Riwaya: Hatia (Mipango nyuma ya kisogo changu)

Muandishi:- Joseph .D. Migini

Call/txt:- +255766604683

Josephdeo70@gmail.com

#10

"mbona sikuelewi kiongozi". Nikaongea huku nikioneshwa kushangazwa na kile alichokuwa akikisema.

"utaelewa tu sababu ni wengi wanaokuja hapa wanakuwa kama wewe mwanzoni ila mwishoni akili inawakaa sawa sawa na kutueleza". Akaingiza tena mkono wake kwenye mfuko ule na kutoa kitu ambacho ilikuwa mara yangu ya kwanza kukiona.

"hii ndio imefanya sisi kufika kwako ni GPRS ambayo ilikuwa kwenye mwili wa mama. Na bahati nzuri ni kuwa ulipoitoa ukaisahau kwako na wewe kukimbilia huko unapopaita Maisome sio!!?. Mshangao wa dhahiri ukanivaa huku mwili sasa ukipoteza uhimili wa ujasiri.

"nadhani walinao niframe hii kesi wamejipanga sana na bahati iliyo mbaya hata nyinyi mmeingia kwenye mtego huo". Nikamwambia bwana yule aliyeendelea kunionesha tabasamu pana kwenye sura yake.

"vizuri kama unaweza kutufundisha kile tulichokuwa na taaluma nacho, na hiyo ni kwa sababu wewe ni bora kutuliko. Kama uliweza kumchukua na kumficha tusipoweza kumuona basi uko vizuri kushindana na idara". Kauli yake ikanifanya kuwa nifahamu watu wanao nishikilia nao ni idara ya usalama wa taifa.

Japo sikuwa na uhakika wa moja kwa moja. Ila idara ya usalama wa taifa ndio ilikuwa ikihusishwa na kuwashikiria watu kwa stahili ambayo mimi nimeshikiriwa.

INAENDELEA….

Unakaribishwa kwa maoni na ushauri.



GPRS
 
Muandishi:- Joseph .D. Migini

Call/txt:- +255766604683

Josephdeo70@gmail.com

#10

"mbona sikuelewi kiongozi". Nikaongea huku nikioneshwa kushangazwa na kile alichokuwa akikisema.

"utaelewa tu sababu ni wengi wanaokuja hapa wanakuwa kama wewe mwanzoni ila mwishoni akili inawakaa sawa sawa na kutueleza". Akaingiza tena mkono wake kwenye mfuko ule na kutoa kitu ambacho ilikuwa mara yangu ya kwanza kukiona.

"hii ndio imefanya sisi kufika kwako ni GPRS ambayo ilikuwa kwenye mwili wa mama. Na bahati nzuri ni kuwa ulipoitoa ukaisahau kwako na wewe kukimbilia huko unapopaita Maisome sio!!?. Mshangao wa dhahiri ukanivaa huku mwili sasa ukipoteza uhimili wa ujasiri.

"nadhani walinao niframe hii kesi wamejipanga sana na bahati iliyo mbaya hata nyinyi mmeingia kwenye mtego huo". Nikamwambia bwana yule aliyeendelea kunionesha tabasamu pana kwenye sura yake.

"vizuri kama unaweza kutufundisha kile tulichokuwa na taaluma nacho, na hiyo ni kwa sababu wewe ni bora kutuliko. Kama uliweza kumchukua na kumficha tusipoweza kumuona basi uko vizuri kushindana na idara". Kauli yake ikanifanya kuwa nifahamu watu wanao nishikilia nao ni idara ya usalama wa taifa.

Japo sikuwa na uhakika wa moja kwa moja. Ila idara ya usalama wa taifa ndio ilikuwa ikihusishwa na kuwashikiria watu kwa stahili ambayo mimi nimeshikiriwa.

INAENDELEA….

Unakaribishwa kwa maoni na ushauri.

Mkuu Hongera kwa utunzi wa Hii burudani ya macho na akili. Unapoendelea ungeunga kidogo huu mtiririko kwa at least uwe wa episode moja moja inayokamilisha simulizi ndogo ndani ya simulizi kubwa.
 
Mkuu Hongera kwa utunzi wa Hii burudani ya macho na akili. Unapoendelea ungeunga kidogo huu mtiririko kwa at least uwe wa episode moja moja inayokamilisha simulizi ndogo ndani ya simulizi kubwa.
Asante kwa ushauri nitalifanyia kazi hilo
 
Muandishi:- Joseph .D. Migini

Call/txt:- +255766604683

Josephdeo70@gmail.com

#11

"ningependa kuwa kama ulivyosema lakini trust me bro sijafanya, na siwezi kufanya chochote kile kibaya".

