Ripoti za Kalenga zagongana

Ripoti za Kalenga zagongana

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Katika hali ya sintofahamu,Ripoti mbili zilizotua Makao Makuu ya CCM-Dodoma kutoka Jimbo la Uchaguzi la Kalenga zinakinzana. Taarifa za kiitelijensia kutoka Makao Makuu zinaonesha kuwa kuna Ripoti toka kwa Timu ya Kampeni Jimboni humo na ile ya Timu ya Watafiti wa Kisiasa iliyotumwa Kalenga. Ripoti husika zinakinzana kwa kiasi kikubwa.

Wakati Ripoti ya Timu ya Kampeni ikidai kuwa CCM inakubalika na ushindi unanukia,Ripoti ya Washambuzi inaonesha kuwa hali si ya kuridhisha na hivyo chama kinaombwa kuongeza nguvu Kalenga. Baada ya Ripoti hizo za awali kutua chamani, hali ya taharuki imetanda katika Ofisi za chama hapa Dodoma.


Ili kuujua ukweli,chama kinapanga kutuma Timu Huru kurudi na hali halisi ya huko. Nitawajuza kitakachojiri


Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
 
hapo mashambulizi yataongeza polisi na vijana wakuprovoke fujo na kuandaa vituo hewa mzee tupa tupa tahadhali uliyoileta itawafanya waandae mbinu ya kuwamaliza baadhi ya watu unawajua tena viongozi wako
 
Wataiba kura watatawala kwa muda lkn mwishowao upo njiani unakuja.nani alijua moi atapigwa mweleka na chama chake KANU.yuko wapi mzee wanyayoo moi nanialikua anakohoa ktk utawala wake
Baadaye wakenya walimchoka na kumbwanga chini na KANU yake
 
Wataiba kura watatawala kwa muda lkn mwishowao upo njiani unakuja.nani alijua moi atapigwa mweleka na chama chake KANU.yuko wapi mzee wanyayoo moi nanialikua anakohoa ktk utawala wake
Baadaye wakenya walimchoka na kumbwanga chini na KANU yake
 
Katiba hoi na kalenga pia, hatoki mtu hapa.
 
Katika hali ya sintofahamu,Ripoti mbili zilizotua Makao Makuu ya CCM-Dodoma kutoka Jimbo la Uchaguzi la Kalenga zinakinzana. Taarifa za kiitelijensia kutoka Makao Makuu zinaonesha kuwa kuna Ripoti toka kwa Timu ya Kampeni Jimboni humo na ile ya Timu ya Watafiti wa Kisiasa iliyotumwa Kalenga. Ripoti husika zinakinzana kwa kiasi kikubwa.

Wakati Ripoti ya Timu ya Kampeni ikidai kuwa CCM inakubalika na ushindi unanukia,Ripoti ya Washambuzi inaonesha kuwa hali si ya kuridhisha na hivyo chama kinaombwa kuongeza nguvu Kalenga. Baada ya Ripoti hizo za awali kutua chamani, hali ya taharuki imetanda katika Ofisi za chama hapa Dodoma.


Ili kuujua ukweli,chama kinapanga kutuma Timu Huru kurudi na hali halisi ya huko. Nitawajuza kitakachojiri


Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
Chama Chakavu kwakweli kina hali mbaya na kinajitahidi kufa kiofisa.
 
Mipango yao kupeleka waliomwagiwa tindikali kuinadi ccm. Hawa jamaa ovyo, siasa wanazigeuza kuwa ughaidi.

Upo sahihi kwani wote tumeona Mwigulu badala ya kunadi sera za chama amewaleta watu kutuka Kahama na Igunda kujakutafuta huruma ya wanaKalenga. Naomba sana watu wakalenga wasidanganyike. Nani asiyejua hujuma za CCM kwenye uchaguzi? Tafakali chukua hatua
 
Ccm wameichoka watu inawakumbuka wakati wa uchaguzi tu ona afya hadi huko muhimbili madoctor wamekata tamaa huduma ya kubahatisha kije chama kingine kiwape matumaini watanzania kilete barabara,maji,usafiri wa umma,shule na vitabu,dawa hospitali,wote tutibiwe nchini,watoto shule za msingi wapewe uji wote,kwa kutumia rasilimali zetu siyo kuacha maccm wakisadirisha maliasili zetu
 
Mtasema sana humu ktk mitandao ila siye tunawasubiri ktk pitch tunakukamueni hadi mkome. Tatizo lenu mna midomo mirefu kama Chukulubu bin Chakubanga wa Polo baba wa Chupaki lakini siku nyingi mnajua dawa yenu ishakwiva mmeinywa ktk chaguzi za madiwani sasa mjiandae mtainywa Kalenga na mtainywa pia Chalinze lakini msiogope sana walau kidogo imepoa mtainywa japo Uchungu umezidi lakini imepoa kipindi kile cha chopa 3 kata 3 ilikua i moto sana hadi Mbowe alipoionja aliungua maskini. Tutaendelea kuwanyoosha hadi mkome.
 
Mtasema sana humu ktk mitandao ila siye tunawasubiri ktk pitch tunakukamueni hadi mkome. Tatizo lenu mna midomo mirefu kama Chukulubu bin Chakubanga wa Polo baba wa Chupaki lakini siku nyingi mnajua dawa yenu ishakwiva mmeinywa ktk chaguzi za madiwani sasa mjiandae mtainywa Kalenga na mtainywa pia Chalinze lakini msiogope sana walau kidogo imepoa mtainywa japo Uchungu umezidi lakini imepoa kipindi kile cha chopa 3 kata 3 ilikua i moto sana hadi Mbowe alipoionja aliungua maskini. Tutaendelea kuwanyoosha hadi mkome.

Dada,hujielewi ni kukusamehe bure. Wengi wenu mmekaririshwa tu kuwa CDM ilishindwa uchaguzi wa madiwani,mkiulizwa kivipi hamjui kitu. Hovyo kabisa,andika mambo yako kwa ushahidi. CDM ndiyo inapamba moto hakuna ilichopoteza,go back to school maana pengine utafunguka.
 
lakini huyu mtoa hoja hapa si watammaliza kama kweli yupo viunga vya CCM!!! Hizi si taarifa za kutoa hapa akisikia Nape utasakwa hadi majogoo.
 
Back
Top Bottom