Reels zinaisha lakini Roho inabaki

Reels zinaisha lakini Roho inabaki

Paspii0

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2020
Posts
638
Reaction score
1,038
Habari zenu mabingwa wa mahekalu ya ghorofa, mabepari wa Instagram, na ma celebrity wa maokoto group,

Twende kazi……………!

Mmejenga nyumba za kupendeza hadi ukipita sakafu inafanya screenshot. Mmeseti vibanda vya mbwa vya kisasa kuliko bedroom ya bibi yangu kijijini matemanga. Mmeweka ring light hadi kabati linapiga pose. Ila Biblia iko pale juu ya friji, ikifuga vumbi na maneno ya uzima.

Yaani wardrobe yenu ina rangi zote za rainbow, lakini hamjui hata kama Warumi walikuwa watu au wimbo wa Aslay.

Kila siku mnachapisha…!

"Hustle hard, sleep later."
"Secure the bag."
"Catch flights not feelings."


Lakini hata mstari mmoja wa Zaburi 23 mnausoma kama ni bio ya mtu mwingine.

Sawa jamani, mafanikio ni baraka. Lakini sasa hadi Mungu anabisha hodi anasema …….

"Hodi? Au ndo nime unfollowiwa?"

Tusome kidogo Biblia (usipate pressure, hata app ni sawa)…..!

“Maana mwanadamu atafaidi nini akiupata ulimwengu wote, lakini akapoteza roho yake?” Marko 8:36

Wewe kila siku unapiga “manifesting mansion, manifesting Maldives”, lakini hujawahi manifest sala hata ya dakika mbili. Umejaa wishlists lakini huna prayer list.

Yesu alisema……!

“Tafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake, na hayo mengine mtazidishiwa.” Mathayo 6:33

Lakini nyinyi mmepanga hivi……!

  1. Tafuta followers
  2. Tafuta Pesa au maokoto
  3. Tafuta Mwanaume au Mwanamke wa ndoto
  4. Halafu maybe Mungu akitokea, mpe Sunday 10:30 - 12:00 (kama hakuna EPL)
Kumbuka, kaburi hakina balcony. Hakuna Netflix kule, hakuna Wi-Fi, na hakuna rebranding. Ni wewe, roho yako, na CV ya matendo yako. Yamkini Msalaba wa kaburi ndio antenna 😇…

“Kuna wakati kwa kila jambo chini ya jua...” Mhubiri 3:1

Lakini pia kuna mwisho wa kila kitu. Hiyo deadline ya roho haina snooze button.

Basi ndugu zang kabla hujanunua Tesla ya kuonyesha kwa ex, nunua muda wa kukumbuka Muumba wako. Ukinunua iPhone 39 Pro Max Ultra AI Edition, pakua pia Bible App. Usisahau kupiga update ya kiroho.

Na mwisho kabisa, kama una t shirt 80 na jirani hana hata moja ya kujifunika, hiyo si fashion hiyo ni kufunga macho kwa maumivu ya binadamu.

“Yeyote mwenye kanzu mbili na amgawie asiye na yoyote.” Luka 3:11

Kwa hiyo kabla hujapost “2025 Goals, Soft life only”, tafadhali andika hii kwanza….!

“Goal #1: Kumbuka una roho.”

Wasalaam kwa upendo, hekima na kawarning ka upole,

Mtumishi asiye verified

~mwanenu Chavalikungu!



 
Ndugu Paspii0 umeongea vema sana..
Umemzungumzia tajiri kwa mambo mengi,kujenga nyumba ya fahari,nguo nyingi, na kabla ya kununua Tesla apakue bible app,nk…

Vipi kuhusu maskini,yeye anapaswa kukumbuka kufanya nini kabla hajalala njaa,kabla hajapata hela ya kulipa kodi ya nyumba nk…. Kwa maana hakuna heri kwa tajiri wala maskini ktk kumtumikia Mungu. Pia tajiri na masikini wote ni sawa mbele za bwana.
 
🙏
Vipi kuhusu maskini,yeye anapaswa kukumbuka kufanya nini kabla halala njaa,kabla hajapata hela ya kulipa kodi ya nyumba nk…. Kwa maana hakuna heri kwa tajiri wala maskini ktk kumtumikia Mungu. Pia tajiri na masikini wote ni sawa mbele za bwana.
Masikini pia anapaswa kuwa na uhusiano wa karibu na Mungu, akijua kwamba siyo mali au hali ya kiuchumi inayomfanya kuwa na maana mbele za Mungu, bali ni moyo wake na nia yake.

Masikini lazima atambue kumtanguliza Mungu katika kila hali. Hata kabla hajapata chakula cha leo au kodi ya nyumba, maskini anapaswa kuwa na shukrani kwa kile alicho nacho, hata kama ni kidogo. Biblia inatufundisha kuwa Mungu ni mtoa kwa wingi, na hata maskini ana haki ya kumtumikia Mungu kwa uaminifu, akijua kwamba Mungu hatamwacha katika dhiki.

Lamsingi hapa tuzingatie kwamba kama ilivyo kwa tajiri, maskini anapaswa kuwa na ushirika wa kiroho na Mungu, akijua kuwa mali au umasikini havimfanyi mtu kuwa bora au duni mbele za Mungu. Mungu anataka wote tuwe na moyo wa kutaka kumtumikia kwa uaminifu, iwe tajiri au maskini.

REJEA …..!
1. Heri maskini wa roho, kwa maana ufalme wa mbinguni ni wao." Mathayo 5:3,
2.Huyu maskini alilia, Bwana akamsikia, Akamwokoa kutoka katika shida zake zote."Zaburi 34:6
3.Vijana wangu wapendwa, je, Mungu hakuwachagua maskini wa ulimwengu huu kuwa matajiri katika imani na warithi wa ufalme alioahidi wale wanaompenda?"Yakobo 2:5
 
Back
Top Bottom