"sawa, vipi kuhusu hii". Alitoa picha ambayo ilinionesha niko nazungumza na watu fulani ambao hawakuwa wanaonekana kwani picha ile iliwapiga wakiwa wamempa mgongo mpigaji.

"inahusiana na nini hii?". Nikamuuliza kwani nilikuwa nakumbuka kuwa watu wale ndio walinipa taarifa ambazo ndio zilinifanya nami nikaingia kwenye kilimo.

Siku ambayo picha hii ilipigwa ilikuwa siku ya kawaida tu ambapo nilitoka nyumbani na kwenda shule ya msingi kitangiri mahali ambapo ndipo kibarua changu kilikuwa. Nilifika shuleni hapo na kuingia kwenye kipindi cha hesabu darasa la nne. Nilipotoka kwenye kipindi nikaenda kupata kifungua kinywa kwenye ofisi ya waalimu. Baada ya hapo ndipo walipokuja watu wale ambao sikuwa nawafahamu ila nilivutiwa na namna walivyokuwa wakizungumza kuhusu fursa za kilimo.

Watu wale walijitambulisha kama SHAMBA HURIA COMPANY walijinasibu kuwa ni wanunuzi wa mazao kwa bei shindani. Watu wale walitoa miongozo mingi katika kilimo huku wakiwa na ushahidi kadhaa za watu waliofanikiwa kwenye kilimo na wale walioshindwa.

Huku wakitupa sababu nyingi za kwanini kama waajiliwa tuwekeze kwenye kilimo kwani mnunuzi wa mazao ambayo tutalima wapo na wananunua kwa bei shindani sokoni.

Ili likanivutia zaidi na hapo ndipo nikaomba kuongea na watu wale pembeni na huo ndio wakati ambao picha ile ilipigwa.

Kwani nilikuwa na watu wanne kutoka kwenye kampuni hiyo na tulisogea pembeni kabisa na jengo la shule na mazingira ya kwenye picha hiyo yalionesha vile. Sasa ikiwa tulikuwa tukiongea habari za kilimo kwanini picha ile ije kutumika kwenye tuhuma za kupotea kwa mke wa waziri mkuu?.

INAENDELEA….

Unakaribishwa kwa maoni na ushauri.
 
Unaweza kupata muendelezo wa riwaya hii bure kabisa kupitia group hili

Binafsi ni muandishi wa RIWAYA Pengine sio mzuri kuliko muandishi unayemfahamu.

Ila yapo mazuri mengi...ili kudhibitisha hilo jiunge na Group hili la WhatsApp bure kabisa.. Falsafa70
 
Muandishi:- Joseph .D. Migini

Call/txt:- +255766604683

Josephdeo70@gmail.com

#12

Hili swali likanifanya nirudishe mawazo yangu pale ambapo nikakumbuka kuwa kulikuwa na picha mikononi mwangu ambapo niliulizwa swali. "hawa ni jamaa ambao walinishawishi kuingia kwenye kilimo kwa sera zao. Nashangaa kuona picha hii leo wakati tukio hilo lina zaidi ya miezi sita sasa!".

Bwana yule akatabasamu kidogo kisha akatoa picha nyingine ambayo iliwaonesha watu wale wale. Wakiwa sehemu nyingine ambayo ilikuwa ni kama yenye usiri na picha ile ilionesha kuwa watu wale walikuwa wakijadiliana jambo. Kisha akatoa picha nyingine tena ikiwaonesha watu wengine kabisa lakini kati ya hao wawili walikuwa ni wale ambao nimekwisha kuwaona ila bado sikuelewa kwanini nioneshwe zile picha na zina uhusiano gani na hatia zangu.

"hawa wawili wamekutwa wamekufa na wengine hawaonekani kabisa. Sababu ya kukuonesha haya ni kuwa hawa walihusika na kupotea kwa mke wa waziri na bintiye. Pengine ndio maboss wako hivyo unaweza kutuambia kuwahusu!". Akauliza kisha akajiweka sawa kunisikia.

"hawa walikuja kutuelezea habari za kilimo nami nikavutiwa sana na habari hizo. Kisha nikawasogeza pembeni ili wanipe habari zaidi kuhusu hayo waliyokuwa wakiyahubiri. Ndio hii picha ikapigwa na sielewa kwanini ilipigwa na baadae tukaachana mpaka leo unaponiambia haya sijui walipo zaidi ya anuani ya kampuni yao inapopatikana". Nikanyamaza kuonesha kuwa sikuwa na kingine cha kuongolea.

