Mtalii wa Kisiasa
Member
- May 3, 2019
- 53
- 144
RELI YA STANDARD GAUGE,BWAWA LA RUFIJI,MIDEGE ATCL VINATOSHA KUJIBU HOJA YA ZITTO.
Leo 10:15am,29/09/2019.
Awamu ya tano ina miradi mingi nchi nzima,miradi inayoonekana kwa macho na sio miradi hewa ama ya kitapeli kama miradi tuliyowahi kuisikia siku za nyuma,Miradi mingi ya barabara nchi nzima, meli, vivuko, umeme, maji, afya, utalii, bandari, viwanja vya ndege. Kodi inayokusanywa haifikii hizo gharama za miradi yote hiyo.
Zitto anapaswa kujua kama tunakopa basi pesa inakwenda mahali sahihi katika miradi hiyo na si vinginevyo,Zitto alipaswa kuja na hoja kama takwimu za deni kuongezeka zimesababishwa na wizi,ufisadi au matumizi mabaya na sio kuja na takwimu za deni linalojenga miradi mbalimbali na kusema deni ni kubwa kuliko deni la Awamu ya nne,huu ni ujinga.
Nimuulize ndugu Zitto,kwani awamu ya 4 zilifanyika shughuli gani za kiuchumi zinazoonekana kwa macho haya ya mwili?!!......mbona ilikopa fedha nyingi sana!!!!
Zitto unasema zile barabara ambazo kila leo tunamkweza Magufuli zilijengwa awamu ya nne,lakini Awamu hii ya tano imeenda mbali kuzitanua na kujenga barabara nane,
Zitto unasema Pesa ambazo zilizojenga daraja la Kigamboni zilitoka awamu ya nne,lakini Awamu ya tano inajenga daraja la baharini la Surrender na daraja la Kigongo,Busisi katika Ziwa Victoria lenye urefu wa zaidi ya Kilomita tatu na nusu,Unasema UDOM ilijengwa awamu ya nne,lakini umeona mifuko ya pensheni ya Uzeeni ilivyoyumba hata kuanzisha kikokotoo kipya!?
Ni sawa kabisa Awamu ya nne ili-invest kwenye social services lakini Awamu hii ya tano ina-invest kwenye miradi mikubwa ambayo nimeitaja.
Zitto unasema Awamu ya tano imejenga Zahanati 300 nchi nzima,Unasema tukizichanganya zote pamoja zinaweza kufikia gharama za hospitali moja ya Mloganzila.
Zitto unasema Awamu ya tano imetumia zaidi ya Trilioni moja kununua ndege wakati Awamu ya nne ilitumia zaidi ya trilioni moja kujenga chuo kikuu cha Udom,Ni sawa kabisa lakini wanafunzi wanaomaliza Udom wangeenda kufanya kazi wapi!?
Awamu ya tano imeamua kufufua mashirika ya Atcl na Ttcl ili kurejesha ajira,kurejea kwa Atcl kuna hitaji iwe na ndege zaidi ya thelathini ili kukidhi soko na sasa tayari tuna ndege 11 nane tayari zinafanya biashara na zinaleta faida kubwa na tatu zinamaliziwa kutengenezwa kiwandani.
Zitto unasema Awamu ya tano haijapandisha Mshahara wala hakuna ajira ila deni limeongezeka,Awamu ya tano imejitahidi sana kulipa malimbikizo ya Watumishi yaliyotokana na Awamu ya tatu na Awamu ya nne,
Hivyo basi Awamu ya tano imetumia gharama nyingi kusawazisha makosa ya Awamu ya nne na kulipa malimbikizo na madai ya Awamu za nyuma,tunatumaini baada ya hapo Taifa litatembea kwa miguu yake na kupiga hatua kubwa mbele.
Zitto unasema Terminal three ni mradi wa Awamu ya nne lakini ahujui mradi ulisimama 2015 hadi Awamu ya tano ilipofanya tathmini upya,lakini terminal three ni theluthi tu ya miradi mikubwa ya Awamu ya tano,kutaja miradi michache tu,
1.Ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard gauge)
2.Ujenzi wa bomba la mafuta la Uganda ambalo litahusu vile vile upanuzi wa bandari ya Tanga
Ujenzi wa Export Processing Zone ya Kurasini – itakayokuwa mhimili wa biashara kati ya China na Ukanda huu wa Afrika.
