtaarifu Abdul mmoja wa vijana wake ambao hupenda kuwakodisha akiwa kwenye mizunguko yake na wakati akiwa hataki kuendesha. Abdul alimpitia Jacob nyumbani kwake maeneo ya Sinza Mori mida ya saa tatu unusu usiku.
“vipi bosi, naona leo umekaa kiburudani Zaidi?” Abdul alimuambia Jacob ambaye alikuwa amevaa fulana ya blue na suluali ya jeans nyeusi.
“Si unajua wazee wa masauti Akudo wako Miami Hotel, sasa nataka nikakate kiu huko” Jacob alisema.
“Ahhh wale jamaa hata mie nawakubali sana” Abdul alijibu.
Saa nne na robo ilimkuta Jacob ameshatulia kitini katika ukumbi wa hoteli ya Miami. Akudo walikuwa wameshaanza kushambulia jukwaa taratibu. Alitafuta sehemu na kukaa, kabla ya kuagiza aletewe vinywaji. Vinywaji vililetwa na taratibu akaanza kujipigilia huku akiyapa fursa macho yake yaweze kutalii katika ukumbi mpana wa hoteli hiyo...kusafisha macho. Jacob aliamua aweke mbili-tatu ili wakati mambo yakichanganya nae awe kamili.
Tangu alipoingia hotelini hapo, Jacob Matata alionekana kuwa mtulivu, japo utulivu ni hali ya kujifunza tu kwake, asili yake ni mtu mchangamfu sana na mtundu unaweza sema. Hata ukienda mitaa aliyokulia pale Mwanza mjini maeneo ya Kirumba mwaloni, ambapo nyumba ambayo wazazi wake walikuwa wamepanga ilikuwa jirani na msikiti wa Taqwa, siku hizi kuna shule ya sekondari ya kiislamu pale, ukiuliza utaambiwa wakati Jacob anakuwa miaka ile ya 1991, wazazi walikuwa wakiwazuia watoto wao wasicheze pamoja nae. Alikuwa mtundu balaa.
Kadri masaa yalivyokuwa yakizidi kukatika, ndivyo ukumbi huo ulivyokuwa ukipungua watu. Pamoja na kuwa kulikuwa na watu wengi wa umri na maumbile tofauti, lakini macho ya Jacob Matata yaligota kwa msichana mmoja aliyekuwa ametulia tuli juu ya kiti upande wa kulia wa ukumbi huo. Alipozidi kumtazama, Jacob aliweza kubaini uzuri wa msichana huyo. Hivyo mara kwa mara macho yake yakawa yanapendelea kuangalia upande alipokuwa amekaa kiumbe huyo wa kike. Dakika kumi baadae Jacob alitupia macho kwa yule msichana mrembo na kubaini kuwa hakuwepo sehemu ile aliyokuwa amekaa.
Wakati anageuza macho katika jitihada za kujaribu kuangaza ili aweze kuona kama bado msichana huyo alikuwepo ukumbini hapo, ndipo macho yake yalipogongana moja kwa moja na yale ya msichana mrembo akiwa amekaa hatua chache tu kwa nyuma yake. Macho yao yalipogongana, yule msichana aliachia tabasamu la kukaribisha. Kuona hivyo, Jacob aliachia lake la mwitikio kisha akasita kidogo. Aliangalia saa yake ya mkononi na kubaini kuwa tayari ilikuwa inaelekea kuwa saa tano na robo usiku. Jacob alisimama, kabla ya kupiga hatua yoyote alizungusha macho yake huku na huko ili kuona kama kulikuwa na lolote, alipooona hakuna aligeuka na kuanza kuelekea alipokuwa amekaa yule mrembo.
Haikuwachukua muda mrefu wakajikuta wameshatambulishana. Muda si muda wakakubaliana kumalizia muda uliobaki kwa kucheza muziki pamoja. Na wakati huo huo ule wimbo maarufu wa ‘yako wapi mapenzi? ulikuwa ukiimbwa kwa ustadi mkubwa nae Bella. Haikuwa siri kuwa kila mmoja katika watu hawa alikuwa amevutiwa na mwenzie.
Sijui kama ndio ilikuwa kosa au la, pale Jacob alipomuuliza msichana huyu kama alikuwa na mtu yeyote. Jibu alilolipata lilikuwa ni lile ambalo Jacob alikuwa anaombea apewe. Kule kusikia kuwa Regina hakuwa na mtu kulimfurahisha sana Jacob. Hapo ndipo akauliza swali la kichokozi na ambalo hata hivyo ndilo liloleta kizaa zaa kinachoendelea.
Wakati huu walikuwa bado wamekumbatiana katika hali ya mapenzi huku Jacob akiwa anasisitiza kutaka kujua sababu ya mrembo huyu, aliyejitambulisha kama Regina kusema kuwa haiwezekani yeye kuolewa.
“Kweli haitawezekana, hata kitendo cha mimi kukumbatiana na wewe kiasi hiki ni ujasiri tu nilio nao, haikutakiwa mimi nikukumbatie kiasi hiki, nimeshindwa kujizuia Jacob nimeshindwa..........umenivutia, nimekupenda Jacob. Naomba niondoke maana najua kuwa muda wangu wa kukaa hapa umeisha na nahitajika mahali” Regina alisema huku akitaka kujitoa kifuani kwa Jacob, ambaye mpaka hapo alikuwa na hamu ya kujua ni kitu gani kimemsibu binti mrembo kama huyo.
“Hapana Regina kabla haujaondoka naomba unijulishe tatizo lako, kwani siamini kuwa swali langu ndilo lilosababisha wewe utokwe na machozi mengi kiasi hiki, niko tayari kukusaidia kwa namna yoyote ile kama nitakayoweza” Jacob alisema huku akizidi kumvuta Regina ili atulie zaidi katika kifua chake.
“Jacob, nakuonea huruma sana kwani hata hapa tu najua maisha yako yatakuwa mashakani” Alisema Regina huku akiinua Kichwa chake na kuangaza hapa na pale ukumbini hapo.
“Hatarini kivipi Regina? Mbona sikuelewi?”
“Kuna watu Jacob, watu wasiotaka niolewe kwa faida yao. Kama ni kuolewa basi inamaanisha kifo chang………” Kabla Regina hajamalizia, Jacob alishitukia anapigwa na kitu kizito kisogoni na papo hapo akajikuta anapoteza uwezo wa kupambanua mambo, hata mashairi ya wimbo wa ‘safari sio kifo’ wa Akudo Impact akawa anasikia yakipotelea hewani, akapoteza fahamu na hivyo kutojua ni nini kilikuwa kinaendelea.