Regia mtema memorial event

Regia mtema memorial event

PISTO LERO

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2011
Posts
2,819
Reaction score
1,455
.........................REGIA MTEMA MEMORIAL EVENT...................

Siku ya Jumatatu; tarehe 14 January 2013 ni siku ambayo Regia Mtema Foundation imeitenga maalumu kwa ajili ya kumbukumbu ya Regia Mtema. Katika siku hii maalumu wote mnakaribishwa Peacock Hotel ambako kutakuwa na maada mbalimbali zitakazowasilishwa na kujadiliwa kama alivyozisimamia Regia. Katika siku hii maalumu wageni na wadau mbalimbali wamethibitisha kushiriki.Hafla hii maalumu itaanza saa 9.00 Alasiri na kumalizika 2.00 usiku na kisha kufuatiwa na chakula cha usiku.



Ratiba kamili itahusisha matukio yafuatayo:

Historia ya Regia itakayowasilishwa na Mh. David Kafulila
Mada juu ya Rushwa itakayowakilishwa na Takukuru
Ulemavu Siyo Kutoweza itakayowasilishwa na Bi Shida Salum - Mwenyekiti CHAWATA
Nafasi ya Kijana katika kuchochea maendeleo na demokrasia - Mh. January Makamba


MIDAHALO:


Documentary za Regia Mtema
Remarks kutoka kwa Mh. Zitto Kabwe; Mh. John Mnyika na Hussein Bashe na Mzee Mtema
Chakula cha jioni
Networking


Wasimamizi wa hafla hii watakuwa: Pascal Mayalla na Lara Williams

MJENGWA.
 

Attachments

  • mtema_572fd.jpg
    mtema_572fd.jpg
    32.2 KB · Views: 49
naomba ufafanuzi,wanaotakiwa kuhudhuria?kuna limit ya watu fulani au?
 
Back
Top Bottom