3.Kufufuliwa kwa ATCL na TTCL.
4.Ununuzi wa ndege 10 zikiwemo Boeing 3 na Airbus 4.
5.kuhamia Mji Mkuu wa Dodoma.
6.Upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam.
7.Ujenzi wa daraja la kilomita tatu katika Ziwa Victoria.
8.Ujenzi wa Meli nane katika Ziwa Nyasa,Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika.
9.Ujenzi wa Bwawa kubwa la Umeme la Rufiji kwa jina la Mwalimu Nyerere Dam.
10.Mradi wa kuzalisha megawati 240 za umeme wa Kinyerezi II unaoendelea kujengwa.
11.Miradi ya kupanua viwanja vya ndege nchini kwa mfano- Dodoma, na mingine inayoendelea -katika viwanja vya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya n.k.
12.Ujenzi wa maghala ya taifa ya kuhifadhi chakula yenye uwezo wa kuhifadhi tani 350 yatakayojengwa kwa msaada wa Serikali ya Hungary katika sehemu mbalimbali nchini hususan katika mikoa inayozalisha mazao ya nafaka kwa wingi.
13.Ujenzi wa Viwanda kama cha kutengeneza marumaru cha Mkuranga, Pwani ambacho ujenzi wake unaendelea
Kiwanda cha kuzalisha mbolea mkoani Lindi – kinajengwa
Kiwanda cha bidhaa za chuma – mkoani Pwani ambacho kiko mbioni kukamilika.
14. Sambamba na ujenzi wa meli 8, kuna upanuzi wa banadari ya Mwanza, na kuna ujenzi wa meli yenye kubwa ukanda wa A.Mashari na Kati - huko Mwanza (unaendelea).
15. Upanuzi wa viwanja wa ndege mbalimbali hapa nchini.
16. Upanuzi, ujenzi na uboreshwaji wa miundo mbinu mbalimbali ya barabara hapa nchini.
17. Uimarishwaji wa miundombinu na usambazaji wa umeme hapa nchini.
18. Elimu na mikopo kwa vijana wetu, Elimu bora hadi kidato cha 4, mafunzo bure kupitia VETA, etc
19. Ujenzi na ukarabati wavyama hospitali, vituo vya afya na zahanati mbalimbali hapa nchini, uboreshaji wa huduma za afya ikiwa ni pamoja na kuweka vifaa vya kisasa na kuongeza maarifa kwa wataalamu.
20.Interchange kubwa kabisa ya Ubungo.
21.Fly Over ya Mfugale pale Tazara.
22.Daraja la baharini la Surrender.
Kwa hakika vitu ni vingi ila muda ni mchache.
-Nikukumbushe tu Awamu ya tano ilivyoanza 2016.
Hostel za Chuo cha UDSM.
Hostel za Askari Magereza.
Ununuzi wa Ndege 2 (Nyingine 3 zikaja ndani ya Mwaka huo huo wa 2016).
Ujenzi wa Flyover Tazara na Ubungo
Upanuzi wa Airport Mwanza
Upanuzi barabara ya Moroco Dar es Salaam.
Upanuzi wa Kisasa Airport Dar
Kukomesha Rushwa
Kurejesha nidhamu Makazini.
-Na haya yalianza tarehe 12/4/2017;
Uzinduzi ujenzi wa reli kwa ajili ya treni ya Umeme.
Ujenzi wa barabara ya Mtwara-Tandahimba
Kukomesha Watumishi Wenye Feki hivyo kuokoa Mabilioni ya Fedha.
Barabara ya kuunganisha Wilaya za Kibondo kigoma Kaliua huko Tabora.
Miradi Mikubwa ya Maji :
Uwezeshaji Ujenzi Bomba la Mafuta kutoka Hoima mpaka Tanga.
Kwa kweli Awamu ya tano chini ya Rais wetu John Magufuli imefanya makubwa sanaa.
Kila upitapo sasa hivi ni ujenzi unaendelea...Dar es Salaam kila kona Barabara ya Tandale-Sinza- Mawasiliano barabara imejengwa,Mitaa ya Kinondoni hivi ina lami,Ubungo Interchange inajengwa
Madaraja yanajengwa
Upanuzi wa barabara kuu ya Ubungo hadi chalinze unafanywa
Daraja Kilombero miaka yote wapigaji walikuwa wanakula hela za wananchi kuwavusha ila sasa limejengwa
-Flyovers zinajengwa
Miradi ya umeme inajengwa na miradi mingi ni kwa hela za watanzania wenyewe.