"kampuni gani?". Akaniuliza.

"walisema inaitwa SHAMBA HURIA COMPANY LIMITED. Na anuni zao ni S.L.P 1250". Nilipomjibu bwana yule akazama kwenye simu yake na kubonyeza kwa mda kisha akanitazama na kunionesha kitu kwenye simu yake.

Ni bure sasa kusoma hiii riwaya na nyingine nyingi unachopaswa kufanya ni kujiunga na group hili la WhatsApp up

 
Bado ujachelewa kuwa moja kati ya watu ambao Ni wanufaika wa riwaya za bure kutoka hapa.... Cha kufanya ni kubofya link hii

 
Riwaya:- HATIA
(Mipango nyuma ya kisogo changu)
Muandishi:- Joseph .D. Migini
Call/txt:- +255655500516
Josephdeo70@gmail.com

#13

Macho yangu yalikuwa yanaona vyema japo maandishi yalikuwa kwa lugha ya kiingereza. Ila niliweza kuyaelewa vizuri mno kwani yalielezea kuwa kampuni ile ilifunga huduma zake nchini zaidi ya miaka mitano nyuma. Huku sababu ya kufungwa kwa huduma hizo ni kutaka kulijua zaidi soko la hapa nchini kwani walianzisha biashara pasipo kuwa na uelewa wa soko.

Taarifa hii ilinifanya kushangaa kwani watu wale walikuja na vitambulisho kutoka kwenye kampuni hiyo hiyo. Na haikuishia kwenye vitambulisho mpaka wakatuonesha wavuti wao ambao ulikuwa umepakiwa taarifa kadha wa kadha juu ya manunuzi ya mazao.

Sasa taarifa ya kuwa kampuni hiyo ilifungwa kwa zaidi ya miaka mitano nyuma ilifanya akili yangu kushikwa na ukakasi. Huku ikijilaumu mara kadhaa kwa kushindwa kufuatilia ukweli wa taarifa zile walizokuwa wakinipa mabwana wale. Nilikuwa nimezama kwenye tafakuri juu ya hilo na sauti ya bwana yule ikanishitua kwa kuniambia.

"basi unaweza kuwa na wakati mgumu kutokea sasa!. Kwani hatuna mda wa kutosha". Alipoongea hivyo akanyanyuka na haikuchukua mda wanaume wale aliokuwa nao wakaninyanyua.

Bado nilikuwa na pingu mikononi wakanitoa kwenye chumba kile. Tukashika korodo ndefu ambayo ilikuwa na milango kadhaa. Tukakata kona na kukukutana na korido nyingine hii ilikuwa ndogo tofauti na ile tuliyotoka. Kisha mlango ukafunguliwa na hapo nikapokelewa na harufu kali ambayo ilizipa pua zangu wakati mgumu kuelewa ni harufu ya nini kwani ilikuwa mbaya.


NB: Unakaribishwa kwa maoni na ushauri. Pia vyema kama ukitusaidia kuwafikia wengine kwa kusambaza link ya group letu. Ambalo ni bure kabisa kujiunga..
 
Inapendeza kuona familia hii ya wapenzi wa riwaya inakua kila iitwapo leo nawe ujachelewa kujiunga nayo...

Gharama ni wewe pamoja na app yako ya WhatsApp tu hakuna kingine. Bofya hii link

Pic_1659680804512.jpg
 
Ndani ya group mambo yapo mbio mno kuliko haya maelezo natayari tuko na riwaya mpya.

Tembelea group hili kwa gharama ya bure kabisa karibu

Screenshot_20220806-212122.jpg
 
Riwaya:- HATIA

(Mipango nyuma ya kisogo changu)

Muandishi:- Joseph .D. Migini

Call/txt:- +255655500516

Josephdeo70@gmail.com

#14

Tulipopiga hatua zaidi kuingia ndani ndipo nikaelewa kuwa harufu ile ilikuwa ya damu pamoja na nyama za binadamu. Chumba hicho kilikuwa ni chumba cha mateso nami sikuelewa ni kwanini walinileta pale. Ila kama ilivyo kawaida yangu nikajipa utulivu mahali ambapo mwili uligoma kuupokea.

Mwili ukaanza kutetemeka kuelezea hisia zake za woga. Nikasimamishwa huku mikono yangu ikifungwa kwa juu na minyororo. Woga ulikuwa mkubwa na uliojionesha dhahiri usoni mwangu huku mabwana wale wakionesha kuwa hawakuwa na huruma hata kidogo dhidi yangu. Walipomaliza hivyo wakatoka nje na kuuacha mlango ule ukiwa wazi.

