RC, RPC na RSO Morogoro mjiangalie

RC, RPC na RSO Morogoro mjiangalie

mmteule

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2011
Posts
6,035
Reaction score
15,064
Katika hali ya kusikitisha kwenye Mkoa wa Morogoro, Mkoa mkongwe wenye kamati ya ulinzi na usalama iliyotimia inawezekanaje kiwanda cha kutengeneza silaha kikawa mjini (Eneo la Masika) kwa muda mreeefu mpaka pale kilipovumbuliwa na askari wa TANAPA???? tena na kukutwa na shehena ya silaha.... Shame on youu!
Niliumia sana moyoni kuona habari hio via ITV, Ningekuwa na mamlaka hakika kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa ningepiga chini jana hiyo hiyo ili kuleta fundisho. Polisi wapo Morogoro, TISS wapo kila aina ya vyombo vya usalama vipo hivi mtawaeleza nini watanzania kwamba nini kiliwakwamisha kugundua chaka hilo la wahalifu. Nani alaumiwe, mjiangalie watanzania wa leo sio wa jana...tumewaona hata kama hamtawajibishwa!
 
Ukifanyika uchunguzi huru si ajabu ukakuta jamaa walikuwa wanapata malighafi kutoka ngerengere.
 
Hii gov utaumiza kichwa chako bure,unakuta wamevaa miwani kumbe ya mbao,ukiona limebumbuluka ujue kuna maslahi wametofautiana ki maslahi wakaunguzana,chezea bongo wewe.
 
Kati ya mambo yanayo rudisha Nchi hii nyuma ni kufuga wazembe.kwa vyovyote vile hawa jamaa walitakiwa wafutwe kazi.unakuta mtu kafanya uzembe wa kupindukia lakini bado analindwa kwa kuhamishwa kwenda mahali pengine.wana kila aina ya facilities za kufanyia kazi lakini mtu hawajibiki.
 
duh... usalama w taifa nao walikuwa wapi ?.

silaha, mabomu, tindikali.... nn kitafuata...? hii nch bwana.
 
Back
Top Bottom