Miaka yote maeneo ya Mbezi na kimara walikuwa hawapati maji japo yanapita njia hiyo hiyo lakini sasa maji yamefika mbezi, na bado wanaendelea kutandaza mabomba ili kupeleka maji.
Awali waliokuwa wanakula hela za wananchi ni wenye miradi ya kuuza maji kwa magari. Ila sasa wananchi wamekombolewa.
Utendaji kazi umeimarika, sasa hivi kila mmoja anaona cheo akipewa ni kama kakalia kaa la moto..Yale mambo ya kupiga hela na kukaa ofisini kupiga usingizi yameisha watu ni kazi la sivyo unawajibishwa.
Madawa sasa yanapatikana hospitali, ile hali ya madawa ya hospitali yanapelekwa katika Pharmas binafsi imeisha.
Hospitali sasa za serikali ukienda mgonjwa anajaliwa sio kama ilivyokuwa awali.
Taasisi za serikali wafanyakazi wamekuwa wanawajibika ....hakika nidhamu imeimarika.
Kwa sasa taasisi za serikali zinajiendesha kibiashara na si kihasara kama ilivyokuwa awali, ilikuwa ni ulaji tuu wa hela, upigaji dili, taasisi zinakufa, hakuna gawio kwa serikali, ila sasa zinatoa gawio...Hakika kila kitu ni usimamizi imara, ukicheka na kima utavuna mabua.
Awali watu walikuwa wanaulilia uongozi, hata wasio kuwa na elimu walikuwa wanagombea kupata uongozi, sasa uongozi umekuwa mgumu sababu kama wewe si muwajibikaji una ndoto za kupiga tuu, hupati nafasi, Uongozi umekuwa una hadhi kwa sasa.
Hakika Naisifu Serikali ya CCM ya Awamu ya tano,Namsifu sana Rais wetu John Magufuli.
Nimalizie kwa kusema,Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni,Mungu Mbariki Rais wetu John Magufuli,Mungu ibariki Tanzania.
Nikiishia hapa,Mimi ni,
Msemakweli Chakubanga.
Dar es Salaam.
0755078854.
Leo 10:15am,29/09/2019.
Awamu ya tano ina miradi mingi nchi nzima,miradi inayoonekana kwa macho na sio miradi hewa ama ya kitapeli kama miradi tuliyowahi kuisikia siku za nyuma,Miradi mingi ya barabara nchi nzima, meli, vivuko, umeme, maji, afya, utalii, bandari, viwanja vya ndege. Kodi inayokusanywa haifikii hizo gharama za miradi yote hiyo.
Zitto anapaswa kujua kama tunakopa basi pesa inakwenda mahali sahihi katika miradi hiyo na si vinginevyo,Zitto alipaswa kuja na hoja kama takwimu za deni kuongezeka zimesababishwa na wizi,ufisadi au matumizi mabaya na sio kuja na takwimu za deni linalojenga miradi mbalimbali na kusema deni ni kubwa kuliko deni la Awamu ya nne,huu ni ujinga.
Nimuulize ndugu Zitto,kwani awamu ya 4 zilifanyika shughuli gani za kiuchumi zinazoonekana kwa macho haya ya mwili?!!......mbona ilikopa fedha nyingi sana!!!!
Zitto unasema zile barabara ambazo kila leo tunamkweza Magufuli zilijengwa awamu ya nne,lakini Awamu hii ya tano imeenda mbali kuzitanua na kujenga barabara nane,
Zitto unasema Pesa ambazo zilizojenga daraja la Kigamboni zilitoka awamu ya nne,lakini Awamu ya tano inajenga daraja la baharini la Surrender na daraja la Kigongo,Busisi katika Ziwa Victoria lenye urefu wa zaidi ya Kilomita tatu na nusu,Unasema UDOM ilijengwa awamu ya nne,lakini umeona mifuko ya pensheni ya Uzeeni ilivyoyumba hata kuanzisha kikokotoo kipya!?
Ni sawa kabisa Awamu ya nne ili-invest kwenye social services lakini Awamu hii ya tano ina-invest kwenye miradi mikubwa ambayo nimeitaja.
