RC Shigela: Wagonjwa wa Corona waliopatikana Zanzibar wakitokea Tanga huenda ugonjwa huo walipatia ndani ya boti au gatini Unguja

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
84,285
142,471
Mkuu wa mkoa wa Tanga mh Shigela amesema watu wawili walioripotiwa Zanzibar kuwa ni wagonjwa wa Corona waliotokea Tanga huenda maambukizi hayo waliyapata ndani ya boti au bandarini Unguja.

Shigela amesema wamezitembelea familia za wagonjwa hao jijini Tanga na kuzikuta zikiwa buheri wa afya hata hivyo wameziweka katika karantini kwa mujibu wa taratibu za nchi.

Naye mkuu wa wilaya ya Pangani amesema katika boti waliyopanda hao wagonjwa kulikuwa na abiria 6 na mmojawapo ni raia wa Ujerumani ambaye wanamfuatilia.

Source Eatv habari!
 
Hivi waziri mkuu si kakataza hawa watu kutoa toa habari za korona? Nini wasichomuelewa kwani?
 
Aache siasa asubir maturity (14 days) tena wakiwa karantini ili kunusuru maambukizi kwa wengine. Asiseme buheri wa afya akidhani Corona ni kama kujikwaa kwamba kidonda kitaonekana immediately....

Sent using Jamii Forums mobile app
Tayari wana zaidi ya siku 14 tangu last contact na muathirika, hao jamaa wameondoka Tanga tar 18 March, ni zaidi ya week mbili sasa, dalili zote zinaonyesha wameupatia Zenji au njiani kuelekea Zenji.
 
Huyu RC bure kabisa, sasa kipi anachojitetea, kwani ni dhambi kwa mkoa wake kuwa na wagonjwa wa corona hadi aanze kujitetea na kuleta hoja dhanifu tena za kienyeji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi mtu akiambukizwa ndani ya masaa matatu anainyesha dalili?

Inainyesha ugali umewekwa mbele zaidi kuliko utaalamu

E Ngai tusaidie
Mkuu hao watu walitoka Tanga siku nyingi zilizo pita kuanzia tarehe 18 March kurudi nyuma.
 
Hivi mtu akiambukizwa ndani ya masaa matatu anaonyesha dalili?

Inaonyesha ugali umewekwa mbele zaidi kuliko utaalamu

E Ngai tusaidie
dalili zinaanzia siku mbili hadi kumi na nne,sawa mke wa pili wa lisu
 
Hivi waziri mkuu si kakataza hawa watu kutoa toa habari za korona? Nini wasichomuelewa kwani?
Yaani Wanachofanya Ni Makosa Matupu
Wanaoruhusiwa Kuongelea Corona Virus Diseases 19
Na Kutoa Taarifa Kwa Umma Ni Hawa Tu:-
1. Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
2. Makamu Wa Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
3. Waziri Mkuu Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
4. Waziri Wa Afya
5. Msemaji Wa Serikali
 
Mkuu wa mkoa wa Tanga mh Shigela amesema watu wawili walioripotiwa Zanzibar kuwa ni wagonjwa wa Corona waliotokea Tanga huenda maambukizi hayo waliyapata ndani ya boti au bandarini Unguja.

Shigela amesema wamezitembelea familia za wagonjwa hao jijini Tanga na kuzikuta zikiwa buheri wa afya hata hivyo wameziweka katika karantini kwa mujibu wa taratibu za nchi.

Naye mkuu wa wilaya ya Pangani amesema katika boti waliyopanda hao wagonjwa kulikuwa na abiria 6 na mmojawapo ni raia wa Ujerumani ambaye wanamfuatilia.

Source Eatv habari!
Hivi hawa viongozi wamechanganyikiwa?...
Unajua Covid-19 sio mchezo...very stupid indeed

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zanzibar kujimwambafy kwingi, walitoa taarifa upesi upesi, pasipo kuishirikisha serikali ya muungano, na mabango katika rugha ya kingereza walidesign, kuitangazia dunia, wakahitimisha kuwa wametokanayo bara, na wazanzibari wakaanza mauzi kwa kutaka watanganyika kuzuiwa kuingia Zanzibar, kumbee yenyewe ndo kisima cha Corona. Stupid!
 
Back
Top Bottom