RC Mbeya ateka Mafarisayo mchana kweupe

RC Mbeya ateka Mafarisayo mchana kweupe

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
16,099
Reaction score
24,338
Katika hali ya kushangaza ulimwengu, mkuu wa mkoa wa Mbeya ndugu Chalamila, amekusanya mafarisayo na masadukayo kuiombea na kuzindika ujenzi wa ofisi mpya Toya mkuu wa mkoa baada ya ile ya awali iliyojengwa na Wajerumani mwaka 1952 kuvunjwa.

Maajabu ni pale Sadukayo mmoja alipokuwa akisali akawa ananukuu vifungu vya Biblia akisema "Wale wanataja magari yao, farasi wao lakini sisi tunalitaja jina la jiwe" yaani wamefika pahala wanamfananisha Jiwe na Mungu, hiki ni kiburi cha uzima, na uzuri mafarisayo na masadukayo waliwakilisha dini zote, kwahiyo hapa nazunguzia Vatican na Mecca kasoro walokole siku hizi hawapo kwenye upuuzi huu zaidi ya hawa wanao jiita manabii na mitume.

Mungu atunusuru, tumevunja jengo ambalo lingeweza kuwa kivutio cha utalii tunafikiri utalii ni wanyama pekee, Spain, Italy, Morroco na uingereza wana watalii mara 10 ya tanzania lakini hakuna wanyama wengi kama huku , ni majengo
Watanzania wengi wakienda ulaya wamapiga picha na maghorofa tena kwa kulipa, huo ndio utalii, sisi tunavunja na kujenga majengo ya wachina ya slide window na tiles, shame om us!

Walishindwa vipi kujenga ofisi pajala pengone ama pembeni?
 
Nimeona kuwa watu wanao mpenda Mungu huchukiwa na waumini fake wanaoa mtaja Mungu wakiwa na shida.
 
Mimi niliishi Mbeya yangu ukoloni sikuwahi kusikia chifu wa Kinyakyusa Mbeya zaidi ya kina Lyoto. Kuna hawa wapya wanaojidai kuwa ni wazaliwa wa Mbeya! Hawa niwaongo si machifu halisi haiwezekani mnyakyusa wa Bulyaga ukawa chifu wa Mbeya. Kuna hawa mitume na manabii wapya na makanisa yao mapya, makanisa ya Mbeya yalikuwa Moravian, Katoliki, Anglikani, Seventhday, Jeshi la Wokovu na Mashahidi wa Yehova, kuna watu hapa watahoji KKKT! Haikuwepo kwani inafanana na Moravian hivyo ilikuwa jimbo la kaskazini na mashariki na Moraviani jimbo la magharibi na kusini, hivyo hawa manabii na mitume wanaojidai nao ni wa Mbeya hapana hawa ni wachuuzi toka maeneo mengine.
 
Mafarisayo na Wasadukayo walikuwa ni ‘wanasheria wasomi’ wabobevu kweli kweli, usiwafananishe na mambo ya kijinga.
 
Kabla ya kuvunja mlishapokea watalii wangapi kwenye hilo jengo.?
 
Mimi niliishi Mbeya yangu ukoloni sikuwahi kusikia chifu wa Kinyakyusa Mbeya zaidi ya kina Lyoto. Kuna hawa wapya wanaojidai kuwa ni wazaliwa wa Mbeya! Hawa niwaongo si machifu halisi haiwezekani mnyakyusa wa Bulyaga ukawa chifu wa Mbeya. Kuna hawa mitume na manabii wapya na makanisa yao mapya, makanisa ya Mbeya yalikuwa Moravian, Katoliki, Anglikani, Seventhday, Jeshi la Wokovu na Mashahidi wa Yehova, kuna watu hapa watahoji KKKT! Haikuwepo kwani inafanana na Moravian hivyo ilikuwa jimbo la kaskazini na mashariki na Moraviani jimbo la magharibi na kusini, hivyo hawa manabii na mitume wanaojidai nao ni wa Mbeya hapana hawa ni wachuuzi toka maeneo mengine.
Acha uzushi yaan morovian ilianza kabla kkkt wakat temple kwetu la kkkt limejengwa kipindi cha utawala wa kijeruman...kumbe hata hujui asili ya morovian
 
Back
Top Bottom