Zitto unasema Awamu ya tano imejenga Zahanati 300 nchi nzima,Unasema tukizichanganya zote pamoja zinaweza kufikia gharama za hospitali moja ya Mloganzila.
Zitto unasema Awamu ya tano imetumia zaidi ya Trilioni moja kununua ndege wakati Awamu ya nne ilitumia zaidi ya trilioni moja kujenga chuo kikuu cha Udom,Ni sawa kabisa lakini wanafunzi wanaomaliza Udom wangeenda kufanya kazi wapi!?
Awamu ya tano imeamua kufufua mashirika ya Atcl na Ttcl ili kurejesha ajira,kurejea kwa Atcl kuna hitaji iwe na ndege zaidi ya thelathini ili kukidhi soko na sasa tayari tuna ndege 11 nane tayari zinafanya biashara na zinaleta faida kubwa na tatu zinamaliziwa kutengenezwa kiwandani.
Zitto unasema Awamu ya tano haijapandisha Mshahara wala hakuna ajira ila deni limeongezeka,Awamu ya tano imejitahidi sana kulipa malimbikizo ya Watumishi yaliyotokana na Awamu ya tatu na Awamu ya nne,
Hivyo basi Awamu ya tano imetumia gharama nyingi kusawazisha makosa ya Awamu ya nne na kulipa malimbikizo na madai ya Awamu za nyuma,tunatumaini baada ya hapo Taifa litatembea kwa miguu yake na kupiga hatua kubwa mbele.
Zitto unasema Terminal three ni mradi wa Awamu ya nne lakini ahujui mradi ulisimama 2015 hadi Awamu ya tano ilipofanya tathmini upya,lakini terminal three ni theluthi tu ya miradi mikubwa ya Awamu ya tano,kutaja miradi michache tu,
1.Ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard gauge)
2.Ujenzi wa bomba la mafuta la Uganda ambalo litahusu vile vile upanuzi wa bandari ya Tanga
Ujenzi wa Export Processing Zone ya Kurasini – itakayokuwa mhimili wa biashara kati ya China na Ukanda huu wa Afrika.
3.Kufufuliwa kwa ATCL na TTCL.
4.Ununuzi wa ndege 10 zikiwemo Boeing 3 na Airbus 4.
5.kuhamia Mji Mkuu wa Dodoma.
6.Upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam.
7.Ujenzi wa daraja la kilomita tatu katika Ziwa Victoria.
8.Ujenzi wa Meli nane katika Ziwa Nyasa,Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika.
9.Ujenzi wa Bwawa kubwa la Umeme la Rufiji kwa jina la Mwalimu Nyerere Dam.
10.Mradi wa kuzalisha megawati 240 za umeme wa Kinyerezi II unaoendelea kujengwa.
11.Miradi ya kupanua viwanja vya ndege nchini kwa mfano- Dodoma, na mingine inayoendelea -katika viwanja vya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya n.k.
12.Ujenzi wa maghala ya taifa ya kuhifadhi chakula yenye uwezo wa kuhifadhi tani 350 yatakayojengwa kwa msaada wa Serikali ya Hungary katika sehemu mbalimbali nchini hususan katika mikoa inayozalisha mazao ya nafaka kwa wingi.
13.Ujenzi wa Viwanda kama cha kutengeneza marumaru cha Mkuranga, Pwani ambacho ujenzi wake unaendelea
Kiwanda cha kuzalisha mbolea mkoani Lindi – kinajengwa
Kiwanda cha bidhaa za chuma – mkoani Pwani ambacho kiko mbioni kukamilika.
14. Sambamba na ujenzi wa meli 8, kuna upanuzi wa banadari ya Mwanza, na kuna ujenzi wa meli yenye kubwa ukanda wa A.Mashari na Kati - huko Mwanza (unaendelea).
15. Upanuzi wa viwanja wa ndege mbalimbali hapa nchini.
16. Upanuzi, ujenzi na uboreshwaji wa miundo mbinu mbalimbali ya barabara hapa nchini.
17. Uimarishwaji wa miundombinu na usambazaji wa umeme hapa nchini.
18. Elimu na mikopo kwa vijana wetu, Elimu bora hadi kidato cha 4, mafunzo bure kupitia VETA, etc
19. Ujenzi na ukarabati wavyama hospitali, vituo vya afya na zahanati mbalimbali hapa nchini, uboreshaji wa huduma za afya ikiwa ni pamoja na kuweka vifaa vya kisasa na kuongeza maarifa kwa wataalamu.
