Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 17,464
- 21,195
Wakati ulimwengu ukijiandaa kuangalia pambano la kukata na shoka kati ya Floyd Mayweather(The Pretty Boy) na Conor McGregor mnamo tarehe 26 August pamoja na lile la Canelo Alvarez na Gennady Golovkin mnamo September.
Wadau wengi wa ngumi pamoja na ma boxer's wengi wamekuwa na mtazamo tofauti hasa pambano la Floyd na McGregor.
Miongoni mwa mabondia wanaolipinga kwa vikali pambano ni pamoja na Manny Pacquiao au mzee wa cherehani kama vijana wengi wa mtaani wanavyopenda kumuita kutokana na kasi na ngumi zake nyingi za mfululizo kwa wakati mmoja .
Pacquiao amekuwa akiliponda mara kwa mara pambano hilo akidai kuwa McGregor hana uwezo hata kidogo wa kumkalisha Floyd hivyo kitendo cha kumpanga Floyd na McGregor ni kitendo cha kumuonea sana McGregor na kumuongezea idadi ya mapambano ya ushindi Floyd
View attachment 552843
Mbali na Pac,bondia mwengine ambaye aliwahi kutamba miaka ya nyuma kidogo aitwae Sugar ray Leonard naye amekuwa akikosoa vikali pambano hilo ,hata hivyo kadri hili pambano linavyozidi kukosolewa ndivyo hamu ya kutazama pambano hili linazidi kuzidi na wadhamini wengi ndivyo wanavyozidi kumiminika.
Katika pambano hilo Floyd ataondoka na dola za kimarekani 250Million wakati Conor atapata us dollars 75Million ingawaje kwa Conor hili ndilo pambano alilopata pesa kubwa zaidi.
Floyd amedai kuwa hili ndilo pambano lake la mwisho na hatopigana tena.
Lakini wapenzi wa mchezo wa boxing wamemtaka Floyd kabla hajastafu apande ulingoni arudiane na Canelo Alvarez.
Santos Saul Alvarez au jina la utani Canelo Alvarez amepigana mapambano 51 na kati ya hayo ameshinda 49 ametoka sare pambano moja na amepigwa pambano moja na Floyd Mayweather .
Mashabiki wa Canelo wanadai Floyd alimpiga Canelo kipindi kile kwa sababu Canelo hakuwa na uzoefu wa kutosha kipindi hicho ila kwa sasa wanaimani kubwa Floyd hawezi kumaliza hata round tano akizipiga na Canelo Alvarez.
View attachment 552855Santos Saul Alvarez(Canelo Alvarez)
View attachment 552856
Unbeaten man Floyd Mayweather.
Nikiwa kama shabiki nguli wa Floyd nasemaje Floyd ataendelea kuwa bora karne na karne hatotokea mtu wa kumkalisha dunia hii hata warudiane mara mia huyu dogo bado ataendelea kupokea kichapo tu.
Wadau wengi wa ngumi pamoja na ma boxer's wengi wamekuwa na mtazamo tofauti hasa pambano la Floyd na McGregor.
Miongoni mwa mabondia wanaolipinga kwa vikali pambano ni pamoja na Manny Pacquiao au mzee wa cherehani kama vijana wengi wa mtaani wanavyopenda kumuita kutokana na kasi na ngumi zake nyingi za mfululizo kwa wakati mmoja .
Pacquiao amekuwa akiliponda mara kwa mara pambano hilo akidai kuwa McGregor hana uwezo hata kidogo wa kumkalisha Floyd hivyo kitendo cha kumpanga Floyd na McGregor ni kitendo cha kumuonea sana McGregor na kumuongezea idadi ya mapambano ya ushindi Floyd
View attachment 552843
Mbali na Pac,bondia mwengine ambaye aliwahi kutamba miaka ya nyuma kidogo aitwae Sugar ray Leonard naye amekuwa akikosoa vikali pambano hilo ,hata hivyo kadri hili pambano linavyozidi kukosolewa ndivyo hamu ya kutazama pambano hili linazidi kuzidi na wadhamini wengi ndivyo wanavyozidi kumiminika.
Katika pambano hilo Floyd ataondoka na dola za kimarekani 250Million wakati Conor atapata us dollars 75Million ingawaje kwa Conor hili ndilo pambano alilopata pesa kubwa zaidi.
Floyd amedai kuwa hili ndilo pambano lake la mwisho na hatopigana tena.
Lakini wapenzi wa mchezo wa boxing wamemtaka Floyd kabla hajastafu apande ulingoni arudiane na Canelo Alvarez.
Santos Saul Alvarez au jina la utani Canelo Alvarez amepigana mapambano 51 na kati ya hayo ameshinda 49 ametoka sare pambano moja na amepigwa pambano moja na Floyd Mayweather .
Mashabiki wa Canelo wanadai Floyd alimpiga Canelo kipindi kile kwa sababu Canelo hakuwa na uzoefu wa kutosha kipindi hicho ila kwa sasa wanaimani kubwa Floyd hawezi kumaliza hata round tano akizipiga na Canelo Alvarez.
View attachment 552855Santos Saul Alvarez(Canelo Alvarez)
View attachment 552856
Unbeaten man Floyd Mayweather.
Nikiwa kama shabiki nguli wa Floyd nasemaje Floyd ataendelea kuwa bora karne na karne hatotokea mtu wa kumkalisha dunia hii hata warudiane mara mia huyu dogo bado ataendelea kupokea kichapo tu.