John John Msakuzi
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 279
- 99
Akiongea na wanahabari, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Annamringi Macha amesema kuwa hadi kufikia mwaka 2025 chini ya Rais Samia, Dhahabu zenye uzito wa gramu 1,301,842.81 zenye thamani ya shilingi bilioni 134.78 zimeuzwa kupitia soko la madini la Mkoa, ambapo shilingi bilioni 9.43 zimekusanywa kama mrahaba na ada za ukaguzi.
Aidha, amesema leseni za wachimbaji wadogo zimeongezeka kutoka 126 mwaka 2020 hadi 573 mwaka 2025, jambo linaloashiria ongezeko la shughuli za uchimbaji na ushiriki mpana wa wananchi katika sekta ya madini, ikiwemo vikundi vya wanawake waliopata leseni za uchimbaji.
Aidha, amesema leseni za wachimbaji wadogo zimeongezeka kutoka 126 mwaka 2020 hadi 573 mwaka 2025, jambo linaloashiria ongezeko la shughuli za uchimbaji na ushiriki mpana wa wananchi katika sekta ya madini, ikiwemo vikundi vya wanawake waliopata leseni za uchimbaji.