20.Interchange kubwa kabisa ya Ubungo.
21.Fly Over ya Mfugale pale Tazara.
22.Daraja la baharini la Surrender.
Kwa hakika vitu ni vingi ila muda ni mchache.
-Nikukumbushe tu Awamu ya tano ilivyoanza 2016.
Hostel za Chuo cha UDSM.
Hostel za Askari Magereza.
Ununuzi wa Ndege 2 (Nyingine 3 zikaja ndani ya Mwaka huo huo wa 2016).
Ujenzi wa Flyover Tazara na Ubungo
Upanuzi wa Airport Mwanza
Upanuzi barabara ya Moroco Dar es Salaam.
Upanuzi wa Kisasa Airport Dar
Kukomesha Rushwa
Kurejesha nidhamu Makazini.
-Na haya yalianza tarehe 12/4/2017;
Uzinduzi ujenzi wa reli kwa ajili ya treni ya Umeme.
Ujenzi wa barabara ya Mtwara-Tandahimba
Kukomesha Watumishi Wenye Feki hivyo kuokoa Mabilioni ya Fedha.
Barabara ya kuunganisha Wilaya za Kibondo kigoma Kaliua huko Tabora.
Miradi Mikubwa ya Maji :
Uwezeshaji Ujenzi Bomba la Mafuta kutoka Hoima mpaka Tanga.
Kwa kweli Awamu ya tano chini ya Rais wetu John Magufuli imefanya makubwa sanaa.
Kila upitapo sasa hivi ni ujenzi unaendelea...Dar es Salaam kila kona Barabara ya Tandale-Sinza- Mawasiliano barabara imejengwa,Mitaa ya Kinondoni hivi ina lami,Ubungo Interchange inajengwa
Madaraja yanajengwa
Upanuzi wa barabara kuu ya Ubungo hadi chalinze unafanywa
Daraja Kilombero miaka yote wapigaji walikuwa wanakula hela za wananchi kuwavusha ila sasa limejengwa
-Flyovers zinajengwa
Miradi ya umeme inajengwa na miradi mingi ni kwa hela za watanzania wenyewe.
Miaka yote maeneo ya Mbezi na kimara walikuwa hawapati maji japo yanapita njia hiyo hiyo lakini sasa maji yamefika mbezi, na bado wanaendelea kutandaza mabomba ili kupeleka maji.
Awali waliokuwa wanakula hela za wananchi ni wenye miradi ya kuuza maji kwa magari. Ila sasa wananchi wamekombolewa.
Utendaji kazi umeimarika, sasa hivi kila mmoja anaona cheo akipewa ni kama kakalia kaa la moto..Yale mambo ya kupiga hela na kukaa ofisini kupiga usingizi yameisha watu ni kazi la sivyo unawajibishwa.
Madawa sasa yanapatikana hospitali, ile hali ya madawa ya hospitali yanapelekwa katika Pharmas binafsi imeisha.
Hospitali sasa za serikali ukienda mgonjwa anajaliwa sio kama ilivyokuwa awali.
Taasisi za serikali wafanyakazi wamekuwa wanawajibika ....hakika nidhamu imeimarika.
Kwa sasa taasisi za serikali zinajiendesha kibiashara na si kihasara kama ilivyokuwa awali, ilikuwa ni ulaji tuu wa hela, upigaji dili, taasisi zinakufa, hakuna gawio kwa serikali, ila sasa zinatoa gawio...Hakika kila kitu ni usimamizi imara, ukicheka na kima utavuna mabua.
Awali watu walikuwa wanaulilia uongozi, hata wasio kuwa na elimu walikuwa wanagombea kupata uongozi, sasa uongozi umekuwa mgumu sababu kama wewe si muwajibikaji una ndoto za kupiga tuu, hupati nafasi, Uongozi umekuwa una hadhi kwa sasa.
Hakika Naisifu Serikali ya CCM ya Awamu ya tano,Namsifu sana Rais wetu John Magufuli.
Nimalizie kwa kusema,Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni,Mungu Mbariki Rais wetu John Magufuli,Mungu ibariki Tanzania.
Nikiishia hapa,Mimi ni,
Msemakweli Chakubanga.
Dar es Salaam.
0755078854.