tatamajuva
Member
- Sep 11, 2019
- 74
- 84
REFORMATION NI MUHIMU CWT
Wiki Jana 15 may 2020 kulikuwa na uchaguzi wa viongozi cwt ngazi ya wilaya shinyanga DC. Kwakweli CWT kimekuwa siyo chama cha kutetea maslahi ya walimu bali ni cha wachumia tumbo kutokana na mchakato wako ulivyoendeshwa. It's shame! Uchaguzi uliojaa rushwa, uchaguzi ambao uongozi uliokuwepo ulipanga nani awe kiongozi wa chama hicho, haiwezekani viongozi wa CWT waandae malazi ya wapiga kura, chakula, vinywaji for 2 days. Hivi unataraji tutapata viongozi wazuri katika chama hiki?
CWT shinyanga DC ni uozo mtupu, haijawahi kushuhudiwa hali hii, baada ya uchaguzi kuna kiongozi aligombea nafasi ya mkoa na kwa njia ileile aliyotumia alishinda lakini nafasi ya ngazi ya wilaya tayari aliandaliwa mtu ambaye kamati imekubaliana awe huyo headmaster wa shule fulani, je, tutafika?
CWT ni jipu linalosubiri kutumbuliwa, na mtumbuaji ni mkuu wa nchi.
CWT wanagawa T-shirt siku 10 baada ya sherehe za Mei Mosi? Hii syndicate ya baadhi ya watu, na kwa manufaa yao ya kulindana ili kuchumia tumbo.
Mwakilishi wa shule moja ya msingi aliandikiwa barua ya kutenguliwa kushiriki mkutano mkuu kwa kukosa sifa siku 1 kabla ya uchaguzi CWT Shy DC na hii ilitokana na mwakilishi huyu kuwa na msimamo thabiti alipoambiwa awasilishe salary slip 3 na barua iliyoandikwa kwake ni kupitia kwa mkuu wa shule ambapo ni kinyume na katiba, pia mkuu wa shule aliteua mwakilishi mwingine kinyume na katiba, hivyo uchaguzi kukiukwa kwa kiwango cha hali ya juu.
Mwakilishi huyo alirusha barua hiyo kwenye group fulani la WhatsApp na ndipo taarifa hii ilipothibitika na huu ni uonevu mkubwa, kwani anastahili kulipwa stahiki zake kama mwakilishi halali, pili mwakilishi aliyeteuliwa. Na mkuu wa shule alipiga kura kinyume na katiba inayotaka mwakilishi achaguliwe na wanachama katika kituo cha kazi.
Ova
Sent using Jamii Forums mobile app