Redio za Tanzania na BBC

Redio za Tanzania na BBC

Joined
Jun 15, 2015
Posts
73
Reaction score
9
Habari wana jf!

Moja kwa moja bila kupoteza muda napenda kutoa dukuduku langu la moyoni ambalo limekuwa likinipa wakati mgumu sana juu ya redio za hapa nchini. Tofauti na watangazaji wa BBC Idhaa ya Kiswahili au BBC Eglish, redio zetu zinakera sana.

Muda wote ni miziki tu mara bolingo, taarabu nk hadi inakera sana. Hakuna ubunifu wowote kwa hawa ndugu zetu watangazaji kama wenzao wa BBC au DW redio ambao muda mwingi wanaweka vipindi vya kuelimisha jamii.

Ushauri wangu, Serikali iendelee kumulika sekta ya habari na mawasiliano na wamiliki wa vyombo vya habari hapa nchini ili kuongeza weledi kataka utoaji wa habari na burudani.

Watangazaji wengi ni kama wamekosa UBUNIFU kama si elimu stahiki juu ya taaluma zao. Nadiliki kusema watangazaji wengi wamepitia vyuo vya uchochoroni( back door).

Sidhani kama watu wa IJMC, St.Augustine na vyuo vyenye majina wanaweza kuishia kupiga nyimbo za bolingo au sindimba,taarabu na nyinginezo saa 24.

Kuna knowledge kubwa sana ambayo inatakiwa kuwa impacted katika jamii ukiachilia mbali changamoto za mwaka wa uchaguzi, BVR, magonjwa yasiyo ambukiza, ajali, mabadiliko ya tabia ya nchi, kilimo, elimu, utamaduni, maadili na mambo mengi kadhaa wa kadhaa ambayo yanaweza kubadilisha jamii na kuleta maendeleo.

Ukifuatialia kamwe huwezi kukuta mijadala kama hiyo ktk redio stesheni zetu.Ukifungulia redio zetu jambo la kwanza ni muziki tuuuuuuuu tumechoka! igeni na kwa watangazaji wenzanu wa BBC, burudani kidogo elimu kwa sana!

Tena siku hizi kuna system unakuta kuna mtangazaji wa kiume na wa kike au jinsia moja kazi ni kubishana wao tu na kujadili upuuzi mara utasikia saa ya kupaka rangi sijui nini wanaishia kupiga umbea tu ukifuatilia kwa umakini utagundua tu kichwani ni empty vessels.

Hawana jipya bora hata vyombo vya habari viwe chini ya TBC Taifa.
icon6.png
icon6.png

 
Wao wanafanya vipindi ambavyo wasikilizaji wanapenda.... utawawekea wabongo news na uchambuzi muda wote hiyo redio utaskiliza mmiliki tu
 
hata hao wanawake ambao ni popular kama lala1 na heaven on earth ambao hata waki comment au kutoa post ya kipuuzi wanapewa 5 kwa sana na comments lukuki they were once Junior members just like me.Naamini ipo siku na mm ntakuwa popular hapa JF na ntabadiliki akili ndogo km hizi zenye mlengo wa kudhalau Juniors.Young boyz make men
 
hata hao wanawake ambao ni popular kama lala1 na heaven on earth ambao hata waki comment au kutoa post ya kipuuzi wanapewa 5 kwa sana na comments lukuki they were once Junior members just like me.Naamini ipo siku na mm ntakuwa popular hapa JF na ntabadiliki akili ndogo km hizi zenye mlengo wa kudhalau Juniors.Young boyz make men
kumbe ni wivu unakusumbua!!? sasa mada yako hapa ni nini? kuhusu TBC au umaarufu wa lara 1 na Heaven on Earth?
 
Last edited by a moderator:
Ndugu mleta mada, tbc taifa ni ya nje au ndani?
 
Yawezekana ukawa na mawazo mazuri ila uwasilishaji wako...hasa pale mwanzo umeonesha kutokujiamini.
 
kumbe ni wivu unakusumbua!!? sasa mada yako hapa ni nini? kuhusu TBC au umaarufu wa lara 1 na Heaven on Earth?

Eti jamaa anataka ziwe chini ya TBC, Angependekeza namna bora ya kuweka taaluma zao ila amekuja kishabiki sana katoa mfano wa watangazaji makini kutoka chuo Fulani,.... loading......
 
