Ridhiwani Kikwete upo? Tuna mwezi wa tatu sasa hatuna maji Chalinze

TAWA

JF-Expert Member
Jun 23, 2013
3,667
1,566
Wanabodi salamu,

Toka mwaka jana mwezi wa 11 tarehe 23 maji ya bomba katika mji wa chalinze yamekuwa ni hadithi na lulu. Hali imekuwa mbaya sana hasa katika kipindi hiki cha mlipuko wa kipindu pindu kwa baadhi ya maeneo ya nchi yetu.

Cha kushangaza katika hali kama hiyo, mbunge wetu haonekani wala kuzingumza chochote, kitu hiki kinafanya watu waanze kujuta kwa nini walimchgua huyu bwana.

WITO WANGU KWA MH. RIZ:
Watu walikuchagua ili wewe uwe msemaji wao, kama shughuli hiyo imekushinda fanya wende watu wachague watu wengine wa vyma vingine labda watakuwa na msaada kwao.

Tumekuchoka labda tukikwambia hivi utasikia.
 
Du! ni sheeda kweli kweli Mi mwenyewe ni mkazi wa chalinze shida hii naijua vizuri lakini nawalaumu zaidi wazawa, hawako tayari kubadilika wameendekeza ngoma za kigodoro zaidi kuliko suala la maendeleo wachatuendelee kuumia tu!
 
Muacheni mh. mbunge apumzishe akili.
Ni wazi alikuwa na nia njema lakini mzee wa majipu kashezitolea investments macho kwa zaidi ya 90%! Hapa ni kuutegemea zaidi mfuko wa jimbo.
 
Wana bodi salamu, toka mwka jana mwezi wa 11 tarehe 23 maji ya bomba katika mji wa chalinze yamekuwa ni hadithi na lulu. Hali imekuwa mbaya sana hasa katika kipindi hiki cha mlipuko wa kipindu pindu kwa baadhi ya maeneo ya nchi yetu.
Cha kushangaza katika hali kama hiyo, mbunge wetu haonekani wala kuzingumza chochote, kitu hiki kinafanya watu waanze kujuta kwa nini walimchgua huyu bwana.
WITO WANGU KWA MH. RIZ, watu walikuchagua ili wewe uwe msemaji wao, kama shughuli hiyo imekushinda fanya wende watu wachague watu wengine wa vyma vingine labda watakuwa na msaada kwao.
Tumekuchoka labda tukikwambia hivi utasikia.
Kama aliwa nunua mkampa kura mnahitaji nini tena kwake?? Msubirini tena 2020. Endeleeni kuvaa t shits na kanga hadi aje tena
 
Wana bodi salamu, toka mwka jana mwezi wa 11 tarehe 23 maji ya bomba katika mji wa chalinze yamekuwa ni hadithi na lulu. Hali imekuwa mbaya sana hasa katika kipindi hiki cha mlipuko wa kipindu pindu kwa baadhi ya maeneo ya nchi yetu.
Cha kushangaza katika hali kama hiyo, mbunge wetu haonekani wala kuzingumza chochote, kitu hiki kinafanya watu waanze kujuta kwa nini walimchgua huyu bwana.
WITO WANGU KWA MH. RIZ, watu walikuchagua ili wewe uwe msemaji wao, kama shughuli hiyo imekushinda fanya wende watu wachague watu wengine wa vyma vingine labda watakuwa na msaada kwao.
Tumekuchoka labda tukikwambia hivi utasikia.

Chezea Mtikisiko wa Panone, makontena, home shopping centre na flow meters hauwezi kumuacha mtu salama; yupo anatunga sheria za kubypass majipu!
 
Hafadhali umemtaja mbunge wako na mimi namkumbusha Halima Mdee, kawe tuna kero nyingi njoo huku achana na huyo binti wa Bunda kwa kipindi hiki muhimu.
 
HIVI Chalinze Kuna Huduma Ya MAJI SAFI Na Salama!!!!!!!!??? MAANA Uwa Nawaona Wakazi Wa MAENEO Hayo Wakienda Na Mabaiskeli Kuchota Maji Kwa BIN KLEB, Pale AFROIL Petrol Station!!!
 
HIVI Chalinze Kuna Huduma Ya MAJI SAFI Na Salama!!!!!!!!??? MAANA Uwa Nawaona Wakazi Wa MAENEO Hayo Wakienda Na Mabaiskeli Kuchota Maji Kwa BIN KLEB, Pale AFROIL Petrol Station!!!
Yanatuokoa sana haya maji ya Afroil ila sasa ni cha chumvi.
Kwa sasa tunatumia maji ya lambo la matuli, ng'ombe humo humo.
 
Yanatuokoa sana haya maji ya Afroil ila sasa ni cha chumvi.
Kwa sasa tunatumia maji ya lambo la matuli, ng'ombe humo humo.
DUUHH!!! Poleni Saana Mkuu!! SASA Pamoja Na Kuishi Jimbo Moja Na Rais Mstaafu Na Mwanaye Ndiye Mbunge Wenu, Bado Hata Leo Huduma Ya Maji Safi Na Salama Ni BIDHAA ADIMU!!! Walau Kuchimba Visima VIREFU Na VIFUPI, Ili Viweze Kuwasaidia Wapiga Kura Wake, Kama Huyo Mwarabu Ameweza, Inashindikana Vp Kwa Familia Kubwa Kama Hiyo Ya Kikwete!!?? HAYA MAJI Ya MTO Wami Nayo Vp Imekuwa Story Miaka YOTE Tu!!!!!!!!??? ILA Ndio Mjitambue Kuwa, Sio Kila MTU Anaweza Kuwa Kiongozi Tu, Eti Babake, Mamake, Mjombake, Babuye / Bibiye Au Shangaziye Ni Viongozi!!!! MLICHAGUA Kwa Ukabila Tu, Sio Kwa Sifa STAHIKI!! SASA Mtulie Mlipwe!!!!
 
DUUHH!!! Poleni Saana Mkuu!! SASA Pamoja Na Kuishi Jimbo Moja Na Rais Mstaafu Na Mwanaye Ndiye Mbunge Wenu, Bado Hata Leo Huduma Ya Maji Safi Na Salama Ni BIDHAA ADIMU!!! Walau Kuchimba Visima VIREFU Na VIFUPI, Ili Viweze Kuwasaidia Wapiga Kura Wake, Kama Huyo Mwarabu Ameweza, Inashindikana Vp Kwa Familia Kubwa Kama Hiyo Ya Kikwete!!?? HAYA MAJI Ya MTO Wami Nayo Vp Imekuwa Story Miaka YOTE Tu!!!!!!!!??? ILA Ndio Mjitambue Kuwa, Sio Kila MTU Anaweza Kuwa Kiongozi Tu, Eti Babake, Mamake, Mjombake, Babuye / Bibiye Au Shangaziye Ni Viongozi!!!! MLICHAGUA Kwa Ukabila Tu, Sio Kwa Sifa STAHIKI!! SASA Mtulie Mlipwe!!!!
Mi mgeni tu hapa, siasa za hapa ni ngumu sana.
 
Yupo biz anatetea mali za familia.....hawezi kuwakumbuka.....
 
Chezea Mtikisiko wa Panone, makontena, home shopping centre na flow meters hauwezi kumuacha mtu salama; yupo anatunga sheria za kubypass majipu!
Na bado....mtaisoma na kuiandika hiyo namba.
 
Back
Top Bottom