Ripoti ya Mh. Rais juu ya economic impact- Itafumbua mengi

Akili Unazo!

JF-Expert Member
Feb 18, 2009
3,930
4,912
Wakuu,

Ni Juzi tu kama siyo Jana toka Ripoti ya kamati ya awali kuwekwa hadharani kuna watu wanatoa michango mingi, wengine ukiwaangalia wanajaribu kupotosha umma kuwa Rais amevunja sheria na mikataba ya uwekezaji juu ya hii sekta ya madini.

Na kuwa siku hawa wawekezaji watakapo kwenda kuproscuute huko kwenye Mahakama za Kimataifa basi watakaoathirika na gharama husika ni sisi wenyewe Wananchi. Hilo halipingiki, ila tujiulizi, huu uoga wetu unatokana na nini? Ni kweli kuingia mikataba mibaya haiwezi kuwa challenged? Hata kama waliopita walifumbia macho, kwa hiyo hakuna wakuja kuyafumbua na kuyaweka wazi ili hata waliokuwa waoga siku za nyuma wajue tulikuwa tunaibiwa?

Ripoti ya kamati ya pili ya Mh. Rais, itapelekea hata hizo Mahakama za Kimataifa za uwekezaji kupotea, kwa kuwa madhara ya kiuchumi ambayo nchi yetu imepitia kwa kuibeba na kuiogoba hii mikataba itauonyesha umma kuwa ukoloni bado upo.

Tuendelee kuvuta subira japo wabishi hawakosekani lakini huo ndio ukweli, miaka 15 Tumeibiwa sana na hawa wawekezaji hawatakuwa na nguvu tena ya kutushinda.
 
Kuna mbunge majuzi alikuwa busy kuutetea mfumo wa protectionism bila kujua kuwa Tanzania kama mwanachama wa WTO (na zamani GATT) tuliridhia kutotekeleza huo mfumo.
 
Ni muhimu kushirikishwa kwa wanasheria bila kujari tofauti za kivyama akitaka kudili kisiasa zaidi halipingiki tutaingia kulipa mihera ilihali mtaani hali mbaya
 
Dowans mkataba ulikuwa wa hovyo tukauvunja matokea tukawalipa maradufu
Serikali isione haya kumuuliza Lowassa alipitia njia gani kuvunja wa City Water
 
Dowans mkataba ulikuwa wa hovyo tukauvunja matokea tukawalipa maradufu
Serikali isione haya kumuuliza Lowassa alipitia njia gani kuvunja wa City Water
Mkuu umesahau kuwa huyo Mzee ni Gwiji LA siasa za tz na Africa?
 
Hawakosekani lakini Huo ndio Ukweli, Miaka 15 Tumeibiwa sana na hawa wawekezaji


tulipashwa kuwapeleka court na si kuamua vinginevyo kwenye jukwaa la wahariri
 
Dowans mkataba ulikuwa wa hovyo tukauvunja matokea tukawalipa maradufu
Serikali isione haya kumuuliza Lowassa alipitia njia gani kuvunja wa City Water
Yaani hiyo mahakama iliyoketi hapa hapa bongo??
 
Wakuu,

Ni Juzi tu kama siyo Jana toka Ripoti ya kamati ya awali kuwekwa hadharani kuna watu wanatoa michango mingi, wengine ukiwaangalia wanajaribu kupotosha umma kuwa Rais amevunja sheria na mikataba ya uwekezaji juu ya hii sekta ya madini.

Na kuwa siku hawa wawekezaji watakapo kwenda kuproscuute huko kwenye Mahakama za Kimataifa basi watakaoathirika na gharama husika ni sisi wenyewe Wananchi. Hilo halipingiki, ila tujiulizi, huu uoga wetu unatokana na nini? Ni kweli kuingia mikataba mibaya haiwezi kuwa challenged? Hata kama waliopita walifumbia macho, kwa hiyo hakuna wakuja kuyafumbua na kuyaweka wazi ili hata waliokuwa waoga siku za nyuma wajue tulikuwa tunaibiwa?

Ripoti ya kamati ya pili ya Mh. Rais, itapelekea hata hizo Mahakama za Kimataifa za uwekezaji kupotea, kwa kuwa madhara ya kiuchumi ambayo nchi yetu imepitia kwa kuibeba na kuiogoba hii mikataba itauonyesha umma kuwa ukoloni bado upo.

Tuendelee kuvuta subira japo wabishi hawakosekani lakini huo ndio ukweli, miaka 15 Tumeibiwa sana na hawa wawekezaji hawatakuwa na nguvu tena ya kutushinda.
Our country isn't a colonial state any more ...those dogs who wish it, have their choice to leave or to stay.
 
Back
Top Bottom