RFA, kipindi hiki kina kasoro

RFA, kipindi hiki kina kasoro

Mantombazane

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2014
Posts
579
Reaction score
367
Jana 18/06/2015 kwenye muda wa saa 3.30 kuelekea saa 4.00 asubuhi kulikuwa na kipindi RFA ambacho sikikumbuki jina lake lakini watangazaji walikuwa wa kike wakipokea wakizungumza na kupokea sms kutoka kwa wasikilizaji na kuzungumza mambo mbali mbali yanayo husu matukio yaliyowatukia watu walipokuwa wanasoma shule za msingi na hasa kuhusiana na walimu mbali mbali jinsi walivyokuwa wanawachapa viboko kwa makosa mbali mbali.

Ambacho sikukipenda ni ile tabia ya kutaja majina ya walimu redioni kuwa eti waliwachapa viboko wengine wakisema viboko vinne, wengine sita na wengine tisa. Cha ajabu na watangazaji nao wakawa wanataja majina ya walimu waliowachapa wakati wakiwa shule za msingi.

Sijui wengine wataonaje lakini mimi naona huo sio ungwana kuanza kuwaanika redioni walimu waliowaadabisha nyakati hizo. Historia kama hizo zinapaswa kuzizungumzwa watu wakikutana au bila kutaja majina ya wahusika hadharani kwani ni kama kutaka kuonesha kuwa walimu fulani walikuwa wakorofi, wakali, waonezi nk wakati wao walikuwa wanatimiza wajibu wao wa kusimamia nidhamu ya wanafunzi kwa mujibu wa sheria na ndio maana baadhi ya wanaowaanika walimu wao redioni wako katika nafasi mbali mbali za kiutendaji. Kama wangewaacha bila kuwaadabisha huenda nao wasingefanikiwa kimaisha kwani wangeharibika.

Mimi nashauri mtindo huo uachwe kwani unakera walimu wenyewe ambao wengine wameshatangulia mbele za haki, wengine kustaafu, wengine bado wako kazini na wengine wako katika nyadhifa mbali mbali.

Hao akina dada walikuwa wanaongoza hicho kipindi kama wanaona raha kuanika redioni majina ya walimu wao waliowaadhibu basi wangeanika na majina ya wavulana waliowavunja bikira kama kwao halitakuwa jambo la kuwefedhehesha.

RFA rekebisheni ujinga huo.
 
Kitaaluma makosa hayo ni makubwa sana. Kwa akili ya mtaani linaweza kuonekana jambo dogo na hata kukosa mchango humu JF.
 
Umesema kweli mkuu naaamini uongozi wa rfa na redio nyingine wanaingia humu cha muhimu wajirekebishe na wasirudie hili kosa.
 
Bila walimu kusimama imala watu wengi walikuwa wamepinda na wasingefika hapo walipo.kuna wakati mwalim alikuwa anapita mabwenini kuhakikisha hakuna mwanafunzi aliyelala wakati wa kujisomea usiku utadhani mwanafunzi akifanikiwa atagawana nae hayo mafanikio. Ni wakati wa kukumbuka jinsi walim wetu walivyojituma kutuchunga kimaadili na kitaaluma mpaka tumefika hapa tulipo.

Hivi uliposhindikana kimaadili: Darasani huhudhulii, ukihudhulia mazoezi hufanyi, unakwepa usafi wa shule na kazi nyingine za nje, nk, wangekufanyaje?! Shukuru hawakukufukuza shule waliona bora wakuchape yaishe kuliko k ukufukuza shule.
 
Kuna siku watakutana na watu waliopinda wawafungulie kesi za madai ya kuchafuliwa majina, hapo ndo akili zao zitapata akili..!
 
Kitaaluma makosa hayo ni makubwa sana. Kwa akili ya mtaani linaweza kuonekana jambo dogo na hata kukosa mchango humu JF.

Yaani kwa sasa rfa wanako elekea siju mwisho wao ni wapi maana wamepoteza mwelekeo wa kiutangazaji kabisa.
 
Umesema kweli mkuu naaamini uongozi wa rfa na redio nyingine wanaingia humu cha muhimu wajirekebishe na wasirudie hili kosa.

Tatizo ni hao watangazaji wenyewe wanao ajiriwa hawana maadili kuanzia huko kwenye malezi yao,wachilia mbali ethics za utangazaji
 
Yaani kutandikwa stiki imekuwa mada ya kusikilizwa RFA!!!!!

Katoto kana kiburi ukikaacha kafanye kanavyojiskia haiwi shule tena.binafsi kila nikikumbuka nilichapwa kwa makosa yepi huwa najikuta nakuwa makini sana.kuchelewa,kuchomekea,kufeli,uchafu,uharibifu Wa Mali za shule,nidham,homework,

Kama ulifanikiwa kukwepa vyote hivyo,wewe ni zaidi ya mwalimu.
 
Nilikuwa na uwezo kimasomo darasani lakini nilikuwa nikikosa maswali matano kati ya hamsini nilitandikwa barabara na walimu wangu.Nia kuu ilikuwa natakiwa nipate yote au angalau nikose mawili tu.Na faida ya wao kuwa wakali leo hii naiona katika maisha.Hakika nilikosa raha na kuongeza umakini na sijawachukia walimu.Hiyo ilikuwa ni miaka ya themanini hadi tisini mwanzoni.Isipokuwa huwa katika maongezi naongea kwa utani na kuwakumbuka watu wangu na wazazi wangu wale wazuri.Wasirudie tena huo upuuzi hao wanahabari mkuu.
 
Back
Top Bottom