Last edited by a moderator:
Tatizo wabongo mmezoea kuropoka tu uchumi wa Uingereza ndiyo unaendesha BBC... Watangazaji wa redio hizo wanalipwa vyema kabisa.... Uchumi wa German unaendesha Deutch Welle..... Jiulize uchumi wa Tz unaendesha TBc je kuna nini huko????? Sio sahihi kuchanganya mambo haya..... Kwa upande wa redio zipo zinazojitahidi kama RFA kuanzia alfajiri saa 11 wanakamua Sana jaribu kusikiliza ila kubwa kuna uwekezaji mdogo kwa wanahabari hasa kuwafanya wawe na mambo mengi ya kuwaelimisha raia..... Serikali na wamiliki wa media Ndio wa kuwalaumu ingawa kwa Kiasi fulani wapo Watangazaji makanjanja ambao sijui wanakula maharage ya wapiii..... Binafsi nawapongeza RFA kuanzia 11....pia redio one baadhi ya nyakati na hata clouds fm Kiasi chake
 
Wamiliki wengi wa media hawana mitaji ya kutosha wanategemea matangazo ya mitandao ya simu akina we ndorobooo nn ndo wawalipe watangazaji Wao pia wale humohumo,hence wanakosa hela za kufanya Utafiti ili kukuletea vipindi vizuri kama hivo vya BBC nk bila TMF kuwaboost holaa! .....afterall hao ijmc siku hzi sjmc st agustine nk wanazalisha sio watangazaji most of the graduates wanaishia kuwa bank tellers,pro au ndo program managers wanaotoa order ya hiyo miziki,zipo radio chache zinajaribu kv rfa,r1,wanaweka vipindi mtambuka the rest ni danzi tu ndo maana kizazi chetu ni kudanzi tu kwenye kila kitu. Limao
 
Wao wanafanya vipindi ambavyo wasikilizaji wanapenda.... utawawekea wabongo news na uchambuzi muda wote hiyo redio utaskiliza mmiliki tu
It is absolutely ulichosema, bila kubadilisha mindset za watu hata ukibadilisha programu za matangazo unaweza kuishia kusikiliza mmiliki peke yake.

Ukifanya research utagundua kuwa zile radio zinazopendelea kutangaza mambo ya udaku ndiyo zinakuwa na wasikilizaji wengi.

Panda kwenye madaladala, almost 90% ya madereva wana-tune radio yso ya udaku ya 'mawingu'

Vivyo hivyo kwenye magazeti, yale yanayoandika mambo serious 'yanadoda' kwenye vibanda vya magazeti, wakati yale ya udaku yanayoandika mambo ya 'vyumbani' mwa watu yakiwa yanagombewa vituoni, hasa hasa na kina dada.

Kwa hiyo la muhimu ni kuanza kuwabadilisha kwanza wananchi fikra zao ili waone madhara ya kuendekeza mambo ya udaku na umuhimu wa kuzingatia mambo ambayo ni serious kwa maisha yao.
 
It is absolutely ulichosema, bila kubadilisha mindset za watu hata ukibadilisha programu za matangazo unaweza kuishia kusikiliza mmiliki peke yake.

Ukifanya research utagundua kuwa zile radio zinazopendelea kutangaza mambo ya udaku ndiyo zinakuwa na wasikilizaji wengi.

Panda kwenye madaladala, almost 90% ya madereva wana-tune radio yso ya udaku ya 'mawingu'

Vivyo hivyo kwenye magazeti, yale yanayoandika mambo serious 'yanadoda' kwenye vibanda vya magazeti, wakati yale ya udaku yanayoandika mambo ya 'vyumbani' mwa watu yakiwa yanagombewa vituoni, hasa hasa na kina dada.

Kwa hiyo la muhimu ni kuanza kuwabadilisha kwanza wananchi fikra zao ili waone madhara ya kuendekeza mambo ya udaku na umuhimu wa kuzingatia mambo ambayo ni serious kwa maisha yao.

Mystery-Spot on:Hata humu JF mambo ni yale yale.Sijaelewa kwa nini Watanzania wengi tunapenda hizo habari za udaku na hasa masuala ya mapenzi.Angalia Threads humu zinazohusu Udaku wa Kingono,comments hadi pomon,lakini member akiweka thread nzuri inayohusu mambo ya msingi ya Mtanzania hah wapi wachangiaje wachahce sana.Hicho hicho ndicho kinatokea kwenye redio,magazeti,TV,nk.!
 
Nakushauri uweke TBC TAIFA na ung'oe tuning gear.
Frequency zipo ili uchague radio unayoitaka si wote wataiga TBC watafungwa kwa kuiba jina na nadharia za vipindi.
 
Tofautisha BBC na radio kama Clouds,Kiss fm,East Afrıca,Magic,Efm,Choıce.Hz redıo zina mision na target zake.Hata ukienda huko England,USA na Germany, zipo za aina hyo.BBC,DW,VOA ni radio za kipropaganda na ziko highly funded na mabeparı na pia zinasimamiwa na mashirika ya Kijasusi.Wanatafuta habari kwa gharama kubwa, mashirıka yetu hata ya taifa hayawezi mudu.
 
Mtangazaji Jerry Muro kuna wkt alikuwa anafanya kazi nzuri za kuelimisha wa Tz.Fund alipata wapi au ni ubunifu wake tu?
 
hahaha... word,thread za ngono zimewafanya baadh ya members kuwa maarufu km HEAVEN ON EARTH.hawakosi kuchangia ht iweje
 
hahaha... word,thread za ngono MMU zimewapa baadh ya members umaarufu km HEAVEN ON EARTH.wanachangia ht iwe 02.00am
 
Back
Top Bottom