Akaingia bwana mwingine mwenye sura mbaya kuitazama huku ndevu zikiwa zimejaa kwenye kidevu chake. Mdomoni mwake kulikuwa na sigara akawa anatoa moshi nje na alinisogelea karibu zaidi huku akinipulizia moshi wa sigara aliyokuwa akivuta. Huku akinitizama kwa macho yenye uroho sana.

Sikuwa mtumiaji hivyo hali hiyo ikawa kero kwangu lakini sikuweza kuongea. Alipomaliza sigara yake akatupa kishungu chini na kisha akachana fulana yangu na baada ya hapo akaondoa na suruali yangu. Sikuwa naelewa bwana yule anataka kufanya nini kwangu. Ila niliomba Mungu isiwe kitendo ambacho kilikuwa kwenye mawazo yangu kwani sikuwa na uwezo wa kukihimili.

Nikiwa kwenye lindi la mawazo hayo ghafla nikashitushwa na ngumi nzito upande wa mbavu zangu za kushoto. Maumivu yakafanya nikatoa ukelele kwani sikuwa naweza kuhimili uzito wa ngumi aliyorusha bwana yule. Lakini ukelele wangu ni kama uliwasha taa ya kijana kwa bwana yule ambaye aliendelea kurusha ngumi bila kukoma. Mpaka hapo ngozi yangu nyeupe iligeuka kuwa nyekundu na kuvia kwa damu. Nililia sana lakini ni kama bwana yule hakuwa hanajali.


NB: Unakaribishwa kwa maoni na ushauri. Pia vyema kama ukitusaidia kuwafikia wengine kwa kusambaza link ya group letu. Ambalo ni bure kabisa kujiunga..

 
Riwaya:- HATIA

(Mipango nyuma ya kisogo changu)

Muandishi:- Joseph .D. Migini

Call/txt:- +255655500516

Josephdeo70@gmail.com



#15

Alitulia baada ya kusababisha maumivu makali kwenye mwili wangu ambayo sikuwahi kuyahisi toka nazaliwa. Akawasha tena sigara huku mimi nikiwa siwezi hata kuinua shingo yangu kutazama mbele. Akavuta tena pafu kadhaa kutoka kwenye sigara ile na kuizima kisha akanifungua ambapo niliporomoka kama ambavyo ghorofa lililovunjwa linapoanguka. Akanidaka kabla sijafika chini kisha akanikalisha kwenye kiti na kunifunga kwa minyororo ambayo ilikizunguka kiti kile.

Sikuwa na uwezo hata wa kutikisa mkono wangu hivyo nikatulia akaingia yule bwana aliyekuwa akinihoji. Akashika kichwa changu na kufanya kama anakipeleka juu hii ikafanya niweze kumuangalia.

Nilipo muangalia tu akatabasamu nami nikamuuliza.

"kwanini unanifanyia hivi?". Hasira ilikuwa imetawala kwenye kifua changu kwani sikuhisi kuwa nastahili hayo ambayo watu wale wananifanyia.

"Sosi nadhani haitakiwi kufika huko tunapoelekea ila unatulazimisha na kutusukuma kufika. Hapo ni mwanzo tunakoelekea ni patamu zaidi". Sura yake ilikuwa imebadilika toka kwenye tabasam mpaka kuweka mikunjo ya hasira.

"sijui chochote….siju...i.i.i". Machozi yalimwagika kutokana na hasira pamoja na uchungu niliokuwa nao.

Bwana yule akaenda mpaka ilipokuwa kona ya chumba kile kisha kuchukua rungu. Akavua koti lake la suti na kukunja mikono ya shati lake kisha kusogea nilipo na rungu lile. Licha ya kusisitiza kuwa sikuwa najua lolote bwana yule alipiga magoti yangu uchungu wake nilihisi mifupa ya magoti yangu ikisagika. Nililia mpaka sauti ikakatika kisha machozi pekee ndio yakabaki yanatoka. Rungu zisizokuwa na idadi zikafanya mpaka nijihisi ganzi kwenye miguu na kutohisi tena kama nina miguu. Sikuwa naweza hata kujitetea kwani nilifungwa vilivyo na minyororo hiyo.

NB: Unakaribishwa kwa maoni na ushauri. Pia vyema kama ukitusaidia kuwafikia wengine kwa kusambaza link ya group letu. Ambalo ni bure kabisa kujiunga..

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom